jmushi1
Platinum Member
- Nov 2, 2007
- 24,989
- 22,521
Maoni yako ni mazuri kama ungeondoa iyo repetence ya mara Father,mara Padre,nyie manajidai mnazungumza honestly behind ananymous screen names, lakini mna nia ya kisiasa. Ofcorse mnataka wale wanachama wa CDM ambao si wakristo wajione wanaongozwa na Padre ama kiongozi wa dini ya wakristo.Padre Dr.Willbroad Slaa,kwanza niseme nashukuru kwamba Kiongozi wa Ngazi ya juu sana katika Chama cha siasa unakuwepo katika kuchangia mada hapa katika forum za nanmna hii,hivyo kutuliza na kukidhi kiu ya wachangiaji wengi ambao huhitaji majibu na misimamo ya jikoni,nikimaanisha kutoka Chamani,ambako wewe ni mmojawapo ya wawakilishi wa moja kwa moja.
Father,ningependa nitangulize imani yangu kabla sijasema nitakacho sema
NINAAMINI KWAMBA SI MARA ZOTE KILE NINACHOKIAMINI NDIO KIWE CHA KWELI AU SAHIHI
NINAJUA KWAMBA MARA NYINGI BINADAMU TUNACHUKULIA KWAMBA MISIMAMO YETU NDIO ILIYO SAHIHI ZAIDI,NA ILE YA WENZETU SI SAHIHI KWA SABABU TUNAONA KWAMBA SISI NDIO SISI TU
NIAAMINI KWAMBA MARA NYINGI MAMBO KAMA VILE YA DINI,SIASA,NA MAPENZI YANAENDESHWA KI-USHABIKI ZAIDI(i.e 1.shabiki wa Simba hata siku moja hatokiri wazi ama kushawishika kwamba Yanga ni wazuri kuliko wao,hata kama itokee mathalani Yanga anaongoza na Simba anashikilia nafasi ya mwisho ,ama kinyume chake 2.M Protestant ni vigumu sana kumwelewa mkatoliki pale mkatoliki anapomwambia m protestant "Hapana,sisi hatuabudu sanamu,bali tunasujudu",kwa sababu tu Mprotestant hamwelewi vema Mkatoliki)
NINAAMINI KWAMBA WATU WENGI DUNIANI WANAONA WAZAZI WAO NDIO WA MAANA ZAIDI DUNIANI KWA SABABU TU NDIO WATU WA KARIBU ZAIDI NA WAO,NI WATU WANAOWATATULIA MATATIZO YAO,NA NDIO WATU WALIOWAFAHAMU KI UKARIBU ZAIDI TOKA UTOTO WAO....INGAWAJE WAZAZI HAWA KWA WATU WENGINE WATAONEKANA HAWAFAI KABISA(inawezekana ikawa kweli hawafai ama ni mtazamo tu wa hao watu wengine)
Father,kwa kusema hayo juu,si nia yangu ukubaliane nami nitakachokwambia,bali ni nia yangu kukushawishi wewe na wengine kwama tunahitaji kujua kwamba katika nchi hii hakutakuja tokea siku watu wote wakawa na mawazo yaleyale kwa sababu hawa watu wanatoka katika familia tofauti,kabila tofauti,dini tofauti,kanda tofauti,(vyote hivi vinachangia sana mtazamo wa mtu katika kuchanganua jambo lolote maishani)......NINAOMBA TUFIKIE MAHALI PA KUKUBALIANA KUTOKUKUBALIANA,hili ni jambo muhimu ili kuleta HESHIMA......JAZBA haitasaidia hasa pale tutakapoona mbona watu wanaonyesha kutokukubaliana na KILE SISI TUNACHOAMINI NDICHO CHA KWELI.....
HIVYO BASI;
NI VEMA UKAWASISITIZIA HAWA WANANCHI WALIO NA MSIMAMO WA UPANDE WA CHADEMA(sijui nimepatia hapa?au niseme msimamo wa mageuzi ya Katiba yanayoridhiwa na Chadema?au na vyama vya Upinzani?au na wana mageuzi ya katiiba?-niko tayari kusahihishwa,yawezekana nimekosea)kuacha KUZOMEA....na yule aliyesema kushangilia haikatazwi,naomba tuelewe kwamba katika saikolojia,Binadamu wote tuna hulka ya kupenda kusifiwa....NDIO maana nadhani tunaweza kubadilisha ujumbe wetu kwa KUWASHANGILIA wale wanaoongea tunachotaka,na kuwasikiliza na kukaa kimya kwa wale wanaoongea kile tusichotaka kukisikia......hili linahitaji UVUMILIVU,kwani saikolojia pia inasema mtu anapoongea kile usichotaka kukisikia,utatamani UMZOMEE,lakini kwa sababu ya kanuni ya KUHESHIMIANA ili kila mtu asikike,basi NI VEMA KUKUBALIANA KUTOKUKUBALIANA,i mean kukaa kimya mtu anapoongea kile tusichokipenda ili kutokuonyesha tumemdharau.
Father,mara nyingi kwenye siasa ni viongozi wanaoelewa ki undani zaidi real OBJECTIVES,na wananchi wengi huwa wanaendeshwa na USHABIKI zaidi.
TUPUNGUZE USHABIKI ILI SUALA HILI LA KATIBA LIFIKIE MUAFAKA WA MAJORITY.
TUJUE KWAMBA KILA UPANDE UNAWEZA KUSHINDA KILE INACHOTETEA(WANAMAGEUZI WANAWEZA KUSHINDA,WENYE MSIMAMO MWINGINE WANAWEZA SHINDA)
Nawakilisha.ninajua yawezekana mawazo yangu si sahihi,kwani ninaamini katika kukubaliana kutokukubaliana.
Ningeomba mwongozo kwenye hili,kiutaratibu kwenye medani za kisiasa,kama mtu aliwahi kuwa Rais,basi hata akistaafu,si ajabu kusikia akiwa referenced as "president",na mara nyingi huelezwa kuwa ni mstaafu.Sasa kwa upande wa Dr Slaa,yeye tayari yuko kwenye siasa na upadre alishaachana nao.Hilo uliheshimu.Ningependa kujua kama mtu ukiachana na upadre kama unaruhusiwa kuitwa padre.Na kama si sahihi,basi ni bora tu umwite Dr Slaa,ama katibu nk.