Mheshimiwa Spika, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inaitaka Serikalikutoa kauli rasmi kama Rasimu ya Muswada waSheria ya Mapitio ya Katiba ndio inawakilisha msimamo wa Serikali juu yamchakato wa kutungwa kwa Katiba Mpya. Kama nihivyo, basi Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inapenda kuweka wazi msimamo wakeMuswada huu haukubaliki hata kidogo. Kwanza, Kambi Rasmi ya Upinzani haikubalianina mamlaka makubwa yanayopendekezwa kupewa Rais wa Jamhuri ya Muungano na Raiswa Zanzibarchini ya Muswada huu. Urais wa Kifalme kamakanuni kuu ya kikatiba na kisiasa ndiyo ambayo imetufikisha hapa tulipo leo:taifa lenye wananchi maskini, lililojaa ufisadi, lisilojali demokrasia na hakiza binadamu na lenye kuongozwa na watawala wasiowajibika kwa wananchi au kwavyombo vya uwakilishi vya wananchi. Mfumo huu hauwezi kutumika tena kulipatiataifa letu Katiba Mpya ya kidemokrasia itakayokidhi mahitaji ya karne hii nanyingine zijazo.
Pili, mapendekezo ya Rasimu ya Muswada hayakubalikikwa sababu yanaweka mchakato wa Katiba Mpya kwenye huruma na/au fadhila ya Raiswa Zanzibar na siasa za Zanzibar kwa ujumla. Kwa mapendekezo haya,Rais wa Zanzibarasipokubaliana na jambo lolote linalohitaji ridhaa yake basi mchakato mzimautasimama au kusitishwa. Aidha, endapo katika kura ya maoni inayopendekezwa,theluthi mbili ya Wazanzibari hawatakubaliana na Katiba Mpya basi Katiba hiyohaitapitishwa hata kama inakubaliwa kwa kiasikikubwa na wananchi wa Tanzania Bara. Mustakbala wa taifa letu hauwezi kuwekwa tenarehani kwenye siasa za Zanzibarna kwenye matakwa ya Wazanzibari kwa kiasi hicho. Kuhusiana na jambo hili,Kambi Rasmi ya Upinzani inapendekeza kwamba Rais wa Zanzibar ahusishwe tu katika masuala yakikatiba ambayo ni ya Muungano tu. Nje ya masuala hayo, Rais wa Zanzibar hana sababuyoyote ya kuhusishwa na mchakato wa kikatiba unaohusu mambo ya Tanzania Bara.Aidha, wajumbe wa Tume ya Mapitio ya Katiba ambaowatatoka Zanzibarwahusike tu katika mchakato wa masuala ya kikatiba ambayo ni ya Muungano tu.Vile vile, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inapendekeza wananchi wa Zanzibar washiriki katikakura ya maoni inayohusu mfumo mpya wa Muungano tu. Hii ndio kusema kwamba, kamavile ambavyo viongozi, wawakilishi na wananchi wa Tanzania Barahawajashirikishwa katika mchakato wa kikatiba wa Zanzibar kwa sababu ulihusumambo yasiyokuwa ya Muungano, vivyo hivyo viongozi, wawakilishi na wananchi waZanzibar wasishiriki katika mchakato wa kikatiba wa mambo yasiyokuwa yakikatiba kwa upande wa Tanzania Bara.