BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,015
Tunavuna aibu Wapinzani
Stella Nyemenohi
Daily News; Thursday,January 01, 2009 @20:00
BAADHI ya vyama vya upinzani vimeshutumu majibizano baina ya Chama cha Wananchi (CUF) na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kwa kuielezea hali hiyo kuwa ni fedheha kwa upinzani. Wakati chama cha Democratic (DP) kimesema ugomvi huo hauna maslahi yoyote kwa wananchi, kwa upande wa Chama cha Tanzania Labour (TLP), kimesema hiyo ni aibu ambayo upinzani unaivuna.
Ingawa Mwenyekiti wa TLP, Augustino Mrema alisema anaamini kuwa hali hiyo ya mikwaruzano ni ya mpito, lakini alisema kitendo cha vyama vya upinzani kutofautiana kunadhihirisha kuwa dhamana waliyopewa hawajaitambua.
Mrema ambaye alisisitiza kuwa vyama vya upinzani vinakwenda pabaya, alisema ipo haja ya kurudi katika meza ya mazungumzo hususani baada ya uchaguzi mdogo wa Mbeya Vijijini kumalizika.
Ni kweli tunavuna aibu. Fedheha tunapata, lakini najua tutafika mahala tutajitambua, alisema Mrema na kusisitiza kuwa shetani aliyejiingiza kati ya CUF na Chadema, anaathiri vyama vyote vya upinzani.
Hata hivyo, Mrema alisema pamoja na mikwaruzano hiyo kuwa ya muda hususan kutokana na Uchaguzi huo Mdogo wa Mbeya Vijijini, lakini alilaumu hatua ya vyama kutokufikia Mwafaka wa kusimamisha mgombea mmoja.
Alisema kama vyama vya upinzani vingeungana, ingelikuwa rahisi kuokoa mamilioni ya shilingi yanayotarajiwa kutumika katika kampeni. Alitoa mfano wa Chadema na kusema Sh milioni 120 ambazo chama hicho kilisema kitatumia, zingeunganishwa na zile za CUF, zingewezesha kukitikisa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi huo.
Naye Mwenyekiti wa DP, Mchungaji Christopher Mtikila alishutumu ugomvi baina ya CUF na Chadema kwa kusema hauna uhusiano wowote na maendeleo ya wananchi wa Mbeya Vijijini. Mtikila alisema, wanapogombana hawa wanajimaliza wenyewe. Alishauri ushindani wa vyama usiwe wa kukwaruzana bali uwe wa kutangaza sera zitakazowavuta wananchi.
Tangu mchakato wa uchaguzi Mbeya Vijijini uanze, kumekuwapo na majibizano baina ya CUF na Chadema. Juzi, CUF ilikaririwa katika taarifa yake ikiishutumu Chadema kuwa haiheshimu makubaliano ya kuanzishwa kwa umoja wa upinzani.
Stella Nyemenohi
Daily News; Thursday,January 01, 2009 @20:00
BAADHI ya vyama vya upinzani vimeshutumu majibizano baina ya Chama cha Wananchi (CUF) na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kwa kuielezea hali hiyo kuwa ni fedheha kwa upinzani. Wakati chama cha Democratic (DP) kimesema ugomvi huo hauna maslahi yoyote kwa wananchi, kwa upande wa Chama cha Tanzania Labour (TLP), kimesema hiyo ni aibu ambayo upinzani unaivuna.
Ingawa Mwenyekiti wa TLP, Augustino Mrema alisema anaamini kuwa hali hiyo ya mikwaruzano ni ya mpito, lakini alisema kitendo cha vyama vya upinzani kutofautiana kunadhihirisha kuwa dhamana waliyopewa hawajaitambua.
Mrema ambaye alisisitiza kuwa vyama vya upinzani vinakwenda pabaya, alisema ipo haja ya kurudi katika meza ya mazungumzo hususani baada ya uchaguzi mdogo wa Mbeya Vijijini kumalizika.
Ni kweli tunavuna aibu. Fedheha tunapata, lakini najua tutafika mahala tutajitambua, alisema Mrema na kusisitiza kuwa shetani aliyejiingiza kati ya CUF na Chadema, anaathiri vyama vyote vya upinzani.
Hata hivyo, Mrema alisema pamoja na mikwaruzano hiyo kuwa ya muda hususan kutokana na Uchaguzi huo Mdogo wa Mbeya Vijijini, lakini alilaumu hatua ya vyama kutokufikia Mwafaka wa kusimamisha mgombea mmoja.
Alisema kama vyama vya upinzani vingeungana, ingelikuwa rahisi kuokoa mamilioni ya shilingi yanayotarajiwa kutumika katika kampeni. Alitoa mfano wa Chadema na kusema Sh milioni 120 ambazo chama hicho kilisema kitatumia, zingeunganishwa na zile za CUF, zingewezesha kukitikisa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi huo.
Naye Mwenyekiti wa DP, Mchungaji Christopher Mtikila alishutumu ugomvi baina ya CUF na Chadema kwa kusema hauna uhusiano wowote na maendeleo ya wananchi wa Mbeya Vijijini. Mtikila alisema, wanapogombana hawa wanajimaliza wenyewe. Alishauri ushindani wa vyama usiwe wa kukwaruzana bali uwe wa kutangaza sera zitakazowavuta wananchi.
Tangu mchakato wa uchaguzi Mbeya Vijijini uanze, kumekuwapo na majibizano baina ya CUF na Chadema. Juzi, CUF ilikaririwa katika taarifa yake ikiishutumu Chadema kuwa haiheshimu makubaliano ya kuanzishwa kwa umoja wa upinzani.