Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,346
- 26,138
Sasa iko wazi kuwa Zitto Kabwe ametangazwa kuvuliwa uanachama wa CHADEMA. Inajulikana kuwa sakata la Zitto lilianzia kwenye ulioitwa mkakati wa mabadiliko uliowahusisha pia Prof. Kitila Mkumbo na Samson Mwigamba.
Baada ya Mkakati wa Mabadiliko kuwekwa wazi/kugunduliwa,kikao cha Kamati Kuu cha CHADEMA kilifanyika kuwajadili wahusika. Waliohusishwa ni Zitto,Prof. Kitila na Mwigamba. Kikao husika kiliwavua nafasi za uongozi wahusika. Zitto alipokwa Unaibu Katibu Mkuu na Naibu Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.
Kuvuliwa uongozi kwa wahusika ulikuwa uamuzi wa dharura na wa haraka ili kupisha uchunguzi wa kina na kuandaliwa kwa mashtaka dhidi yao.
Mashtaka yaliandaliwa na kupelekwa kwa wahusika. Kikao kingine cha Kamati Kuu kiliitishwa. Kililenga kuwahoji,kujadili na kuamua juu ya mashtaka dhidi ya akina Zitto. Kabla ya kikao kufanyika,Zitto alikwenda Mahakama Kuu kuzuia kujadiliwa.
Wenzake hawakwenda Mahakamani. Walijadiliwa na kuvuliwa uanachama wao wa CHADEMA. Mahakamani Zitto alikuwa na maombi madogo na maombi makubwa. Madogo yalikuwa ya dharura. Ya kuizuia Kamati Kuu kumjadili. Ikumbukwe kuwa wakati Zitto anakwenda Mahakamani kikao hakikuwa kimefanyika.
Zitto alifanikiwa kupata zuio la muda kujadiliwa chamani na kimsingi hakujadiliwa kwenye Kamati Kuu iliyoitishwa na wala vikao vilivyofuata. Jaji John Utamwa pia alimuamuru Katibu Mkuu ampe Zitto mwenendo wa Kamati Kuu iliyompoka uongozi.
Mahakamani yalibaki maombi mengine ya kuendelea kuzuiwa kwa CHADEMA kumjadili Zitto hadi atakapowasilisha rufani yake Baraza Kuu. Ni maombi hayo ambayo Mawakili Wasomi wa CHADEMA waliyawasilishi pingamizi la awali.
Kisheria,pingamizi la awali huusiana hasa na mambo ya kisheria kama mamlaka ya mahakama,uwezo wa mwombaji wa kuweza kuomba,matakwa ya nyaraka na kadhalika. Linapowekwa pingamizi la awali,kesi au ombi ya msingi husimama.
Litakaposikilizwa pingamizi la awali na kukubaliwa,kesi ya msingi hutupwa. Linapokataliwa,kesi ya msingi huendelea. Ieleweke kuwa pingamizi la awali linasikilizwa na kuamuliwa rasmi kimahakama kwa kutolewa uamuzi.
Pingamizi la CHADEMA lilijikita hasa kwenye uhalali wa maombi ya Zitto kuwa Masjala kuu ya Mahakama Kuu ya Tanzania-High Court Main Registry. Ikadadavuliwa kuwa Zitto alipaswa kuwasilisha maombi yake Mahakama ya Hakimu Mkazi au Masjala ya Wilaya ya Mahakama Kuu-High Court District Registry.
Pingamizi likapangiwa siku ya kusikilizwa. Siku ilipofika timu za Mawakili wasomi wa wahusika zikajitokeza mahakamani,mbele ya Jaji Utamwa,na kusikilizwa juu ya pingamizi hilo. Mawakili wakaeleza hoja na kila mmoja akasikilizwa. Mwisho mwishoni,Jaji akapanga siku ya kutoa uamuzi juu ya pingamizi hilo ili ijulikane kama maombi ya Zitto yangeendelea kusikilizwa au la.
Baada ya Mkakati wa Mabadiliko kuwekwa wazi/kugunduliwa,kikao cha Kamati Kuu cha CHADEMA kilifanyika kuwajadili wahusika. Waliohusishwa ni Zitto,Prof. Kitila na Mwigamba. Kikao husika kiliwavua nafasi za uongozi wahusika. Zitto alipokwa Unaibu Katibu Mkuu na Naibu Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.
Kuvuliwa uongozi kwa wahusika ulikuwa uamuzi wa dharura na wa haraka ili kupisha uchunguzi wa kina na kuandaliwa kwa mashtaka dhidi yao.
Mashtaka yaliandaliwa na kupelekwa kwa wahusika. Kikao kingine cha Kamati Kuu kiliitishwa. Kililenga kuwahoji,kujadili na kuamua juu ya mashtaka dhidi ya akina Zitto. Kabla ya kikao kufanyika,Zitto alikwenda Mahakama Kuu kuzuia kujadiliwa.
Wenzake hawakwenda Mahakamani. Walijadiliwa na kuvuliwa uanachama wao wa CHADEMA. Mahakamani Zitto alikuwa na maombi madogo na maombi makubwa. Madogo yalikuwa ya dharura. Ya kuizuia Kamati Kuu kumjadili. Ikumbukwe kuwa wakati Zitto anakwenda Mahakamani kikao hakikuwa kimefanyika.
Zitto alifanikiwa kupata zuio la muda kujadiliwa chamani na kimsingi hakujadiliwa kwenye Kamati Kuu iliyoitishwa na wala vikao vilivyofuata. Jaji John Utamwa pia alimuamuru Katibu Mkuu ampe Zitto mwenendo wa Kamati Kuu iliyompoka uongozi.
Mahakamani yalibaki maombi mengine ya kuendelea kuzuiwa kwa CHADEMA kumjadili Zitto hadi atakapowasilisha rufani yake Baraza Kuu. Ni maombi hayo ambayo Mawakili Wasomi wa CHADEMA waliyawasilishi pingamizi la awali.
Kisheria,pingamizi la awali huusiana hasa na mambo ya kisheria kama mamlaka ya mahakama,uwezo wa mwombaji wa kuweza kuomba,matakwa ya nyaraka na kadhalika. Linapowekwa pingamizi la awali,kesi au ombi ya msingi husimama.
Litakaposikilizwa pingamizi la awali na kukubaliwa,kesi ya msingi hutupwa. Linapokataliwa,kesi ya msingi huendelea. Ieleweke kuwa pingamizi la awali linasikilizwa na kuamuliwa rasmi kimahakama kwa kutolewa uamuzi.
Pingamizi la CHADEMA lilijikita hasa kwenye uhalali wa maombi ya Zitto kuwa Masjala kuu ya Mahakama Kuu ya Tanzania-High Court Main Registry. Ikadadavuliwa kuwa Zitto alipaswa kuwasilisha maombi yake Mahakama ya Hakimu Mkazi au Masjala ya Wilaya ya Mahakama Kuu-High Court District Registry.
Pingamizi likapangiwa siku ya kusikilizwa. Siku ilipofika timu za Mawakili wasomi wa wahusika zikajitokeza mahakamani,mbele ya Jaji Utamwa,na kusikilizwa juu ya pingamizi hilo. Mawakili wakaeleza hoja na kila mmoja akasikilizwa. Mwisho mwishoni,Jaji akapanga siku ya kutoa uamuzi juu ya pingamizi hilo ili ijulikane kama maombi ya Zitto yangeendelea kusikilizwa au la.