Komeo Lachuma
JF-Expert Member
- Oct 31, 2014
- 11,163
- 22,739
Sijamsingizia yeyote. Moderators najua mtataka kuufuta huu uzi. Ila sijavunja kanuni yoyote.
Kwa umri samia hawezi kuwa na mtoto kama Tundu Lissu. Nakumbuka samia akiwa zanzibar alimwona Simba mmoja machachari yaani pamoja na kuwa kwenye cage bado hakuwa mnyonge.
Alikuwa akizunguka zunguka mle ndani kibabe na kutisha. Hapo samia akauliza yule simba anaitwa nani? Sikumbuki walijibu nini. Ila nakumbuka akasema haraka apewe jina la Tundu Lissu. Tundu Lissu ana roho ya Simba.
Hata Fisi miamoja Simba atapigana nao na hata wakimshinda kuna fisi nao watakuwa na hali mbaya sana.
Lakini pia wakati huo huo rais samia alisema yeye ni chura. Tena siyo chura tu wa kawaida. Yeye ni chura kiziwi. Hatujui tena chura huyo ana udhaifu gani mwingine. Ila sasa unapata picha katika ulimwengu wa roho. Nini kilimsukuma samia aseme hayo maneno?
Au watu wake walimshauri vibaya?au waandishi walimwandikia maneno vibaya? Yeye Chura na Tundu Lissu Simba?
Tuendeleeni kumwombea rais katika changamoto anazopitia na Mnyaazi Mungu atusikie sisi waja wake. Kama ilivyokuwa jana iwe na leo pia.
Kwa umri samia hawezi kuwa na mtoto kama Tundu Lissu. Nakumbuka samia akiwa zanzibar alimwona Simba mmoja machachari yaani pamoja na kuwa kwenye cage bado hakuwa mnyonge.
Alikuwa akizunguka zunguka mle ndani kibabe na kutisha. Hapo samia akauliza yule simba anaitwa nani? Sikumbuki walijibu nini. Ila nakumbuka akasema haraka apewe jina la Tundu Lissu. Tundu Lissu ana roho ya Simba.
Hata Fisi miamoja Simba atapigana nao na hata wakimshinda kuna fisi nao watakuwa na hali mbaya sana.
Lakini pia wakati huo huo rais samia alisema yeye ni chura. Tena siyo chura tu wa kawaida. Yeye ni chura kiziwi. Hatujui tena chura huyo ana udhaifu gani mwingine. Ila sasa unapata picha katika ulimwengu wa roho. Nini kilimsukuma samia aseme hayo maneno?
Au watu wake walimshauri vibaya?au waandishi walimwandikia maneno vibaya? Yeye Chura na Tundu Lissu Simba?
Tuendeleeni kumwombea rais katika changamoto anazopitia na Mnyaazi Mungu atusikie sisi waja wake. Kama ilivyokuwa jana iwe na leo pia.