Tutawatimua madiwani - Slaa

hiyo tume ya Marando ipewe muda zaidi ihoji na wananchi pia ili kuona wana maoni gani?
ingesaidia katika kutoa decision sahihi
 
Mwanzoni nilikuwa na imani na CDM, lakini kwa mwenendo wao naona wananikatisha tamaa.
Hii habari ya muafaka tuliisikia kwenye vyombo vya habari kipindi, na hakuna kiongozi wa juu aliyekanusha. Baada ya muheshimiwa Lema kupinga hadharani ndio tunasikia kauli za viongozi wa juu.!:israel:
 
Mwanzoni nilikuwa na imani na CDM, lakini kwa mwenendo wao naona wananikatisha tamaa.
Hii habari ya muafaka tuliisikia kwenye vyombo vya habari kipindi, na hakuna kiongozi wa juu aliyekanusha. Baada ya muheshimiwa Lema kupinga hadharani ndio tunasikia kauli za viongozi wa juu.!:israel:
Ukiona hivyo jua Chadema makao makuu huwa hawakurupuki.
 
habari toka cdm arusha ni hivi mala amechemsha yeye kama mwenyekiti wa madiwani ndiyo kacheza mchezo wote kawadanganya wenzake katibu mkuu kawaambia waingie kwenye muafaka . Sasa kila diwani amejiandaa kujitetea yeye anawashawishi wasijieleze
kwani kina marando hawajawapigia kura ya udiwani ila wananchi warudishe kadi wajiunge ccm uchaguzi urudiwe wanauhakika wa kushinda
 
Wacheni kuzuga, mtimueni mwenyekiti wenu aliyekaa na Pinda wakakubaliana. Kumbuka, hao madiwani wamechaguliwa na wananchi na si Slaa. Mwenyekiti wenu alichaguliwa na nani kama si kurithishwa kiti na baba mkwe?Kisha kosea step akubali makosa na msiwatupie madiwani, madiwani labda muwape mshiko wa kutosha wakae kimya, mkiwabughudhi watasema ukweli. Msilalamike baada ya hapo. Sasa naamini yule aliesema cdm itakufa kabla 2015. Tunayaona.

Faiza naomba elimu yako,
 
Niliposikia habari ya muafaka wa Arusha, sikupenda kuchangia kutokana na mazingira ya mgogoro wenyewe na msimamo ulioonyeshwa na CDM toka mwanzo. Niliona kama viongozi wa CDM hawakuwashirikisha wananchi-japo hata kwa taarifa tu kabla ya kutangaza muafaka. Out of blue, tukaambiwa mgogoro umetatuliwa kwa muafaka. Kilichochanganya zaidi, hata baada ya kutangazwa kwa muafaka, viongozi wakuu wa CDM walikuwa kimya mpaka Lema(MP) alipotoka na tamko lake.

Kwa hili la viongozi wa CDM kuchelewa kutoa uamuzi kwa jambo zito kama la Arusha,wamepwaya sana, pia wamewayumbisha wanachama na mashabiki wa CDM. Jambo kama hili lisijirudie tena, kulingana na maadili na msimamo wa chama, nyeupe yafaa kuwa nyeupe na nyeusi kuwa nyeusi. La sivyo tutajikuta njiapanda kama magamba ambao hawajui wafanye nini na mapacha 3.
 
Imani yangu kwa CDM imerudi. Ni bahati mbaya kwamba walichelewesha kutoa tamko, lakini labda walihitaji kukutana kujadili.

Cha muhimu sana ni kwamba sasa tunajua Dr. Slaa na viongozi wa juu wa CDM hawakufanya kosa hili. Bado ni watu thabiti, wenye msimamo.
 
Pembetatu ya Ushindi isipojengwa jumba huporomoka. Labda tukumbushwe, wakati wa makubaliano ya kuendesha Halmashauri ya Kigoma mjini baada ya uchaguzi wa 2005 uongozi wa Taifa ulikuwa na nafasi gani hadi ikakubaliwa kukawa na zamu za kuongoza? Au ulikuwa ni uamuzi wa local party pale?

Precedence ya maridhiano ipo sasa ilifuatwa? kwa sababu japo issues ni tofauti kwa kiasi nadhani ile ya Arusha ilihitaji zaidi uongozi na ushiriki wa Taifa kuliko ile ya Kigoma.
 
Precedence ya maridhiano ipo sasa ilifuatwa? kwa sababu japo issues ni tofauti kwa kiasi nadhani ile ya Arusha ilihitaji zaidi uongozi na ushiriki wa Taifa kuliko ile ya Kigoma.

