Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,709
Kama umeisoma Qur'an inakwambia:
Qur'an 21: 7. Na kabla yako hatukuwatuma ila watu wanaume tulio wapa wahyi (ufunuo). Basi waulizeni wenye ilimu ikiwa nyinyi hamjui
Qur'an 16: 43. Nasi hatukuwatuma kabla yako ila watu wanaume tulio wapa Wahyi (Ufunuo). Basi waulizeni wenye ukumbusho kama nyinyi hamjui
Sasa kijana, unaweza kusoma na usielewe, ni wapi pa kuuliza?
Njia mojawapo rahisi ni hiyo ya kutazama Waislam na kuwaona na kuwasikia na kuwauliza. Ilmu ya Qur'an ni bahri kubwa sana isiyo na mwisho na wala hutamkuta Alim yeyote akakwambia kuwa mimi nimemaliza kila kilichomo kwenye Qur'an kuna specialty zake humo na kuna watu wanabobea kaka hayo.
Nakupa ushauri tu, ikiwa unataka kujuwa Uislam jifunze zaidi kutoka kwa Waislam.
Nakutakia utazamaji mwema.
Si ni Quran hii hii ambayo inadai kuwa rahisi kueleweka?
Sasa kama ni hivyo,yanini tena kutafuta watu wanieleweshe kitu ambacho ni rahisi kueleweka?