Tungejua ugumu wa cheo, wengi tungekaa pembeni

Tungejua ugumu wa cheo, wengi tungekaa pembeni

Malaria 2

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2023
Posts
8,476
Reaction score
12,666
katika Uislamu cheo na madaraka si kitu cha kung’ang’ania au kukipigania kwa hila. Mtume Muhammad ﷺ alitufundisha kuwa cheo ni amanah (uaminifu) na mzigo mkubwa kwa mwenye kupewa.

🔹 Dalili kutoka Hadith:
Mtume ﷺ alimwambia Abdurrahman bin Samura:

"Ewe Abdurrahman! Usiviombe vyeo. Kwa kuwa ukipewa kwa kuviomba, utaachiwa wewe mwenyewe; lakini ukipewa bila kuviomba, utasaidiwa na Mwenyezi Mungu."
(Hadith Sahih Bukhari na Muslim)

Mtume ﷺ alimwambia Abu Dharr (RA):

"Ewe Abu Dharr! Hakika wewe ni dhaifu, na uongozi ni amanah. Na hakika siku ya Qiyamah utakuwa ni fedheha na majuto, isipokuwa kwa yule aliyeuchukua kwa haki na akatimiza wajibu wake."
(Sahih Muslim, Hadith 1825)
 
Hata Uwezo wa kuongoza nchi pia hamna, ni bahati mbaya tu tairi la gari liliisha upepo wakati tunapanda mlima. 🙂 🙂
Screenshot_20250620-214416.png
 
katika Uislamu cheo na madaraka si kitu cha kung’ang’ania au kukipigania kwa hila. Mtume Muhammad ﷺ alitufundisha kuwa cheo ni amanah (uaminifu) na mzigo mkubwa kwa mwenye kupewa.

🔹 Dalili kutoka Hadith:
Mtume ﷺ alimwambia Abdurrahman bin Samura:


(Hadith Sahih Bukhari na Muslim)

Mtume ﷺ alimwambia Abu Dharr (RA):


(Sahih Muslim, Hadith 1825)

Kuna huyu anayeng'ang'ania cheo hadi kuuwa, kuteka na kuwafungia magerezani washindani na wakosoaji wake. Hiyo dini yako au yenu haina neno lolote kwake?
 
Enzi za Mtume Muhammad SAW kwenye mkusanyiko walikuwa wanahesabiwa Wanaume, Wanawake na Watoto?
 
Haya ndio maneno alipashwa kuambiwa na wale wala ubwabwa wanaojiita viongozi wa dini na matumbo yao mapana utadhani wameficha mafenesi.

Waislam wa leo wamekuwa watu wa kupelekwa kama bendera inayofuata upepo tu. Hawatizamii maslahi ya kijamii na usawa na haki ya wote,wao wanatazama ushabiki.

Imagine kwanza Dini inakataza Mwanaume kuongozwa na mwanamke ila wamefumbia macho hilo?

Lakini pia udhalimu na uhaini unaofanywa na wale waliopo nyuma ya mwanamke wao wamekalia kimya ila wanajifanya vifungu vya Dini ya haki wamevishika,hawa kweli wanaijua ibada?

Nikupongeze kwa kusemea ukweli na kusimamia maneno matukufu katika wakati ambao uongo umetamalaki,hila imekuwa ndio ujanja, uongo unafanywa kweli na ndio unasemwa hata mbele za waumini katika nyumba za ibada, haki inafichwa na kudhurumiwa mchana kweupe, na unafiki ndio sifa ya uswahiba.

MUNGU atawalaani hawa Takataka wote.
 
Haya ndio maneno alipashwa kuambiwa na wale wala ubwabwa wanaojiita viongozi wa dini na matumbo yao mapana utadhani wameficha mafenesi.

Waislam wa leo wamekuwa watu wa kupelekwa kama bendera inayofuata upepo tu. Hawatizamii maslahi ya kijamii na usawa na haki ya wote,wao wanatazama ushabiki.

Imagine kwanza Dini inakataza Mwanaume kuongozwa na mwanamke ila wamefumbia macho hilo?

Lakini pia udhalimu na uhaini unaofanywa na wale waliopo nyuma ya mwanamke wao wamekalia kimya ila wanajifanya vifungu vya Dini ya haki wamevishika,hawa kweli wanaijua ibada?

Nikupongeze kwa kusemea ukweli na kusimamia maneno matukufu katika wakati ambao uongo umetamalaki,hila imekuwa unanja, uongo unafanywa kweli, haki inafichwa na unafiki ndio sifa ya uswahiba.

