CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kipo tayari kuwapoteza madiwani wake watatu waliohusika kumaliza kinyemela mgogoro wa kumpata meya wa Manispaa ya Jiji la Arusha, kwa maridhiano ya kugawana madaraka.
CHADEMA imeunda kamati ya watu watatu inayoongozwa na mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho na mwanasheria mkongwe, Mabere Marando, kufanya uchunguzi wa utaratibu uliotumika kufikia maridhiano hayo.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa, alisema maridhiano yaliyofanyika kumpata meya na naibu wake hawayatambui kutokana na upungufu uliojitokeza wakati wa mchakato wa kuwapata viongozi hao.
Madiwani wa CHADEMA wanaodaiwa kukubali kufanya maridhiano ni pamoja n Diwani Estomih Mallah, ambaye atashika nafasi hiyo kuanzia sasa hadi mwaka 2014 atakapomwachia nafasi Diwani wa TLP, Michael Kivuyo, wengine ni John Bayo na Efatha Nanyaro.
Akifafanua upungufu huo, Dk. Slaa alisema kwanza maridhiano hayo hayakufikiwa na idadi ya wajumbe (madiwani) ambao wanaweza kufanya maamuzi, kwamba maridhiano hayo yalifanywa na wajumbe tisa kati ya 21 ya madiwani wote wa halmashauri hiyo.
Aliutaja upungufu mwingine kuwa mkurugenzi wa halmashauri ya jiji hilo alikubali kufanya muafaka bila ya kupata barua ya CHADEMA ya kukubali maridhiano ambayo ina majina ya walioteuliwa na chama hicho kupewa madaraka.
Aliongeza kuwa madiwani wa CHADEMA, watatu walioshiriki kwenye maamuzi husika walifanya hivyo bila kuwashirikisha viongozi wao wa wilaya, mkoa na makao makuu kwa ajili ya kupata baraka zao za kupendekeza majina ya watakaochaguliwa kuwa viongozi.
Alisema upungufu mwingine ni kuwapo kwa mianya ya rushwa ya kuwashawishi madiwani husika kushiriki kwenye maridhiano hayo pasipo kufuata taratibu zinazotakiwa.
Dk. Slaa alisema kutokana na matatizo hayo, CHADEMA haiyatambui maridhiano hayo na kudai kuwa yamefanywa kwa kupindisha kanuni na taratibu za kuwapata viongozi hao.
CHADEMA tunasema kuwa hatuyatambui maridhiano yaliyofikiwa kumpata meya na naibu wake kwani hayakufuata kanuni na taratibu za kuwapata uliofanyika pale ni uchakachuaji wa demokrasia, alisema Dk. Slaa.
Katibu Mkuu huyo alisema chama chake kipo kwa ajili ya kusimamia haki na kwamba kipo tayari kupoteza nafasi ya unaibu meya wa miaka minne aliopewa diwani wake na nafasi nyingine za mwenyekiti wa fedha na elimu.
Tunajua kuwa posho ni tamu sana na hili wamekuwa wakilisema madiwani wetu hawa mara kwa mara lakini chama chetu hakiangalii masilahi ya wachache, kipo kwa ajili ya kutetea haki na usawa wa Watanzania, alisema.
Dk. Slaa alisema kuwa msingi wa mgogoro huo ulianza tangu Desemba mwaka jana hadi chama chao kuomba maandamano ya amani ambayo yaliingiliwa na poslisi waliowajeruhi na kuwaua baadhi ya walioshiriki.
Alisema kama madiwani hao waliamua kufanya maamuzi hayo kwa kuangalia posho bila kuangalia msingi wa mgogoro huo, chama chao kinawachukulia hatua baada ya kuthibitisha yaliyotokea katika maridhiano.
Kiongozi huyo alisema kama chama hicho kila siku kinaikosoa serikali ya CCM na wanachama wake, kipo tayari kufanya maamuzi magumu ya kuwawavua madaraka madiwani wake na kurudia uchaguzi upya.
Dk. Slaa alisema CHADEMA kama chama kingine, hakina watakatifu hivyo kipo tayari kurudiwa kwa uchaguzi wa baadhi ya kata, kama wananchi wa jiji hilo wanavyotaka, kutokana na mgogoro wa umeya ulivyo.
Alisema kamati aliyoiunda ambayo ninaongozwa na Marando, itakayofanya kazi kwa siku sita na baadaye kupeleka ripoti yake kwa kamati kuu na vivyo hivyo, viongozi wa wilaya na Mkoa wa Arusha kupeleka ripoti hiyo kwa ajili ya kutoa hukumu ya haki.
Kabla ya CHADEMA kutoa msimamo wake kama chama, Mwenyekiti wa chama hicho, ambaye pia ni Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe na Mbunge wa Jimbo la Arusha, Goodbless Lema, walinukuliwa na vyombo vya habari kuwa hawayatambui maridhiano hayo.
MY TAKE!
Wale CCM waliokuwa wanatumia nafasi hii kumshataki LEMA kwa wananchi sasa wameumbuka. Lema hakushiriki kuuuafiki muafaka wa arusha na alikuwa bungeni dodoma jamaa wakachukua advantage. However Diwanoi Nanyaro Efatha alishakuja hapa akasema yeye alishiriki kwenye hatua za mwanzo kama mwenyekiti wa BAVICHA mkoa hila hakutilia saini maridhiano ya mwisho na aliyapinga vikali with open eyes. LETS WAIT AND SEE KAMATIO YA MARANDO.*
Though imani yetu kwa CHADEMA arusha sasa imerudi.
