Mvaa Tai
JF-Expert Member
- Aug 11, 2009
- 6,157
- 4,454
Wadau jana nimesikia katika habari za jioni za BBC kwamba nchi wanamotoka wale vijana wanne watuhumiwa wa mlipuko wa Bomu Arusha, wanaitaka Tanzania iwaombe radhi kwa kuwachafua na kuwasababishia usumbufu, Tanzania isipofanya hivyo watavunja uhusiano wa kibalozi na nchi yetu. Je;-
1. Ni utaratibu wa vyombo vya usalama kumtaka radhi mtu au nchi anayotoka kwa kumtuhumu?
2. Hizo nchi hazijawahi kuwatuhumu Watanzania kwa uharifu hata mara moja na kuwakuta hawana hatia?, kama imewahi kutokea walitutaka radhi?
3. Hizi tuhuma kwa hawa vijana zina uzito wa kuvunja uhusiano wa Kibalozi baina ya nchi na nchi iwapo hawatatakwa radhi?
Naishauri Serikali iwatake radhi haraka iwezekanavyo hizi nchi kama ina utaratibu wa kuwataka radhi suspects wote wa uharifu ambao baadaye wanagundulika hawakuhusika, isifanye hivyo kwasababu imetishiwa kuondolewa uhusiano wa kibalozi
1. Ni utaratibu wa vyombo vya usalama kumtaka radhi mtu au nchi anayotoka kwa kumtuhumu?
2. Hizo nchi hazijawahi kuwatuhumu Watanzania kwa uharifu hata mara moja na kuwakuta hawana hatia?, kama imewahi kutokea walitutaka radhi?
3. Hizi tuhuma kwa hawa vijana zina uzito wa kuvunja uhusiano wa Kibalozi baina ya nchi na nchi iwapo hawatatakwa radhi?
Naishauri Serikali iwatake radhi haraka iwezekanavyo hizi nchi kama ina utaratibu wa kuwataka radhi suspects wote wa uharifu ambao baadaye wanagundulika hawakuhusika, isifanye hivyo kwasababu imetishiwa kuondolewa uhusiano wa kibalozi