MUNGU atawalaani hawa Takataka wote.
Takbir
 
Imagine kwanza Dini inakataza Mwanaume kuongozwa na mwanamke ila wamefumbia macho hilo?
Nchi haiongozwi na dini , inaongozwa na katiba , na kwenye katiba kifungu hicho hakuna

Kadiri mnavotumia hoja uchwara ndo wahuni wanaongeza speed
 
Huu ni ukweli anapaswa kuambiwa mwanamama, ila viongozi wa dini yetu wameamua kukaa kimya ili yao yaende.. na uislam haupendi mambo haya.
 
Nchi haiongozwi na dini , inaongozwa na katiba , na kwenye katiba kifungu hicho hakuna

Kadiri mnavotumia hoja uchwara ndo wahuni wanaongeza speed
Naam nakuunga mkono 100% inchi haingozwi na dini na haipaswi kuwa hivyo kwa maslahi mapana ya raia wote ndani ya jamuhuri.

Ila Dini inaongoza maisha yetu ya kila siku, katiba tu imereflect au kuakisi mafunzo ya Dini, ndio maana hata hawa vijukuu vya Farao wasiojua maana ya vibaya kutwa kucha kujizungusha kwenye nyumba za ibada wakijifanya dini wanaijua kwasababu gani unadhani?

Nikwasababu Dini au imani ni sehemu ya muongozo wa kijamii katika kusimamia maadili sio katika kupiga madili.

Katiba lazima wote tuishike ns kuiheshimu kama muongozo wa kitaifa na kitabu kikuu cha sheria na kanuni. Ila tunaporudi katika maisha ya kila siku Dini au imani haikwepeki katika kukumbushana wajibu wetu kama raia.
 
Huu ni ukweli anapaswa kuambiwa mwanamama, ila viongozi wa dini yetu wameamua kukaa kimya ili yao yaende.. na uislam haupendi mambo haya.
Unafiki. Rejea sifa za mnafiki utaona kwa namna gani watu wamechagua kuwa wanafiki kwa makusudi. Na MUNGU hapendi mtu mnafiki.
 
Kuna huyu anayeng'ang'ania cheo hadi kuuwa, kuteka na kuwafungia magerezani washindani na wakosoaji wake. Hiyo dini yako au yenu haina neno lolote kwake?
Hata akina Lissu wanagombania vyeo, mpina pia
 
Nchi haiongozwi na dini , inaongozwa na katiba , na kwenye katiba kifungu hicho hakuna

Kadiri mnavotumia hoja uchwara ndo wahuni wanaongeza speed
Lkn ukifa tunaona msalaba upo mbele, au jeneza limo msiktini.
 
Naam nakuunga mkono 100% inchi haingozwi na dini na haipaswi kuwa hivyo kwa maslahi mapana ya raia wote ndani ya jamuhuri.

Ila Dini inaongoza maisha yetu ya kila siku, katiba tu imereflect au kuakisi mafunzo ya Dini, ndio maana hata hawa vijukuu vya Farao wasiojua maana ya vibaya kutwa kucha kujizungusha kwenye nyumba za ibada wakijifanya dini wanaijua kwasababu gani unadhani?

Nikwasababu Dini au imani ni sehemu ya muongozo wa kijamii katika kusimamia maadili sio katika kupiga madili.

Katiba lazima wote tuishike ns kuiheshimu kama muongozo wa kitaifa na kitabu kikuu cha sheria na kanuni. Ila tunaporudi katika maisha ya kila siku Dini au imani haikwepeki katika kukumbushana wajibu wetu kama raia.
NChi inaongozwa na katiba mkuu, ndo maana hata 2021 aliapishwa kuws rais mkuu, na kwa mbungi ya chama cha mapinduzi 2025 anaenda kuapishwa tena.

Muda huo watanzania sisi tunatamani mabadiliko kws miaka mingi ila uthubutu wa maamuzi magumu hatuna

Ndo tunaishia kujipa matumaini kama hivi

Huku mtaani utasikia "hata dini yake haitaki aongoze" -- hata hatuangalii kama ni muumini kwelikweli au lah

Mimi mtu anayejiita muumini wa kweli wa dini yeyote ile akiwa ccm bado namshangaa


Wananchi kama samia hatumtaki tuchague viongozi wa vyama vingine.
Ila tukiona kwamba hata kama hstumtaki bado atakua rais basi tujikitike kutatua hilo tatizo kwanza
 
Lkn ukifa tunaona msalaba upo mbele, au jeneza limo msiktini.

Hizi hoja ni uchwara mkuu,

KAma hatuwezintumia njia ngumu kuiondoa ccm, tunatakiwa kuwaacha waendelee tu mkuu, mambo mengine hayabni ya kujifariji
 
Hizi hoja ni uchwara mkuu,

KAma hatuwezintumia njia ngumu kuiondoa ccm, tunatakiwa kuwaacha waendelee tu mkuu, mambo mengine hayabni ya kujifariji
Mimi sina haja ya kuiondoa ccm. Chadema wakipewa wataiharibu nchi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom