Kiongozi kwa mwaka unaweza kuwa wahitimu 100,000+ kwa mwaka.
Serikali inahitaji mikakati ya kuwapatia ajira wengi wao. Lakini na yenyewe inahitaji kama wakali 1000 tu kwa shughuli zao.
Maendeleo ya China ni mikakati (na sehemu kubwa ya uongozi wao) ni engineers; sasa aina maana hakuna MBA’s, Econimists and Financials kwenye team yao.
But then it starts with a strategy na system ya kupata vipanga wa kufikia malengo na kusimamia.
Do we have that long term commitment?
Kwa mfano nchi gani ina mikakati ya kuajiri wahitimu "walio wengi"
Definition ya "walio wengi" ni nini kwa number au percentage; kwa hao 100k uliosema unatazamia serikali iajiri wangapi kwa mwaka?
Kuhusu China maelezo yako yamekuwa out of context ya uzi wako mwenyewe!
Wasomi wenye uelewa wanajua elimu inaleta "knowledge" "skills" na attitude. So waliokamilika wana hvyo vyote related to their areas. Wanajua pia elimu ni biashara na wamewekeza so ni jukumu lao kutafutia soko bidhaa yao baada ya kuvuna(kugraduate yani), elimu yao ndio commodity yao kama mkulima na mazao yake.
Kama wameelimika sawasawa wanajua kbs ili wasonge mbele wanatakiwa kuuza commodity zao tena kwa bei na wanavyotaka wao. Hawawezi kusubiri mteja (serikali) awaamulie wafanyie nini bidhaa yao, na wanatakiwa kujua unaweza kuuza popote bila masharti yoyote, wasomi wetu wanajua haya?
Wachina waliona hilo na kila mtu alipambana kutafutia soko alichonacho kichwani ndio wenye MBA walianzisha makampuni mbalimbali ya consultancy, management, banks, mashamba, etc, maengineer na wengine wote wakafuata mikondo hiyohiyo, serikali yao iliajiri wachache sana. Hamna serikali inaweza kubeba wasomi wote, watakua wanafanya nini? Ifungue mashamba? Viwanda? No!
Msomi aliyefanya Masters technically anatakiwa kucreate jobs, wa PhD lengo ni kufanya research, teaching na consultancy, bachelors kuongoza vikundikazi na diploma kushuka chini ndio wazalishaji. Sasa Tanzania kila mtu tangu la saba hadi PhD (za kupika offcourse) wanataka mama awape ajira! Inawezekana wapi??
Nani akaanzishe hizo ajira mnazotaka kuzipata???