Nikifa MkeWangu Asiolewe
JF-Expert Member
- Feb 26, 2024
- 11,250
- 24,084
Kulingana na mila na desturi zetu zinatofautiana kabila hadi kabila na jamii nyingine kwenda jamii nyingine.
Ni kawaida kukuta jamii au tamaduni ya watu hawa haziingiliani na tamaduni za jamii/kabila fln.
Mfano kuna baadhi ya makabila huoa binamu zao wengine huzaa na dada zao nk.
Kule uchagani kama sikudanganywa mwanamke kukupigia goti kama huku usukumani huhesabiwa kama tusi lakini usukumani ni heshima na ni lazima! Huo ndo utofauti kwa kifupi wa jamii na tamaduni zake.
Leo ningependa tujadiri kifamilia zaidi bila kuangalia kwanza tamaduni na desturi zetu kama ni sahihi kufua nguo za baba mkwe kwa wanawake.
Ikumbukwe kwa desturi za kisukuma ni marufuku na haitakiwi kabisa kufua nguo za baba mkwe wake.
Wasukuma walienda mbali zaidi hata bafu walikuwa hawachangii na wakwe zao japo kwa sasa hali ni tofauti(wanachangia)
Tukija kwa ujumla wake ni sahihi au sio sahihi kufua nguo za baba mkwe wako? Iwe kwa sababu yoyote Ile?
Kama sio sahihi ni kwanini?
Manyanza
Karibuni
Ni kawaida kukuta jamii au tamaduni ya watu hawa haziingiliani na tamaduni za jamii/kabila fln.
Mfano kuna baadhi ya makabila huoa binamu zao wengine huzaa na dada zao nk.
Kule uchagani kama sikudanganywa mwanamke kukupigia goti kama huku usukumani huhesabiwa kama tusi lakini usukumani ni heshima na ni lazima! Huo ndo utofauti kwa kifupi wa jamii na tamaduni zake.
Leo ningependa tujadiri kifamilia zaidi bila kuangalia kwanza tamaduni na desturi zetu kama ni sahihi kufua nguo za baba mkwe kwa wanawake.
Ikumbukwe kwa desturi za kisukuma ni marufuku na haitakiwi kabisa kufua nguo za baba mkwe wake.
Wasukuma walienda mbali zaidi hata bafu walikuwa hawachangii na wakwe zao japo kwa sasa hali ni tofauti(wanachangia)
Tukija kwa ujumla wake ni sahihi au sio sahihi kufua nguo za baba mkwe wako? Iwe kwa sababu yoyote Ile?
Kama sio sahihi ni kwanini?
Manyanza
Karibuni