Tundu Lissu umetuangusha kwa nini hukuhudhuria vikao vya kamati za katiba

Status
Not open for further replies.
tundu lissu alikosa maarifa kwa kukimbia vikao hivyo sasa anapiga kelele za nini?

Ni lazima kuhudhuria kikao ili utoe maoni? Yaani hakuna njia nyingine ya kufikisha maoni ila kuhudhuria kikao "in person"?
 
hivi mswasa ulibadilishwa lugha kuto kimombo na kuwa kiswahili ili iweje...je iliwabunge wausome au ili upelekwe kwa wananchi ambao wengi wao hawajui kimombo...
 
Lisu ana haki kuwasilisha mawazo yake. Kwa wale unaoona anapiga kelele mmekosea. alichofanya Celina ni kumattack kujaribu kufunika uozo.. yani unaacha kujadili content unamjadili mtu tena unatafuta sababu dhaifu kabisa. alifanya sahihi kutokwenda. utashirikije wakati unajua watu tayari wamepanga mambo yaende wanavyotaka wao? angekuwa msindikizaji tu!!
Kama aliona mapema kwa nini hakuyasema hayo mapema na kwa maana hiyo asingeweza hata kuhudhuria vikao vya bunge tangu mwanzo. Alilalamika wapi kwamba kamati wamepanga mambo yaende wanavyotaka wao?
 
Lissu hajatutendea haki watanzania kwa hili ni mpiganaji lakini ukipigana bila maarifa mwisho utashindwa
 
hawa jamaa walifanya fujo jana kwenye mdahalo , naona bado wanaendeleza pumba humu

Mkuu hizo siasa za cuf ndio zilivyo. Jana nilikua naangalizia mdaharo huo kwenye kijiwe kimoja mashuhuri yaani, kuna dini fulani inakisakama cdm sana. Na hata ukiangalia kwa umakini wengi wanaopinga cdm huwa na ajenda ya udini. Angalia sana hili au lifanyie kazi.
 
Mkuu hizo siasa za cuf ndio zilivyo. Jana nilikua naangalizia mdaharo huo kwenye kijiwe kimoja mashuhuri yaani, kuna dini fulani inakisakama cdm sana. Na hata ukiangalia kwa umakini wengi wanaopinga cdm huwa na ajenda ya udini. Angalia sana hili au lifanyie kazi.

anzisha post ingine hii haina uhusiano na thread hii huo ni mjadala mwingine tusitoke nje ya mada kwa makusudi
 
kama hakuhudhuria vikao ulitaka akae kimya bungeni na kusinzia kama wengine...? tulimchagua ili atusemee.. popote, kama sio kwenye kamati basi bungeni na kama sio bungeni basi mikutanoni...

aluta kuntinua.. acha awaamshe watz, na sasa wameanza kuamka mmojammoja mpaka nchi nzima iamke..!

sasa tusilalamike kwenye kamati alikokimbia Lissu kanuni za kutoa maoni hazibani kama bungeni. Kwenye kamati upo muda wa kutosha kuchambua hoja tofauti na bungeni na hilo Lissu anajua. kwenye kamati hakuna Rungu la spika. Tundu kakosea
 
Nadhani sababu za msingi za CDM kutoka nje ya bunge watanzania wengi hawajazijua
Imani yangu siku wakijua, hapo ndipo watakapoona kuwa ni mashujaa
Ni rahisi kuwalaumu kwa mtazamo uliofinyu kama huu
Nawasihi mjitafutie kujua siri ya wao kutoka nje kabla ya kuwalaumu
 
Kitu ambacho Celina Kombani na mleta mada hii hawajasema ni kama Lissu alikuwa Tarime siku zote ambazo kamati ilikuwa inakutana! Kwa maneno mengine madai ni kwamba Lissu hakuwahi kuhudhhuria vikao vya Kamati kwa sababu alikuwa Tarime!

Sasa turudi nyuma, Lissu alikwenda Tarime wakati wa sakata la mauaji ya Nyamongo na baada ya kufikishwa mahakamani Jaji alimuamuru asikanyage eneo hilo wakati wote wa kisa. Kesi bado haijaisha. Hivyo ili haya madai yawe sahihi inabidi Celina Kombani na mleta mada aseme kuwa vikao vyote vya kamati vilifanyika kabla ya Lissu kupewa amri na mahakama ya kukanyaga Tarime? Au Lissu aliendelea kukaka Tarime licha ya amri ya jaji ya kutafanya hivyo. Je hili ni kweli?

Pili, kwenye mdahalo jana (Star Tv) Lissu alisema kuwa hoja alizotoa bungeni na anazosema kwenye mdahalo ndizo hizo hizo alizotoa kwenye kamati. Je, Celina Kombani anaweza kutuambia Lissu alitoaje mchango wake kwenye kamati? kupitia kwenye simu? au video conference toka Tarime?!

