Tuwasamehe mafisadi wote tuanze upya

Godwine

JF-Expert Member
Jan 15, 2010
1,371
281
Nadhani imefika wakati tuchore mstari wa kuanza kujenga taifa jipya lisilokuwa na visasi wala malipiziano ya makosa yaliyofanywa na mtu siku za nyuma.Tuwafungulie wafungwa wote na tusamehe kesi zote zinazoendeshwa ili taifa libaki jeupe na lenye mshikamano.Tuweke sheria kali kwa wataofanya makosa mapya kuanzia kipindi hiki. lakini kama mtu aliiba fedha nyingi za serikali na kuzificha nje ya nchi basi tumwamulu azileta na kuwekeza nchini kwetu kwa manufaa ya uchumi wetu. Nadhani kwa mwendo huu baada ya miaka 5 taifa litakuwa mbali kwani kuna takribani trion zaidi ya 9 zilizofichwa na mafisadi nje ya nchi ambazo zikiingizwa kwenye uchumi Tanzania itakuwa kwa kasi na wananchi wengi watanufaika.
 
Ni wazo au niseme ni mpango mzuri kinadharia tu,kivitendo mkuu watakufisadi adi wewe kuna watu atawakisamehewa watajipanga upya kwa ufisad wa kiufundi zaidi wasistukiwe.
 
Ni wazo au niseme ni mpango mzuri kinadharia tu,kivitendo mkuu watakufisadi adi wewe kuna watu atawakisamehewa watajipanga upya kwa ufisad wa kiufundi zaidi wasistukiwe.

​kama tukitaka taifa lirudi kwenye umoja na mshikamano na kupunguza mifarakano isiyo na maana basi ni wakati muafaka katika kuachana na mambo yaliyopita na kupange yajayo
 
Utawasamehe vipi watu amabao hawajitambui na kutambua vitendo vya vya KIFASADI.
 
Waturudishie vyetu walivyotuibia ndipo tuwasamehe. Wewe umelenga kuwalinda mafisadi kwani nahisi una maslahi nao; kwani toka juzi thread zako zimekaa mkao wa kutaka kuwaondoa wale wanaopinga uwizi na ufisadi wa mali za umma waondolewe nchini.
 
Waturudishie vyetu walivyotuibia ndipo tuwasamehe. Wewe umelenga kuwalinda mafisadi kwani nahisi una maslahi nao; kwani toka juzi thread zako zimekaa mkao wa kutaka kuwaondoa wale wanaopinga uwizi na ufisadi wa mali za umma waondolewe nchini.
sio kwamba ninamaslahi na mafisadi lakini ningependa taifa liwe pamoja na kuanza kujenga uchumi kwani wakati taifa likilalamika na upungufu wa mitaji lakini watu wamechimbia chini magunia ya fedha na wengine wakizificha kwenye mabank ya nje. tukiendelea hivi basi uchumi wetu utadumaa na tunaelekea na mwanguko mkubwa wa uchumi wakati wananchi wetu wamechimbia mitaji mikubwa kwa hofu ya kuandamwa....tufike wakati tuache kufikiri visasi ndio njia ya kujenga taifa bali ni umoja wa kitaifa
 
Inabidi tuombe moderator watengeneze button ya invite. Ningependa nione mchango wa member anaitwa fairplayer juu ya hii hoja .
 
Nadhani imefika wakati tuchore mstari wa kuanza kujenga taifa jipya lisilokuwa na visasi wala malipiziano ya makosa yaliyofanywa na mtu siku za nyuma.Tuwafungulie wafungwa wote na tusamehe kesi zote zinazoendeshwa ili taifa libaki jeupe na lenye mshikamano.Tuweke sheria kali kwa wataofanya makosa mapya kuanzia kipindi hiki. lakini kama mtu aliiba fedha nyingi za serikali na kuzificha nje ya nchi basi tumwamulu azileta na kuwekeza nchini kwetu kwa manufaa ya uchumi wetu. Nadhani kwa mwendo huu baada ya miaka 5 taifa litakuwa mbali kwani kuna takribani trion zaidi ya 9 zilizofichwa na mafisadi nje ya nchi ambazo zikiingizwa kwenye uchumi Tanzania itakuwa kwa kasi na wananchi wengi watanufaika.

