October 2pm
Member
- May 2, 2023
- 31
- 28
Habarini wakuu!
Rushwa. Ufisadi, uhujumu uchumi na ubadhirifu wa mali za umma, ukandamizaji na ubinyaji wa haki za binadamu ikiwemo uhuru wa vyombo ya habari,Upindishaji wa haki na sheria, matumizi mabaya ya vyombo vya dola, unyanyasaji na ukosefu wa usawa wa kijinsia miongoni mwa kero na madhila yanayofanyika katika nchi yetu. Yote hayo kwa pamoja huwekwa katika dhana ya ‘mmomonyoko wa maadili” ambacho ni kiini kikuu cha matatizo ndani ya jamii na nchi yetu. Mwanasaikolojia nguli wa Marekani Lawrence Kohlberg alifafanua maadili kama “chanzo cha mtu kitabia. Mchakato wa kufikiri wakati wa mtanziko wa kitabia ambao hutumika kuamua nini kilichochema na nini kilichokibaya, kisha matokeo ya tabia”
Maadili ni mafundisho ya kifalsafa au kisheria ambayo yanalenga kuwafanya watu kuwa na tabia njema, mienendo yenye kufaa ndani ya jamii kusudi waweze kuishi kwa pamoja na amani. Kwamba watu watende mambo Mema na kuacha mambo mabaya.
Maadili kama uadilifu, uwajibikaji, heshima, uchapakazi, ukarimu, na uzalendo ndani ya jamii chanzo chake ni;
Lakini Fikra zenye maono pekee yake hazitoshi, isipokuwa fikra zenye maono yenye uadilifu ambazo viongozi wa nchi yetu wanapaswa kuwa nazo. Hii inamaanisha hatuwezi kutenganisha uongozi na maadili mema ikiwa tunahitaji taifa lenye maendeleo na jamii yenye amani na furaha.
Lakini ni wapi wanapatikana viongozi bora? Tutawapata wapi?
Ni ukweli wa hakika kuwa kamwe viongozi hawatoki mbinguni, isipokuwa ndani ya jamii yetu. Hivyo jamii yenye maadili mema huzalisha viongozi wenye maadili mema. Bila kujali viongozi hao watapatikana katika mfumo upi, uwe mfumo wa kifalme au mfumo wa kidemokrasia ambapo watu wazima wenye akili kwa hiyari wanapata fursa za kuchagua kiongozi atakayewaongoza. Demokrasia inafaida nyingi mno, lakini demokrasia bila maadili haina maana yoyote ile. Kama jamii haina maadili mema bila shaka upo uwezekano mkubwa wa kuchagua viongozi wasio na maadili mema.
Hatuna budi kuzirejelea zile taasisi muhimu ambazo ndio msingi au kiini cha maadili ndani ya jamii. Kama ifuatavyo;
1. Taasisi ya Ndoa iboreshwe na kuimarishwa;
Familia ndio mzizi na kiini cha taifa. Familia ni chanzo kikuu cha maadili. Wazazi na Walezi wanajukumu la kuhakikisha wanalea watoto katika misingi ya maadili mema. Mwandishi wa kitabu cha Mithali katika biblia ameandika; “ Mlee mtoto katika njia impasayo naye hataiacha hata atakapokuwa mzee”(Mithali 22:6) Malezi ya watoto yalenga mambo yafuatayo;
( picha kwa hisani ya tovuti ya adobe stock, google)
2. Kuboresha taasisi na mfumo wa Elimu.
(Picha kwa hisani ya google)
3. Taasisi za Dini
( Picha kwa hisani ya google, watoto wakiwa madrasa wakifundishwa elimu ya dini)
(Picha kwa hisani ya Google, watoto wakiwa kanisani wakifundishwa elimu ya dini)
4. Serikali
(Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Kushoto, na Abeid Karume wanakumbukwa kwa kusisitiza maadili ya viongozi na jamii kwa ujumla, picha kwa hisani ya google).
