Jaji Mfawidhi
JF-Expert Member
- Feb 20, 2016
- 16,969
- 26,058
Tafakuri ya Askofu Benson Kalikawe Bagonza
Rais Samia ameweka rekodi. Tutasahau barabara, madaraja, madarasa na teuzi anazofanya. Lakini hili la kukutana na Chadema katika maadhimisho ya BAWACHA hatutalisahau kirahisi.
Wapo walionuna pande zote mbili za CCM na Upinzani. Ni budi wawepo ili watukumbushe tulikotoka. Hata kuku wa pande mbili hizo hawakuruhusiwa kujamiiana. Leo twakumbatiana!
Mwaka jana 2022 nilihutubia Bawacha Kitaifa kule Iringa. Nilisema tunahitaji Tanzania mpya siyo CCM mpya wala Chadema mpya.
Niliporudi DSM nilikutana na kiongozi wa CCM kitaifa nikamwambia; “Awamu ya Tano imeimarisha upinzani kwa namna ambayo ni vigumu kuubomoa bali kuuruhusu ujibomoe.”
Sasa Rais Samia ameanzisha mchakato wa upinzani kujibomoa wenyewe, si kuruhusu Rais mwingine kama yule aje kuubomoa. Tumuunge mkono Rais Samia anapotumia hoja kuunganisha nchi kuliko kutumia fedha na mabomu kugawa nchi.
Napenda kushauri mambo 10:
1. Kila upande una wahafidhina (Zealots).
Kazi ya kiongozi si kuwapuuza wala kuwafukuza. Ni kujadiliana nao bila kupigana nao. Wakiondoka vyama vitalala.
2. Kufukuzana ni hulka ya viongozi madikteta na walevi wa madaraka.
Rais Samia na Mbowe wajiepushe na hulka hiyo.
3. Kuna mpito unakuja kitaifa.
Mbuzi atalala na chui zizi moja bila kuumizana. Bungeni, serikalini, na hata kwenye kamati. Tujifunze kuishi na hali tusiyoweza kuibadilisha.
4. Ukweli wa yaliyopita ni muhimu kuliko haki kwa yajayo.
Tujifunze kusamehe kosa lililo wazi. Hata marehemu akiacha madeni huwa yanalipwa na warithi.
5. Tusisahau tulipopitishwa.
Si CCM wote waliokubaliana na hali ile. Si wapinzani wote walioichukia hali ile. Ili tusirudi huko tuungane kusema NEVER and NEVER again.
6. Ili tusirudi huko, mifumo imara na taasisi imara ni muhimu kuliko super woman au super mwamba.
Hata kama hatuipendi; KATIBA MPYA ni hitaji la jana kuliko leo na wanaihitaji watawala kuliko watawaliwa.
7. Kiwango cha rushwa bado kiko juu na kinastawisha kiburi cha watawala dhidi ya wananchi.
Wenye fedha wanaanza kujiona juu ya sheria. Rushwa hii ikiingia ndani ya vyama, tutampata mwenye roho isiyo ya Samia na mbaya kuliko Bwana yuleee.
8. Jukumu la Rais ni kuongeza uhuru wa wananchi; si kuupunguza.
Watanzania tuunge mkono jitihada za Rais kuthamini na kuvumilia maoni tofauti. Rais hawezi kufa wala kuugua kwa kuambiwa asiyopenda kusikia.
9. Siku ya wanawake imefana, bado safari ya ukombozi wao ni ndefu.
Maadui wao ni wengi. Hata mwanamme anayekandamizwa na mkewe lakini anajifanya mbabe mbele ya wanaume wenzake asaidiwe na wanawake!
10. Wapinzani wa maridhiano ni wale walioshindwa ndani na nje ya vyama vyao.
Maridhiano yanawanyima uhalali. Lakini wapo wanaotaka maridhiano yaondoe tofauti za mtazamo na maoni tofauti. Hatutaki makasuku wa taifa. Tuheshimu tofauti bila kupigana.
