Inajulikana kama Ibrahimu prize, ni zawadi ya fedha
taslimu ambazo hupewa Kiongozi wa mweusi wa Kiafrika atakayeshinda kulingana na vigezo vilivyowekwa (na huyo Mwarabu na Wazungu kama Bill Clinton), inanikumbusha mchezo wa masumbwi promota na kocha Mzungu ila wanaochapana uwanjani na kuumizana ni sisi
Niga!
Ikumbukwe kwamba ukimuuliza mtu wa Algeria au Tunisia kuhusu Mo Ibrahimu atakwambia ndiyo mdudu gani ,
lkn hapa kwetu kwa Waafrika weusi ndiyo tumegeuza kuwa kigezo cha maisha yetu na kwamba huyo Mwarabu ndiyo anaamua ni yupi kiongozi bora wa Bara giza na yupi siyo, na sisi tunachekelea, ni kama vile mtoto mdogo (
sisi Waafrika Dunia inachukulia kama watoto wadogo) unaambiwa ukirudi Shule fanya mazoezi aliyokupa Mwalimu usome, ukimaliza jioni uoge, ule halafu ulale usisahau kutayarisha sare zako za kesho asubuhi nikija jioni nikikuta umefanya vizuri nitakununulia zawadi ya nguo na viatu vizuri wkt wa Idi au Krismas usipofanya hivyo hakuna zawadi krismasi au Idi umesikia mwanangu? Sisi tuna jibu sawa baba!
,,The Mo Ibrahim Foundation gives multimillion-dollar awards to African leaders who stay honest, promote democracy—and relinquish power".