CHADEMA imeunda kamati ya watu watatu inayoongozwa na mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho na mwanasheria mkongwe, Mabere Marando, kufanya uchunguzi wa utaratibu uliotumika kufikia maridhiano hayo.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa, alisema maridhiano yaliyofanyika kumpata meya na naibu wake hawayatambui kutokana na upungufu uliojitokeza wakati wa mchakato wa kuwapata viongozi hao.
Madiwani wa CHADEMA wanaodaiwa kukubali kufanya maridhiano ni pamoja n Diwani Estomih Mallah, ambaye atashika nafasi hiyo kuanzia sasa hadi mwaka 2014 atakapomwachia nafasi Diwani wa TLP, Michael Kivuyo, wengine ni John Bayo na Efatha Nanyaro.
Akifafanua upungufu huo, Dk. Slaa alisema kwanza maridhiano hayo hayakufikiwa na idadi ya wajumbe (madiwani) ambao wanaweza kufanya maamuzi, kwamba maridhiano hayo yalifanywa na wajumbe tisa kati ya 21 ya madiwani wote wa halmashauri hiyo.
Aliutaja upungufu mwingine kuwa mkurugenzi wa halmashauri ya jiji hilo alikubali kufanya muafaka bila ya kupata barua ya CHADEMA ya kukubali maridhiano ambayo ina majina ya walioteuliwa na chama hicho kupewa madaraka.
Aliongeza kuwa madiwani wa CHADEMA, watatu walioshiriki kwenye maamuzi husika walifanya hivyo bila kuwashirikisha viongozi wao wa wilaya, mkoa na makao makuu kwa ajili ya kupata baraka zao za kupendekeza majina ya watakaochaguliwa kuwa viongozi.
Alisema upungufu mwingine ni kuwapo kwa mianya ya rushwa ya kuwashawishi madiwani husika kushiriki kwenye maridhiano hayo pasipo kufuata taratibu zinazotakiwa.
Dk. Slaa alisema kutokana na matatizo hayo, CHADEMA haiyatambui maridhiano hayo na kudai kuwa yamefanywa kwa kupindisha kanuni na taratibu za kuwapata viongozi hao.
CHADEMA tunasema kuwa hatuyatambui maridhiano yaliyofikiwa kumpata meya na naibu wake kwani hayakufuata kanuni na taratibu za kuwapata uliofanyika pale ni uchakachuaji wa demokrasia, alisema Dk. Slaa.
Katibu Mkuu huyo alisema chama chake kipo kwa ajili ya kusimamia haki na kwamba kipo tayari kupoteza nafasi ya unaibu meya wa miaka minne aliopewa diwani wake na nafasi nyingine za mwenyekiti wa fedha na elimu.
Tunajua kuwa posho ni tamu sana na hili wamekuwa wakilisema madiwani wetu hawa mara kwa mara lakini chama chetu hakiangalii masilahi ya wachache, kipo kwa ajili ya kutetea haki na usawa wa Watanzania, alisema.
Dk. Slaa alisema kuwa msingi wa mgogoro huo ulianza tangu Desemba mwaka jana hadi chama chao kuomba maandamano ya amani ambayo yaliingiliwa na poslisi waliowajeruhi na kuwaua baadhi ya walioshiriki.
Alisema kama madiwani hao waliamua kufanya maamuzi hayo kwa kuangalia posho bila kuangalia msingi wa mgogoro huo, chama chao kinawachukulia hatua baada ya kuthibitisha yaliyotokea katika maridhiano.
Kiongozi huyo alisema kama chama hicho kila siku kinaikosoa serikali ya CCM na wanachama wake, kipo tayari kufanya maamuzi magumu ya kuwawavua madaraka madiwani wake na kurudia uchaguzi upya.
Dk. Slaa alisema CHADEMA kama chama kingine, hakina watakatifu hivyo kipo tayari kurudiwa kwa uchaguzi wa baadhi ya kata, kama wananchi wa jiji hilo wanavyotaka, kutokana na mgogoro wa umeya ulivyo.
Alisema kamati aliyoiunda ambayo ninaongozwa na Marando, itakayofanya kazi kwa siku sita na baadaye kupeleka ripoti yake kwa kamati kuu na vivyo hivyo, viongozi wa wilaya na Mkoa wa Arusha kupeleka ripoti hiyo kwa ajili ya kutoa hukumu ya haki.
Kabla ya CHADEMA kutoa msimamo wake kama chama, Mwenyekiti wa chama hicho, ambaye pia ni Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe na Mbunge wa Jimbo la Arusha, Goodbless Lema, walinukuliwa na vyombo vya habari kuwa hawayatambui maridhiano hayo.
MY TAKE!
Wale CCM waliokuwa wanatumia nafasi hii kumshataki LEMA kwa wananchi sasa wameumbuka. Lema hakushiriki kuuuafiki muafaka wa arusha na alikuwa bungeni dodoma jamaa wakachukua advantage. However Diwanoi Nanyaro Efatha alishakuja hapa akasema yeye alishiriki kwenye hatua za mwanzo kama mwenyekiti wa BAVICHA mkoa hila hakutilia saini maridhiano ya mwisho na aliyapinga vikali with open eyes. LETS WAIT AND SEE KAMATIO YA MARANDO.*
Though imani yetu kwa CHADEMA arusha sasa imerudi.