kakuruvi
JF-Expert Member
- Sep 2, 2009
- 770
- 256
Wana JF na wapenzi wote wa medani ya soka nawaletea taarifa ya kusikitisha kwamba Mchezaji wa zamani wa African Sports ya Tanga, Majimaji ya Songea, Mtibwa Sugar ya Morogoro, Mirambo ya Tabora na Reli Morogoro TWAHA OMARI (RIP) amefariki dunia jana katika hospitali ya Taifa Muhimbili mara tu baada ya kufikishwa kwa tatizo la shinikizo la damu.
Kwa mujibu wa habari za ndugu wa karibu mwili wa marehemu utasafirishwa leo mchana na mazishi yake yanatarajiwa kufanyika kesho nyumbani kwao huko Korogwe Tanga.
Kwa mujibu wa habari za ndugu wa karibu mwili wa marehemu utasafirishwa leo mchana na mazishi yake yanatarajiwa kufanyika kesho nyumbani kwao huko Korogwe Tanga.