Usiwasemee mkuu,waje mbele zetu,wakiri kwamba wao ni mafisadi,watubu tena kwa machozi na kurejesha walivyo kwiba,
sidhani kama binadamu yeyote atashindwa kusamehe!
Shida ni fisadi gani yupo tayari kuachia ukwasi wake?
 
sio kwamba ninamaslahi na mafisadi lakini ningependa taifa liwe pamoja na kuanza kujenga uchumi kwani wakati taifa likilalamika na upungufu wa mitaji lakini watu wamechimbia chini magunia ya fedha na wengine wakizificha kwenye mabank ya nje. Tukiendelea hivi basi uchumi wetu utadumaa na tunaelekea na mwanguko mkubwa wa uchumi wakati wananchi wetu wamechimbia mitaji mikubwa kwa hofu ya kuandamwa....tufike wakati tuache kufikiri visasi ndio njia ya kujenga taifa bali ni umoja wa kitaifa

godwine;
hata kama huna maslahi nao lkn kwa hawa viongozi tulionao sasa hakuna chenye manufaa kitakachofanikiwa kwani wote walishakosa uzalendo na nchi yao. Kumbuka mtu anapoanza ulevi anaanza na moja, mbili, tatu, nne, na mwisho anakuwa na uwezo wa kunywa hata kreti 3 kwa siku, kwani tayari ulevi umeshakuwa sehemu ya maisha yao. Ni sawasawa na ufisadi, kwani waliponza ni taratibu tu lkn with time sasa wamekubuhu na uwizi na ufisadi wa mali za umma umekuwa sehemu ya maisha yao ya kila siku na hakika utafanyaje, mtu kama huyu ni vigumu sana kumwongoa.

Ni wazo zuri kwamba tuanze upya kama taifa, lkn nachelea kusema kwamba kwa mfumo uliopo sasa na aina ya viongozi tulionao naamini kabisa si rahisi kufanikiwa.

Godwine, mimi nakupa neno langu leo hii kwamba kwa hawa viongozi wetu wa sasa, kufikia 2015 nchi yetu itakuwa na hali mbaya sana kiuchumi na kijamii.
 
Nadhani imefika wakati tuchore mstari wa kuanza kujenga taifa jipya lisilokuwa na visasi wala malipiziano ya makosa yaliyofanywa na mtu siku za nyuma.Tuwafungulie wafungwa wote na tusamehe kesi zote zinazoendeshwa ili taifa libaki jeupe na lenye mshikamano.Tuweke sheria kali kwa wataofanya makosa mapya kuanzia kipindi hiki. lakini kama mtu aliiba fedha nyingi za serikali na kuzificha nje ya nchi basi tumwamulu azileta na kuwekeza nchini kwetu kwa manufaa ya uchumi wetu. Nadhani kwa mwendo huu baada ya miaka 5 taifa litakuwa mbali kwani kuna takribani trion zaidi ya 9 zilizofichwa na mafisadi nje ya nchi ambazo zikiingizwa kwenye uchumi Tanzania itakuwa kwa kasi na wananchi wengi watanufaika.

Wanao kutuma wanakutumia vibaya!
Si ni wewe uliyekuja juzi hapa na kubwata eti watu wote wanao tumia vichwa vyao vizuri kufikiri kama dr wa Ukweli na wenzake eti wanyang'anywe uraia?Halafu bila aibu leo unasema tusameheane!
Waambie wafanye hima kutafuta hifadhi nje maana siku zao zinahesabika!
Sawa eeeeeeeeeeh!
 
Back
Top Bottom