Tundu Lissu afunguka bungeni

Tundu Lissu afunguka bungeni

Kwa kweli hata mie nimemshangaa Tundu Lissu msomi wa sheria anakwenda kufanya reference kwenye magazeti ya udaku, magazeti yenyewe ndio haya Tanzania Daima, Uhuru, Kiu.
 
kwani magazeti hutoa habari za uwongo? Kama magazeti yanatoa habari za kweli basi LISSU yuko sahihi.
 
Tuache unazi wa Ki-chadema kwa hili Lissu kachemka yani ana mtumia Kubenea kama reference!
 
Lissu ni mropokaji tu hajui sheria, isipokuwa anajua uropokaji wa sheria na kiingereza chake ni cha kuunga unga, ni janga la kitaifa Lissu, Tundu ni mfa maji haichi kutapa tapa

Mkuu, ukizungumzia lugha, nawe waijua ipi? Maana kama ni kiswahili hapo kwenye weusi italic hapatafsiriki.
 
Kwa kweli hata mie nimemshangaa Tundu Lissu msomi wa sheria anakwenda kufanya reference kwenye magazeti ya udaku, magazeti yenyewe ndio haya Tanzania Daima, Uhuru, Kiu.

Ni Mwanasheria wa issue Mazingira na maji taka, hana utaalamu wa sheria nyingine.
 
dah..siku hizi hata magoti yana2mika kuwaza na si BRAIN.. pole xana kwa mtoa Thread..kafanyiwe upasuaji wa goti lako.
 
Tafadhali,maana wengine tulikuwa mbali na vyombo vya habari,walau tuisome.
 
Leo nimeshangaa sana tundu anatumia magazeti kukazia ushahidi wake kwa kuwataja watu walimtesa Dk ulimboka kwa kutumia magazeti, leo hivi kesho si atatumia magazeti ya UDAKU?

Kwa sababu yamefichua uozo unaogusa watu wako unasema ni udaku, lakini hao hao wakubwa zako kila kukicha ndio wanawaita waandishi wa habari! Unafiki ndio unasumbua watu. Bungeni kuna sehemu maalum ya waandishi wa habari hapo hapo mnawakashifu. Makinda alishajiingiza kwenye huu mtego wa kuropoka na yakamtokea puani.

Mwanahalisi limeandika alichokiongea Dr Ulimboka mwenyewe, na kama watu wangejishughulisha wangeangalia kwenye you tube. Lakini kwa sababu wamezoea cartoon za Tom & Jerry kama hizi anatuletea Kova na Mkenya wake wa kuchonga basi lazima muone Lissu na tatizo.

Kwa bahati nzuri, zilipendwa zimechuja na AG hana jipya. Mwaka jana Lissu kambwaga chini na ule muswada wake wa Katiba mpya. Na alikuwa na kejeli kama hizi za sasa, but 40 days letter bunge likakaa kurekebisha uvundo ule ule aliokuwa anautetea. Wakati mwingine sielewe kumbukumbu za watu zinaharibiwa na nini?
 
Inashangaza sana AG kutoka katika debeta premises na kuingia personal vendatta.Hiyo ni dalili ya inferiority complex

Nilishasema inabidi kesi zake nyingi alizohukumu zipitiwe upya kwa sababu mara nyingi ameonyesha incompetency ya hali ya juu

Nilitegemea muda alopewa angejaribu kutolea majibu changamoto nyingi zinazoikumba mahakama pamoja na ufafanuzi wa utata wa kikatiba juu ya uteuzi wa wakuu wa wilaya na mikoa ambao ni wabunge anatoa majibu yasiyo kuwa na msingi juu ya hoja za kambi ya Upinzani.

Hawa ndio wanaochangia kupoteza nuru ya Tanzania katika nyanja nyingi kwa kutokujua au kudhamiria kufanya kinyume na wajibu walio nao juu ya nchi yetu..!
 
Wengine hawalijui hili , ngoja pro cdm uwaone watakavyo kuijia juu, ila kiukweli jamaa leo kaaibisha sana, jamaa ni mchovu sana wa sheria. Na Lissu ni mtaalam wa sheria za mazingira na si mtaalam wa sheria za katiba

umekariri vibaya!!
 
It's painful to learn that the magamba government is creating political appointments and geographical boundaries at the expense of taxpayer's money for their political gains.
 
Leo nimeshangaa sana tundu anatumia magazeti kukazia ushahidi wake kwa kuwataja watu walimtesa Dk ulimboka kwa kutumia magazeti, leo hivi kesho si atatumia magazeti ya UDAKU?

Hivi magazeti ya Tanzania yanatatizo gani hasa? Au ni ufinyu wa watu kuelewa role ya media? Hivi mbona tunaona sehemu mbalimbali duniani viongozi wakiwajibika kwa yale yaliyoandikwa magazetini? Magazeti ya Tanzania yana nini hasa? Tubadilike bana. Rwanda watu wamekula mvua kwa kile walicho-publish. Such is the power of media. Kama gazeti halisemi ukweli kwanini serikali iendekeze u-ndugai (mpaka sasa sijamwelewa) kupuuza wakati sheria zinazo-govern media zipo? Kumbe basi kuna haja gani ya kusoma magazeti wakati kila kinachoandikwa hakipaswi kuaminiwa? Hebu nissaidieni wadau. Hii ni kero yangu namba moja kati ya kero mbili nilizonazo.
 
Hongera sana Tundu Lissu, mwisho wa UJINGA huu wa CCM ni katiba mpya.

Hivi yule FUNDI MCHUNDO Stella Manyanya alikuwepo? Tunaomba mtywekee hiyo hotuba ya Tundu Lissu hapa JF

Ha ha ha ha,'eti fundi mchundo'jf raha tupu!
 
Hongera sana Tundu Lissu kwa hotuba kali na kwa kuwawekea Mabwepande hii mistari
“Hatulazimiki kuendelea
na uongozi mbovu wa
Chama na Serikali. Wala tukiendelea na hali hii, bila
kubadili uongozi wa
Chama na Serikali, sina hakika kama tutafika huko
salama. Masuala muhimu ya nchi yetu
hayatashughulikiwa.... Na masuala mengine
muhimu ... yataachwa
yajitatue yenyewe.
Nasema katika hali kama hiyo sina hakika kama tutafika salama; na tukifika salama tukiwa na uongozi huu huu wa
Chama na Serikali mbele kutakuwa ni giza tupu. Majuto ni mjukuu, huja baadaye.” Mwl Nyerere.
 
Lissu anaweza kuwa peke yake upande ule wa upinzani na CCM wakaingia woooote kabisa na bado akawarusha kichurachura. Werema kashindwa vifungu vya sheria sasa amehamia kwenye personal vandetta. Na bado sielewi kwanini kwenye zama hizi za vyama vingi mwanasheria mkuu anakuwa bungeni kushindana na wawakilishi wa wananchi? Ushauri wake unatakiwa uishie kwenye baraza la mawaziri. basi.

Mawaziri wenye dhamana watetee kile wanacholeta bungeni, kama wanashindwa kukitetea watawezaje kuisamamia?
 
Back
Top Bottom