Maadili mema ni muarobaini katika kutatua matatizo mengi katika nchi kama ifuatavyo;
Karibuni kwa mjadala, Kura yako ni Muhimu. Ahsante!
Rushwa. Ufisadi, uhujumu uchumi na ubadhirifu wa mali za umma, ukandamizaji na ubinyaji wa haki za binadamu ikiwemo uhuru wa vyombo ya habari,Upindishaji wa haki na sheria, matumizi mabaya ya vyombo vya dola, unyanyasaji na ukosefu wa usawa wa kijinsia miongoni mwa kero na madhila yanayofanyika katika nchi yetu. Yote hayo kwa pamoja huwekwa katika dhana ya ‘mmomonyoko wa maadili” ambacho ni kiini kikuu cha matatizo ndani ya jamii na nchi yetu. Mwanasaikolojia nguli wa Marekani Lawrence Kohlberg alifafanua maadili kama “chanzo cha mtu kitabia. Mchakato wa kufikiri wakati wa mtanziko wa kitabia ambao hutumika kuamua nini kilichochema na nini kilichokibaya, kisha matokeo ya tabia”
Maadili ni mafundisho ya kifalsafa au kisheria ambayo yanalenga kuwafanya watu kuwa na tabia njema, mienendo yenye kufaa ndani ya jamii kusudi waweze kuishi kwa pamoja na amani. Kwamba watu watende mambo Mema na kuacha mambo mabaya.
Maadili kama uadilifu, uwajibikaji, heshima, uchapakazi, ukarimu, na uzalendo ndani ya jamii chanzo chake ni;
- Taasisi ya Ndoa, Familia.
- Taasisi za Elimu kama shule na vyuo
- Taasisi za dini
- Serikali
Lakini Fikra zenye maono pekee yake hazitoshi, isipokuwa fikra zenye maono yenye uadilifu ambazo viongozi wa nchi yetu wanapaswa kuwa nazo. Hii inamaanisha hatuwezi kutenganisha uongozi na maadili mema ikiwa tunahitaji taifa lenye maendeleo na jamii yenye amani na furaha.
Lakini ni wapi wanapatikana viongozi bora? Tutawapata wapi?
Ni ukweli wa hakika kuwa kamwe viongozi hawatoki mbinguni, isipokuwa ndani ya jamii yetu. Hivyo jamii yenye maadili mema huzalisha viongozi wenye maadili mema. Bila kujali viongozi hao watapatikana katika mfumo upi, uwe mfumo wa kifalme au mfumo wa kidemokrasia ambapo watu wazima wenye akili kwa hiyari wanapata fursa za kuchagua kiongozi atakayewaongoza. Demokrasia inafaida nyingi mno, lakini demokrasia bila maadili haina maana yoyote ile. Kama jamii haina maadili mema bila shaka upo uwezekano mkubwa wa kuchagua viongozi wasio na maadili mema.
Hatuna budi kuzirejelea zile taasisi muhimu ambazo ndio msingi au kiini cha maadili ndani ya jamii. Kama ifuatavyo;
1. Taasisi ya Ndoa iboreshwe na kuimarishwa;
Familia ndio mzizi na kiini cha taifa. Familia ni chanzo kikuu cha maadili. Wazazi na Walezi wanajukumu la kuhakikisha wanalea watoto katika misingi ya maadili mema. Mwandishi wa kitabu cha Mithali katika biblia ameandika; “ Mlee mtoto katika njia impasayo naye hataiacha hata atakapokuwa mzee”(Mithali 22:6) Malezi ya watoto yalenga mambo yafuatayo;
- Kuheshimu watu bila kuwabagua, namna bora ya kujiheshimu ni kuheshimu wengine,
- Kufanya kazi kwa bidii, kuwafundisha stadi za maisha na kula kwa jasho lao mwenyewe.
- Kuwa muadilifu, msafi na mwaminifu.
- Kuwa jasiri, mzalendo na kupinga uovu na uhalifu.