Na mwisho, Lissu alisoka vikao siku ngapi? zote? kama ni siku moja au mbili hiyo inamfanya mtu asijue nini kiliongelewa? kamati haichukui minute? na je kuna wajumbe wengine waliokosa vikao? kwa muda gani? kukosa kwao kumewafanya wasijue nini kinaendelea? Na kama mjumbe hayupo kwenye kikao (physically) ina maana hana ruhusa ya kutoa maoni?
 
Kweli mti wenye matunda ndiyo hupigwa mawe, Lissu awepo asiwepo isingebadili kitu, hata hivyo kama hawajawahi kukutana toka April ile kamati ya katiba na sheria mlitaka awepo wapi? sidhani kama ni jambo la maana sana oooh Lissu kuhudhuria kwani yeye ndiye Kiwete?
 
Lisu ana haki kuwasilisha mawazo yake. Kwa wale unaoona anapiga kelele mmekosea. alichofanya Celina ni kumattack kujaribu kufunika uozo.. yani unaacha kujadili content unamjadili mtu tena unatafuta sababu dhaifu kabisa. alifanya sahihi kutokwenda. utashirikije wakati unajua watu tayari wamepanga mambo yaende wanavyotaka wao? angekuwa msindikizaji tu!!

Halima Mdee alikwenda kwenye kamati na wabunge wengine wa chadema je kutohudhuria ulikuwa ni msimamo wa chadema au msimamo binafsi wa Lissu? Huna maana kama huoni kwamba kutohudhuria vikao kwa Lissu nayo ni yaliyomo (content)
 
Hivi ulitaka asiendee kutetea watu waliokuwa wanaonewa huko Tarime, lakini huko kukosekana kwa hiyo siku umeambiwa alishindwa kutoa mchango wake wa mawazo. CCM NA WAKE ZENU CUF mtaweweseka sana
 
chadema wameshikwa pabaya wabishi hao hata kwenye hoja iliyo wazi ni heri tusio na chama. kama mnabisha kuwa Tundu hakukosea basi hakuna haja ya kushika dola mtakuwa wabishi zaidi na hamtashaurika kama CCM
" Chloroquine ni Chungu lakini ni Dawa"

Kwa hiyo kama ni wabishi hatuhitaji mabadiliko"Kwa hiyo unaridhika na hali tete ya nchi ilivyo chini ya Uongozi wa CCM? Kwa hiyo kama Tindu hakuwepo kwenye kikao mabadiliko muhimu ya Katiba hayawezi mpaka awepo yeye?Naona unaongea kama vile umetoka kuanguka kwenye mti.
 
Kitu ambacho Celina Kombani na mleta mada hii hawajasema ni kama Lissu alikuwa Tarime siku zote ambazo kamati ilikuwa inakutana! Kwa maneno mengine madai ni kwamba Lissu hakuwahi kuhudhhuria vikao vya Kamati kwa sababu alikuwa Tarime!

Sasa turudi nyuma, Lissu alikwenda Tarime wakati wa sakata la mauaji ya Nyamongo na baada ya kufikishwa mahakamani Jaji alimuamuru asikanyage eneo hilo wakati wote wa kisa. Kesi bado haijaisha. Hivyo ili haya madai yawe sahihi inabidi Celina Kombani na mleta mada aseme kuwa vikao vyote vya kamati vilifanyika kabla ya Lissu kupewa amri na mahakama ya kukanyaga Tarime? Au Lissu aliendelea kukaka Tarime licha ya amri ya jaji ya kutafanya hivyo. Je hili ni kweli?

Pili, kwenye mdahalo jana (Star Tv) Lissu alisema kuwa hoja alizotoa bungeni na anazosema kwenye mdahalo ndizo hizo hizo alizotoa kwenye kamati. Je, Celina Kombani anaweza kutuambia Lissu alitoaje mchango wake kwenye kamati? kupitia kwenye simu? au video conference toka Tarime?!

Na mwisho, Lissu alisoka vikao siku ngapi? zote? kama ni siku moja au mbili hiyo inamfanya mtu asijue nini kiliongelewa? kamati haichukui minute? na je kuna wajumbe wengine waliokosa vikao? kwa muda gani? kukosa kwao kumewafanya wasijue nini kinaendelea? Na kama mjumbe hayupo kwenye kikao (physically) ina maana hana ruhusa ya kutoa maoni?

hujamwelewa mtoa hoja sio kwamba anataka wewe umjibiye anataka Lissu atoe majibu ya shutuma dhidi yake kwani Kombani alisema alikuwa hahudhurii vikao vya kama na mtuma post kasema juni alikuwa tarime. Lissu aseme alihudhuria vikao vingapi na hakuhudhuria vikao vingapi na kwa nini ili na sisi tupime kama kuna uzito au alikosa kuwajibika. Unaona sasa mitaa wanasema Lissu alipewa milioni 4 ili afanye usanii wa kuwashawisha wenzake watoke bungeni kusudi CCM wabaki peke yao kuunda katiba?
 
kumlinda lissu kakati hoja hii tunakuwa hatumsaidii kujirekebisha

Sawasawa mkuu,.Nahisi huu mtindo utakuja kui cost CDM, manake watu wake wanaona kila kinachofanywa na CDM kipo right..hata kama wakikosea
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom