TV 1 (Viasat 1) majangaa

TV 1 (Viasat 1) majangaa

Na wewe hutumii akili tatizo lenu watanzania hamtaki mabadiliko na ushindani sasa mlitaka waje na style gani ya habari uccm na ucdm?mimi nimewatizama sana na naendelea kuwatizama inaonekana hawataki mlengo wa kushoto wa kulia wanakuja na stori zinazogusa maisha ya watu hata hivyo hiki ni kituo kipya nini maana ya kuja mpya kwenye market na kitu kinachofanana na wenzio?

Hiii tv imekuja na mtizamo wa tofauti tuwape muda tuendelee kuangalia ni kitu gani kipya watafanya umenishangaza unayesema sauti za maripota kama kina ufoo saro na jacquline mselemu wa itv wewe kweli box sasa hao uliowataja ndio umeona maripota bora kwa kuongea sauti za kichaga?Kwani hao walianzia wapi jamani huyo ufoo saro huwezi kumlinganisha sauti yake na ripota wao zainab nani sijui sauti kama BBC.Jifunze kuappreciate mtu akifanya kitu kizuri majungu waachie CCM na CDM.

Sio lazima A kuwa B unataka habari zinazofanana ukiangalia ITV,TBC,EATV kitu kilekile?

Tujifunze kuukubali ushindani jamani kiukweli wanafanya vizuri hilo halina ubishi japo wanatakiwa kurekebisha baadhi ya mambo ninaamini na wao wanapitia mitandao hii kuona comments fanya constructive critisicm yako naamini wana uongozi na watayafanyia kazi maoni yako. Acheni fitna wabongo bwanaa nomaaaa.
 
Jana ilikua mara yao ya kwanza kurusha taarifa ya habari nilichokiona:;

Muonekano wa studio:
Jamani muonekano bado hauna mvuto jaribuni kuboresha kidogo halafu anayechukua picha ya mtangazaji anamvuta sana karibu hata mikono haionekani??

mtangazaji:
mtangazaji alikua hajiamini kabisa style yake ya kurudiarudia neno kama kigugumizi inapoteza mvuto..yule dada alikua na hofu sana.halafu akikosea anacheka./tabasam.labda hajazoea kamera tunategemea siku zijazo atafanya mazoez ya kutosha..na jwa wenngine pia..

mpangilio wa habari:
Jamani habari zenu ni nzuri ila hazina mvuto sababu zinakua ndefu sana..mfano ile habari ya madawa ya kulevya ilikaribia dk 4. ike ya umeme nayo..halafu chambueni habari ambazo zina mashiko..mfano kuna habari ambazo zinahit mtaani na kwenye mitandao ya.kijamii au ulimwenguni tunategemea kuzisikia kwa kina lakin hamkua nazo..mfano ishu ya bunge la katiba lililoanza leo, mkutano wa wasomi n.k ambapo habar hizi zilitanganzwa na karibu vituo vingine vyote..

maripota wenu/ waandishi:
jamani ni heri mngechukua waandishi wazoefu wanaoweza kutafuta strong news.na wenye haiba ya kutangaza habari kama kina ufoo saro..jacline silem hemed kivuyo george marato wa itv samadu hassan n.k n.k yaani mpaka msikilizaji huchoki kuisikiliza habari kwa jins mtangazaj anavyotangaza..kuna huyo sijui ndo zuberi hasaan alitangaza habar kama 4 yaan mpaka unasema kitu gani jamani..

Habari za Africa ni habari 1 kimataifa ndo kabisaa..jamani rekebisheni hapa chukueni aljazeera bbc n.k ma news yamejaa mbona wengine kama star tv au tbc 1 wana mahabar kibao ya kimataifa na yana mtu alieandaa kamakala fulani hivi kanavutia..na wanacopy aljazeera ama bbc cnn n.k

habari za michezo:
mimi ni mdau mzuri wa michezo na nijuavyo habar za michezo zina lugha zake na ucheshi wake..so hata mtangazaji anatakiwa kuwa na machachari fulani hivi jamani yaani awe mdau wa michezo kama kina maulid kitenge. n.k
mtangazaji huyohuyo kusoma habari zote mwanzo mwisho haina mvuto jamani angalao kitaifa, africa na kimataifa awe mwingine; biashara awe mwingine hali kadhalika michezo..
sasa habari zenu za michezo zimebezi kitaifa tuuu sikuona kimataifa jamanii..halafu kama jana mliona ile ya ngumi tuu hamkuona hata zinginezinginee!!?

mwisho:;
mmejitahid sana ila tunawategemea na mlivyosema vituo vingine wajipange duu nkasema hebu nione moto wenu kumbe umekua mdogo sana..nawaombeni bas jamani mfanyiefanyie kazi hayo maoni yangu..nadhani tv 1 itakua favourate kwangu pia so msiniangushe..
Jamani samahanini sana sina taaluma ya uandishi ila haya ni kwa mtazamo wangu tuu..
Mbarikiwe...
Ulivyomtaja tu George Maratu eti naye ni mtangazaji mahiri nimeona thread yako nzima ni ya kipuuzi kabisa.

Mimiii ni Goooorgeeeeee Maratoooooooooo Itveeeeeeeeeeeeee Musomaaaaaaaaaaaaaaaa.

Huu kama si uzuzu ni nini?
 
Back
Top Bottom