Huu mchakato nimeuanza toka tarehe 8, na usiku wa tar 8 kuamkia tar 9 nililala saa nane usiku bila mafanikio, usiku wa kuamkia leo, nimekomaa kuvumilia kuyaangalia yale maputo [emoji23][emoji23] na mtandao ukanikubalia japo kwa kuubembeleza na hatimae mida ya saa kumi na moja kasoro asbh nikakamilisha.
Kwa ambao hawajakamilisha, endeleeni kujaribu na uvumilivu ni muhimu. Hii site ni kujaribu day and night maana kuna wengine walifanikisha jana saa tatu asbh.
Changamoto kubwa za huu mfumo ni pamoja na kuwa slow sanaa, yaani hadi kero. Pia nimeona kwenye Date of Birth (DoB) inapunguza siku moja kwenye tarehe. Mfano ukiandika 1980/01/5, mfumo unabadilisha na kuandika 1980/01/4.
Pia centre namba za shule zinabadilika, mfano S1168 inabadilika S900 baada ya ku-save choices. Kibaya kabisa, unavyozidi kuchelewa nafasi zinajaa. Kwahyo mwishowe utajikuta umefanikiwa kuingia kwenye mfumo na kukuta shule zenye uhitaji wa masomo yako zimeondoka baada ya vacancy zilizokuwepo kujaa.
Mwisho kabisa, nawashauri ambao bado kuwa mfumo hauhitaji hasira, nenda nao kwa uvumilivu.