Tuwakomboe waumini wa kanisa la Gwajima

Tuwakomboe waumini wa kanisa la Gwajima

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
16,255
Reaction score
16,185
Waumini wa kanisa la Gwajima ni watanzania wenzetu ambao wametekwa kiimani. Wanahitaji kukombolewa kutoka kwenye kadhia hii.

Waumini hawa wanatumiwa kama vitega uchumi na ngao ya binadamu dhidi ya watu wajanja wanaofanikisha ajenda zao kupitia kwao.

Taarifa zilizothibitishwa na DC Msando zinaonyesha kuwa viongozi hawa "matepeli" wanawachangisha waumini hawa pesa nyingi wakiwadanganya kuwa wanalipia sehemu ya kufanyia ibada baada ya makanisa yao kufungwa kumbe wanadanganya. Njaa zao zinawasukuma maumini wao waingie kwenye mgogoro na serikali.

Kusudi lao kuu ni sadaka sio kuabudu. Serikali waokoeni watu hawa maana iko siku mtajilaumu sana kwa kuchelewa kuchukua hatua.


View: https://youtu.be/0ePWwrQY49k?si=II5FhZYuKBmFH0Ul
 
Watajua mwenyewe , wakombolewe na Yesu , yeye akishindwa sisi ni nani mpaka tuweze?
 
Watajua mwenyewe , wakombolewe na Yesu , yeye akishindwa sisi ni nani mpaka tuweze?
Hawa ni raia wa Tanzania wanaofanana kabisa na wale waumini wa Askofu Kibwetere. Hawa ni waumini ambao wanatumiwa vibaya na akina Gwajima. Wanapokea maagizo halali na haramu kutoka kwa Gwajima. Je, serikali iko tayari kuona raia wake wako hatarini kwa kiasi hicho. Gwajima anaweza kuwapa amri ya aina yoyote dhidi ya serikali watu hawa na yeye akajificha katikati yao ili asichukuliwe hatua.
 
Hawa ni raia wa Tanzania wanaofanana kabisa na wale waumini wa Askofu Kibwetere. Hawa ni waumini ambao wanatumiwa vibaya na akina Gwajima. Wanapokea maagizo halali na haramu kutoka kwa Gwajima. Je, serikali iko tayari kuona raia wake wako hatarini kwa kiasi hicho. Gwajima anaweza kuwapa amri ya aina yoyote dhidi ya serikali watu hawa na yeye akajificha katikati yao ili asichukuliwe hatua.
Yesu aliowafufua kutoka wafu anashindwa vipi kuwaokoa ? Zipo shuhuda za hao waumini wakikiri maajabu ya yesu , hivyo wamwombe awachomoe kwenye kizaa zaa , mimi naogopa kutekwa bwashee
 
Back
Top Bottom