Tatizo kubwa sio namna walivyoridhiana. Ni maridhiano yenyewe. Hata kama CDM Taifa wangekuwa wamebariki bado tungesikitishwa. Walikufa watu Arusha, kwa kupigania haki. Viongozi wa dini Arusha walikataa kumtambua Maya, kwa vile hakuchaguliwa kwa haki.

Mie nimesema imani yangu kwa Chadema imerudi kwa vile sasa nimeelewa UJINGA huu haukufanywa na CDM Taifa. Ulifanywa na wachache, na baada ya uchunguzi tutafahamu kama walirubuniwa.
 
Hongera Chadema Taifa nadhani mko makini mngekurupuka kuunga mkono ingekula kwenu heri kulaumiwa kwa kuchelewa kutoa tamko kuliko kulaumiwa kwa kuwasaliti wana Arusha big up.
 
Itabidi taifa lishuhudie VITENDO vya CDM kuendelea kumsusia Gaudence Lymo. Madiwani wa CDM (ukiondoa hao WATATU waliopotoka) wasishirikiane na Lymo, na wasihudhurie vikao vyovyote atakavyoitisha.
 
Pembetatu ya Ushindi isipojengwa jumba huporomoka. Labda tukumbushwe, wakati wa makubaliano ya kuendesha Halmashauri ya Kigoma mjini baada ya uchaguzi wa 2005 uongozi wa Taifa ulikuwa na nafasi gani hadi ikakubaliwa kukawa na zamu za kuongoza? Au ulikuwa ni uamuzi wa local party pale?

Precedence ya maridhiano ipo sasa ilifuatwa? kwa sababu japo issues ni tofauti kwa kiasi nadhani ile ya Arusha ilihitaji zaidi uongozi na ushiriki wa Taifa kuliko ile ya Kigoma.

Dhanna ni haraam.
 
Natabiri anguko la CHADEMA. Nilikuwepo Marando alipoikaanga NCCR Mageuzi hadi ikaisha, akawaachia kina Mbatia wakikusanya majivu. Nilidhani watu walijifunza, kumbe bado. Kwa heri CHADEMA. Kitakachotokea mkishawafukuza uanachama hao 3, watajiunga CCM na kugombea tena udiwani kwenye uchaguzi wa marudio na watashinda kwa kishindo, kisha Halmashauri inarudi CCM na watu walewale. Najua kuna moto mwingine miongoni mwa wabunge. You were warned.
Ungekuwa na mtazamo mpana labda ndugu yangu ungeona madhara yaliyopo ccm ni makubwa kiasi gani ili tuendelee kuyapiga vita. Hapa ndio tunaona PEOPLE'S POWER wanakuwa kisiasa kwa asilimia kubwa kuliko ccm. Ni mangapi hapa JF mnaomba majibu ccm lakini hamjibiwi mnaambiwa ni siri, uongozi wa chadema msisite kuchukua maamuzi itakapoonekana kuna mazingira ya ushawishi wa rushwa. Kwanza kumbuka siasa au uongozi wowote wa kubebana ni mbaya sana kwa sababu huwezi kumnyoshea mwenzio kidole hata kama atafanya madudu makubwa kiasi gani. Na ndio maana ccm imeshikwa na kigugumizi kupangua maovu yaliyopo kwa sababu kila mmoja anajua madhambi ya mwenzie. Ni afadhali muwe wachache ambao mnaweza kuwa na ushirikiano kuliko kuwa na lundo ambalo halina faida.

Kama chadema hawatakuwa makini ina maana tutarudi kule kule waliko ccm na uongozi wa kubebana. Wanaposema eti wanataka maendeleo na kuijenga manispaa ya Arusha inabidi tutambue ni mambo gani tunayapiga vita siku zote. Kitu cha kwanza ni haki kwa wote na haki inapatikana ndani ya sheria, na sheria zinapatikana ndani ya hiyo jamii husika sio mtu anajitungia mwenyewe nyumbani.

Pili tukumbuke Tanzania yetu inahitaji juhudi kubwa sana katika kubadilisha mfumo uliopo wa kuchekeana, kindugu, kishangazi, kimjomba nk ili ielekee kwenye mstari wa sheria. Hawa madiwani wa chadema walifanya makosa kutangaza haraka bila kuwafahamisha uongozi wa juu ili kutoa tamko la pamoja. Sioni kama uongozi wa chadema una makosa kwa sababu walikuwa wanasubiri ripoti ya majadiliano yao kabla ya kutangaza muafaka.
 
Back
Top Bottom