Gurudumu
JF-Expert Member
- Feb 5, 2008
- 2,349
- 261
Leo tarehe 7 April, tukio muhimu lilikuwa ni wananchi kutoa maoni yao kuhusu Mswada wa kutunga sheria ya kutunga katiba mpya Tanzania. Binafsi nilitarajia kuona live coverage ya angalau tv mojawapo zilizopo tz
Asubuhi Star tv wakatangaza kwamba kuanzia saa tatu na nusu wataanza kurusha coverage live ya mjadala kutoka Dodoma ukumbi wa Msekwa. Muda ulipofika kwenye screen ikaandikwa kwamba ni live lakini kukawa kuna mjadala kati ya mtangazaji na mwanasheria fulani huko mwanza ambao uliboa sana. Muda fulani katika background wakaonesha watu kwenye ukumbi wa Msekwa wakiongea kuashiria kwamba mjadala umeshaanza lakini sauti hazisikiki. Kisha wakaaga wakaendelewa na vipindi vingine visivyo na tija.
TV zingine zilikuwa zinaendelea na ama tamthilia, muziki, na mambo mengine ambayo sikuona kama yalikuwa ya muhimu kwa watanzania kuliko mjadala wa public hearing zilizofanyika leo Dodoma, Zanzibar na Dsm.
Wakati huo huo, Citizen tv ya Kenya ilikuwa inafanya live coverage ya kesi ya wakenya iliyokuwa inasomwa kwa mara ya kwanza huko The Hegue. Wakati wa mchakato wa katiba mpya ya Kenya, nilifuatilia matukio mengi muhimu live kupitia tv za kenya, kwa kadri nilivyopata muda.
Tukumbuke kwamba live coverage ndiyo inayoaminika zaidi kuliko news clips ambazo zinaweza kuwa zimetomaswa kwa kutumia teknolojia ya kisasa. Taarifa za kilichokuwa kinajiri Dodoma zilisambaa haraka sana kupitia SMS na blogs. Kwa tv yeyote ambayo lengo lake ni kuhabarisha wananchi ingeunganisha mara moja live ili wananchi watazame na kusikia kinachotokea.
Binafsi ningefurahi sana kupata maelezo nini kilitokea na nini kitatokea huko mbele tukizingatia safari hii ya katiba mpya tz ndiyo kwanza tunaianza.
Asubuhi Star tv wakatangaza kwamba kuanzia saa tatu na nusu wataanza kurusha coverage live ya mjadala kutoka Dodoma ukumbi wa Msekwa. Muda ulipofika kwenye screen ikaandikwa kwamba ni live lakini kukawa kuna mjadala kati ya mtangazaji na mwanasheria fulani huko mwanza ambao uliboa sana. Muda fulani katika background wakaonesha watu kwenye ukumbi wa Msekwa wakiongea kuashiria kwamba mjadala umeshaanza lakini sauti hazisikiki. Kisha wakaaga wakaendelewa na vipindi vingine visivyo na tija.
TV zingine zilikuwa zinaendelea na ama tamthilia, muziki, na mambo mengine ambayo sikuona kama yalikuwa ya muhimu kwa watanzania kuliko mjadala wa public hearing zilizofanyika leo Dodoma, Zanzibar na Dsm.
Wakati huo huo, Citizen tv ya Kenya ilikuwa inafanya live coverage ya kesi ya wakenya iliyokuwa inasomwa kwa mara ya kwanza huko The Hegue. Wakati wa mchakato wa katiba mpya ya Kenya, nilifuatilia matukio mengi muhimu live kupitia tv za kenya, kwa kadri nilivyopata muda.
Tukumbuke kwamba live coverage ndiyo inayoaminika zaidi kuliko news clips ambazo zinaweza kuwa zimetomaswa kwa kutumia teknolojia ya kisasa. Taarifa za kilichokuwa kinajiri Dodoma zilisambaa haraka sana kupitia SMS na blogs. Kwa tv yeyote ambayo lengo lake ni kuhabarisha wananchi ingeunganisha mara moja live ili wananchi watazame na kusikia kinachotokea.
Binafsi ningefurahi sana kupata maelezo nini kilitokea na nini kitatokea huko mbele tukizingatia safari hii ya katiba mpya tz ndiyo kwanza tunaianza.