Duh Mzee wa watu kajifia na kinyongo kikubwa lakini laana ya kuwauza wazanzibar iliendelea kumtafuna hadi mauti yalipomkuta.
Mzee A Jumbe alikubali kuziunganisha TANU na ASP kwasababu aliamini Mwl Nyerere angempachika uRais wa JMT.Katika uhai wa muungano hakuna Rais wa Zanzibar aliyefanya ziara nyingi katika mikoa ya Tanganyika kama Mzee Jumbe hakuna na wala hatakuja kutokea hata siku moja.Inaelekea Mwl Nyerere alimwandaa lakini kuibuka kwa Marehemu Sokoine Waziri Mkuu wa wakati wake kulififisha ndoto za Jumbe kuchukua mikoba ya Mwl Nyerere ambaye tayari alishajiandaa kuondoka ikulu ya magogoni kilichochelewesha ni vita ya Kagera ilibidi Mwl aongeze muda kidogo.
Baada ya Jumbe kuona nyota ya Sokoine inazidi kuwaka akaanzisha madai ya kumezwa kama si Sokoine ambaye tayari alionekana wazi angechukua mikoba Jumbe asinge piga kelele wala kuleta madai ya kumezwa.Wakati TANU & ASP zinaunganishwa alijua wazi Zanzibar ingemezwa lakini tamaa ya madaraka ya wakati huo ilimnyamazisha.
Wale wote wanaomshabikia Jumbe wajiulize ni kwanini alikubali kuunganisha TANU & ASP halafu akaja kuikana baadae.Nini ilikuwa sababu ?????.