Tutambuane, nani ni nani katika kudai Katiba mpya

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,815
35,804
Madai ya kupata katiba mpya ni mapambano ya haki ambayo hayawezi kukamilika bila ya kupata katiba nyingine tofauti na iliyopo.

Mwenyekiti Mbowe na baadhi ya wapiganaji (Mola awafanyie wepesi) tayari wako mikononi mwa watesi wetu.

IMG_20210729_192941_480.jpg


Wao wametangulia na hakuna mpambanaji aliye salama.

Pamoja na kuwa mapambano haya ni ya haki na yako kwa mujibu wa sheria, unyeti wake na vizingiti vilivyomo vinalazimu kufahamiana vizuri kwa mustakabala mwema wa zoezi zima.

Yafahamu makundi haya yaliyopo katika jamii yetu:

1. Wadai: Wapambanaji walio dhamiria kuidai haki yao ya kuwa na katiba mpya itakayo wahakikishia wote uhuru, usawa, haki, demokrasia na uwajibikaji.

2. Wadaiwa: Wanufaika wa hali iliyopo sasa. Hawa ni walioko madarakani. Wenye maslahi binafsi yenye uwezekano wa kupotea kwa ujio wa katiba mpya.

3. Washirika: Marafiki zetu wa ndani na nje ambao pamoja na tofauti zetu nao katika mambo mengine, tuna malengo ya mwisho kuhusiana na katiba mpya yanayofanana.

4. Maadui: Hawa ni vibaraka wa wadaiwa. Hapa wamo wale wenye vipigo vya mbwa koko na wote wanaotumika kwa namna yoyote ili kutatiza harakati hizi kwa maslahi yao binafsi na mabwana zao wa #2.

Kwenye kundi hili wamo pia wajumbe kadhaa wa humu JF. Mitizamo yao kupitia nyuzi na comments zao inajieleza wazi.

5. Wasiohusika: Hawa wapo wenye kutokujua kuwa wanahusika na wengine wenye kujitoa ufahamu kwa makusudi (opportunists) ili kupisha kuwa sehemu ya mchakato na kusubiria matunda wale bila karaha.

Wasiohusika kwa kutokujua wanahitaji kuelimishwa. Ndipo umuhimu wa makongamano na mikutano ya vyama vya siasa inayopigwa vita na wadaiwa na maadui zetu ulipo.

Angalizo: tutazamane usoni vizuri kujiridhisha. Mamba wala watu hawawezi kuwa sehemu ya ushauri wa namna ya kuvuka mto salama.
 
Mkuu nisiache ku summarize:

Habari leo mujini, katiba mpya sikia,
Yadaiwa kama deni, Mdaiwa kakimbia,
Mapolisi kulikoni, wadai kuwazuia?

Enyi msiohusika, hoho vipi ziwawashe?
KATIBA KATIBA Ndio MUAFAKA wa kizazi kijacho.
Enyi watawala na mliopita acheni mara moja kuyumbisha taifa la Tanzania ni muhimu kuliko yeyote.
 
Kamamda, ni wewe tu na Mbowe mliobaki. Komaeni mpate hiyo katiba mpya.

Nimejaribu kukurejea nyuzi na comments zako kupata mitizamo yako:

IMG_20210823_055809_947.jpg


Naona angalizo pale kwenye mada, kama lilivyo lina kuhusu sana mkuu. Kwani nina hata haja ya kuendelea kudadavua zaidi?

Hiiiiii bagosha!
 
KATIBA KATIBA Ndio MUAFAKA wa kizazi kijacho.
Enyi watawala na mliopita acheni mara moja kuyumbisha taifa la Tanzania ni muhimu kuliko yeyote.

Mkuu ungefanya maboresho kidogo pale kuwa:

"KATIBA KATIBA Ndio MUAFAKA wa kizazi hiki na kizazi kijacho."

Ingependeza zaidi.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Bwana Johnny Sack unayejinasibu kutushauri kuhusiana na upatikanaji wa mema ya Tanzania, katika makundi 5 hayo katika mada wewe upo lipi?

Zingatia angalizo pia.

Kwamba?

IMG_20220320_084259_400.jpg


Hiiiiii bagosha!
 
"Madai ya kupata katiba mpya ni mapambano ya haki ambayo hayawezi kukamilika bila ya kupata katiba nyingine tofauti na iliyopo."

Wenye wito watafanikisha hili.

Wanaojifanya washauri au kuwa wao hawahusiki ruksa kuufyata.

Aluta Continua.
 
Back
Top Bottom