Tunduma: Vurugu zaibuka mpakani mwa Tanzania na Zambia , Mabomu ya machozi yapigwa

Bado hiyo habari haieleweki! Kumetokea nini mpaka kusababisha hali hiyo?

Sent using Jamii Forums mobile app
Wapi hujaelewa mkuu?

Kifupi Vurugu zimenzishwa na raia wa Zambia ambao ni madalali au wabebeaji, baada ya wenzao kukamatwa jana upande wa Tanzania...

Hao madalali hiyo ni shughuli yao ya kawaida kwa miaka mingi, yaani wazambia wanaotoka maeneo ya mbali mfano Lusaka, Kitwe ama Ndola wakati mwingine Malawi hata Zimbabwe kuja kununua bidhaa Tunduma mara nyingi wakifika huwa wanahitaji wasaidizi ambao ndio hao wabebeaji wakati ununuaji.

Sasa imefika wakati wale wasaidizi wakati mwingine huwaibia hao wageni ama kuwauzi bei kubwa tofauti na hali halisi.

Sasa wafanyabishara wa Upande wa Tunduma wakalalamika polisi kwamba hao watu wanachangia kuharibu biashara hivyo wazuiwe.

Jana ndio ikafanyika operation maalumu kuwakamata hao wabebeaji, baada ya kuona wenzao wamekamatwa walioko nje leo wameanzisha vurugu kwa kuwazuia Watanzania wote kuingia upande wao wa Zambia hata magari yanayovuka mpaka.... Wakishinikiza wenzao waachiwe na serikali ya Tanzania.

Kilichofuata ni mabomu kuwatawanya hao raia, Mpaka wa Zambia na Tanzania imeingiliana sana hivyo kukitokea vurugu upande mmoja wote mnaathirika bila kujali zipo Zambia ama Tanzania.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyo kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Songwe inaonekana upeo wake ni mdogo sana. Anasema hayo mambo yametokea upande wa Zambia, hayamhusu? Hivi huyu anajielewa? Utasemaje kuwa hayakuhusu wakati watu wanaathirika, biashara zinaathirika, mapato ya serikali yanaathirika, n.k.

Tuna viongozi hopeless kabisa. Kikwazo kimojawapo, ukiacha TRA, sheria mbaya, wanasiasa, na sera mbaya, kwa ukuaji wa uchumi wetu, ni Jeshi la Polisi.
 
Huyo kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Songwe inaonekana upeo wake ni mdogo sana. Anasema hayo mambo yametokea upande wa Zambia, hayamhusu? Hivi huyu anajielewa? Utasemaje kuwa hayakuhusu wakati watu wanaathirika, biashara zinaathirika, mapato ya serikali yanaathirika, n.k.

Tuna viongozi hopeless kabisa. Kikwazo kimojawapo, ukiacha TRA, sheria mbaya, wanasiasa, na sera mbaya, kwa ukuaji wa uchumi wetu, ni Jeshi la Polisi.
Baada yakufikiria namna gani ya kukaa na wenzao watatue wao wanaongea ujinga Tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu mimi nimekuelewa vizuri hao mapota wakizambia wamekamatwa na police wetu hapo kuna umoja fulani ambao ni wa kudumu pota wa Kitanzania au machinga wa kitanzania akikamatwa nao hawataki machinga wa kizambia apige kazi upande wetu...kinachotakiwa police wa mpakani wawe na Elimu ya international relation sio kuokotana tuu madhara ndio yanakua makubwa kama hayo...kuna officer mmoja alikua msimamizi wa Zambia alikua kichwa sana sasa hivi nilimkuta Livingston border jamaa aliwaagiza police wa Tanzania na Zambia kutokamatana hovyo na ukimkamata raia asie wa Nchi yako mpelekeni kwao wao watamshughulikia mambo hayo yalipungua kabisa...maana ukifanya fujo upande wa Nakonde kama Mtanzania unapelekwa Tunduma police post na hivyo hivyo kwa Wazambia...kuoneana kukaisha kabisa ....
 
Wapigwe tuu wa Zambia wana robo mbaya sana

Sent using Jamii Forums mobile app
Hujui unachokiongea, asilimia 90 ya biashara ya Tunduma mteja mkuu ni mzambia...Mkoa wa Songwe chanzo chake kikuu cha mapato ni Tunduma....na kwa jinsi huu mpaka ulivyo kaa Tanzania ndio inanufaika zaidi kuliko zambia...

Siku Zambia akiamua kudhibiti mpaka wake na Tunduma tunaisahau.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom