MAMA POROJO
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 4,976
- 784
Wakati wa kufunga muswada wa katiba, Waziri wa sheria na katiba Celina kombani alituambia watanzania kwamba anamshangaa Tundu Lissu anafunguka leo na kutoka bungeni na wanachadema wenzake wakati hakutokea kwenye vikao vya kamati ambako angeweza kutoa maoni yake. Kombani alisema, kwa mfano katika kikao cha mwezi juni, 2011 Lissu alikuwa Tarime wakati wajumbe wengine wakikutana kuandaa mchakato huo kwa ajili ya kuwakilishwa bungeni lakini pia Waziri alisema anayo orodha ya mahudhurio kuthibitisha kwamba Lissu hakuhudhuria. Katika hitimisho lake hilo Kombani alisema, wajumbe wengine kama Halima Mdee na wabunge wengine wa upinzani walihudhuria na walitoa maoni yao ambayo yamepokelewa na kufanyiwa kazi.
Kumbuka kamati hii iliundwa baada ya kukataliwa kwa muswada uliosomwa kwa mara ya kwanza ili kutatibu mchakato huo upya kabla hujasomwa kwa mara ya pili miongoni mwa wajumbe alikuwa Tundu Lissu ambaye taifa limetangaziwa kwamba hakuhudhuria vikao.
my take: 1. Ni kazi gani muhimu zilimbana Lissu kuliko unyeti wa katiba (moyo wa nchi)
2. lissu analetaje maoni yake bungeni wakati maoni hayo angeyatoa kwenye kamati
3. Lissu angehudhuria vikao vya kamati ya katiba angetuambia alitoa maoni gani ambayo hayakupokelewa.
4. Tundu Lissu huwezi kulitumia bunge kama kamati ndogo unawarudisha nyuma wengine.
5. Lissu tuombe radhi watanzania kwa kushindwa kutuwakilisha kwenye kamati
6. Lissu wewe ulikuwa muhimu sana kuanzia ngazi ya kamati ambako hukuhudhuria
7. tundu lissu ulitoa kipambele kwa mamabo mengine kuliko katiba?
Kumbuka kamati hii iliundwa baada ya kukataliwa kwa muswada uliosomwa kwa mara ya kwanza ili kutatibu mchakato huo upya kabla hujasomwa kwa mara ya pili miongoni mwa wajumbe alikuwa Tundu Lissu ambaye taifa limetangaziwa kwamba hakuhudhuria vikao.
my take: 1. Ni kazi gani muhimu zilimbana Lissu kuliko unyeti wa katiba (moyo wa nchi)
2. lissu analetaje maoni yake bungeni wakati maoni hayo angeyatoa kwenye kamati
3. Lissu angehudhuria vikao vya kamati ya katiba angetuambia alitoa maoni gani ambayo hayakupokelewa.
4. Tundu Lissu huwezi kulitumia bunge kama kamati ndogo unawarudisha nyuma wengine.
5. Lissu tuombe radhi watanzania kwa kushindwa kutuwakilisha kwenye kamati
6. Lissu wewe ulikuwa muhimu sana kuanzia ngazi ya kamati ambako hukuhudhuria
7. tundu lissu ulitoa kipambele kwa mamabo mengine kuliko katiba?