Tumuunge mkono Rais Samia. Tumpinge kwa hoja. Tusisahau kirahisi tulikotoka.
Rais Samia ameweka rekodi. Tutasahau barabara, madaraja, madarasa na teuzi anazofanya. Lakini hili la kukutana na Chadema katika maadhimisho ya BAWACHA hatutalisahau kirahisi.
Wapo walionuna pande zote mbili za CCM na Upinzani. Ni budi wawepo ili watukumbushe tulikotoka. Hata kuku wa pande mbili hizo hawakuruhusiwa kujamiiana. Leo twakumbatiana!
Mwaka jana 2022 nilihutubia Bawacha Kitaifa kule Iringa. Nilisema tunahitaji Tanzania mpya siyo CCM mpya wala Chadema mpya.
Niliporudi DSM nilikutana na kiongozi wa CCM kitaifa nikamwambia; “Awamu ya Tano imeimarisha upinzani kwa namna ambayo ni vigumu kuubomoa bali kuuruhusu ujibomoe.”
Sasa Rais Samia ameanzisha mchakato wa upinzani kujibomoa wenyewe, si kuruhusu Rais mwingine kama yule aje kuubomoa. Tumuunge mkono Rais Samia anapotumia hoja kuunganisha nchi kuliko kutumia fedha na mabomu kugawa nchi.
Napenda kushauri mambo 10:
1. Kila upande una wahafidhina (Zealots).
Kazi ya kiongozi si kuwapuuza wala kuwafukuza. Ni kujadiliana nao bila kupigana nao. Wakiondoka vyama vitalala.
2. Kufukuzana ni hulka ya viongozi madikteta na walevi wa madaraka.
Rais Samia na Mbowe wajiepushe na hulka hiyo.
3. Kuna mpito unakuja kitaifa.
Mbuzi atalala na chui zizi moja bila kuumizana. Bungeni, serikalini, na hata kwenye kamati. Tujifunze kuishi na hali tusiyoweza kuibadilisha.
4. Ukweli wa yaliyopita ni muhimu kuliko haki kwa yajayo.
Tujifunze kusamehe kosa lililo wazi. Hata marehemu akiacha madeni huwa yanalipwa na warithi.
5. Tusisahau tulipopitishwa.
Si CCM wote waliokubaliana na hali ile. Si wapinzani wote walioichukia hali ile. Ili tusirudi huko tuungane kusema NEVER and NEVER again.
6. Ili tusirudi huko, mifumo imara na taasisi imara ni muhimu kuliko super woman au super mwamba.
Hata kama hatuipendi; KATIBA MPYA ni hitaji la jana kuliko leo na wanaihitaji watawala kuliko watawaliwa.
7. Kiwango cha rushwa bado kiko juu na kinastawisha kiburi cha watawala dhidi ya wananchi.
Wenye fedha wanaanza kujiona juu ya sheria. Rushwa hii ikiingia ndani ya vyama, tutampata mwenye roho isiyo ya Samia na mbaya kuliko Bwana yuleee.
8. Jukumu la Rais ni kuongeza uhuru wa wananchi; si kuupunguza.
Watanzania tuunge mkono jitihada za Rais kuthamini na kuvumilia maoni tofauti. Rais hawezi kufa wala kuugua kwa kuambiwa asiyopenda kusikia.
9. Siku ya wanawake imefana, bado safari ya ukombozi wao ni ndefu.
Maadui wao ni wengi. Hata mwanamme anayekandamizwa na mkewe lakini anajifanya mbabe mbele ya wanaume wenzake asaidiwe na wanawake!
10. Wapinzani wa maridhiano ni wale walioshindwa ndani na nje ya vyama vyao.
Maridhiano yanawanyima uhalali. Lakini wapo wanaotaka maridhiano yaondoe tofauti za mtazamo na maoni tofauti. Hatutaki makasuku wa taifa. Tuheshimu tofauti bila kupigana.
Tumuunge mkono Rais Samia. Tumpinge kwa hoja. Tusisahau kirahisi tulikotoka.