- Kuheshimu wakati hii ikiwa ni pamoja na kuwafundisha watoto jinsi ya kufanya mambo kwa wakati sahihi katika mazingira sahihi
- Kusaidia jamii hasa watu wasiojiweza,
- Kuwafundisha Elimu ya Fedha
( picha kwa hisani ya tovuti ya adobe stock, google)
2. Kuboresha taasisi na mfumo wa Elimu.
- Kuboresha mitaala na miongozo ya elimu kama kuweka somo la maadili ambalo litafundishwa kama somo.
- Waalimu wawe mfano bora kwa kuwa na tabia njema kwa kufuata maadili ya kazi zao na kubeba wajibu kama walezi wa watoto.
- Ziundwe Programu, matamasha ya kuhamasisha na kukuza maadili ya jamii.
- Wazazi na waalimu wawe karibu na washirikiane. Wazazi wasiwaachie majukumu walimu.
(Picha kwa hisani ya google)
3. Taasisi za Dini
- Yatolewe Mafundisho ya dini kwa watoto yanayolenga kuchukia tabia mbaya
- Kila dini iwe na program za kuwafunza watoto somo la dini na maadili kama ilivyo kwa Wakatoliki Kupitia Sunday Schools, na kwa waislam Kupitia Madrasa.
- Viongozi wa dini wote wawe na vyeti vya taaluma na uthibitisho kutoka kwenye mamlaka za serikali.
( Picha kwa hisani ya google, watoto wakiwa madrasa wakifundishwa elimu ya dini)
(Picha kwa hisani ya Google, watoto wakiwa kanisani wakifundishwa elimu ya dini)
4. Serikali
- Iundwe Katiba Mpya inayoendana na wakati na mazingira ambayo itawafanya watu wote kuwajibika bila kujali ni kiongozi au sio kiongozi. Pasiwepo na kinga ya Rais au kiongozi yeyote. Hii itachochea uwajibikaji.
- Vyombo vya sheria, na vyombo vya dola na Vyombo ya habari viwe huru pasipo kuingiliwa kimajukumu.
- Seriksli idhibiti uhusika wa watu mashuhuri wenye maudhui yanayoharibu maadili ya jamii.
- Pawe na dhamira ya dhati na Adhabu kali katika kupambana na Wala Rushwa, wahujumu uchumi na Wauza madawa ya Kulevya
- Serikali itoe elimu na kuhamasisha jamii kuwa na maadili mema.
(Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Kushoto, na Abeid Karume wanakumbukwa kwa kusisitiza maadili ya viongozi na jamii kwa ujumla, picha kwa hisani ya google).
Maadili mema ni muarobaini katika kutatua matatizo mengi katika nchi kama ifuatavyo;
- Kuchochea Maendeleo kutokana na kuwa na viongozi bora na jamii yenye kuwajibika.
- Kupungua kwa Vitendo vya uhalifu na jinai kama ufisadi, rushwa, utapeli, makosa ya mtandaoni, uzaji wa madawa ya kulevya, jamii ikiwa na maadili hata uhalifu unapungua
- Kutatua tatizo la ajira, kwani vijana watakuwa wachapakazi bila kubagua kazi, viongozi watatengeneza fursa za ajira kwa vijana na wanawake kwani ni sehemu ya wajibu wao.
- Itachochea utawala bora unaoheshimu haki za binadamu. Jamii nayo itaishi kwa kuheshimiana huku ikifuata utawala wa sheria pasipo kujichukulia sheria mkononi.
- Itaboresha huduma za kijamii, watumishi wa umma watakuwa na maadili ya kazi, malalamiko ya kuchelewa kazini au kuwatolea lugha chafu wananchi yatapungua kabisa. Huduma bora za upatikaniji wa haki kwenye vyombo vya dola na mahakamani itaifanya jamii iishi kwa amani.
Karibuni kwa mjadala, Kura yako ni Muhimu. Ahsante!