Habari wanabodi
Kila mtu anafahamu hali ya kisiasa iliyopo nchini kwa sasa. Kumekuwa na kauli za shutuma nyingi na vitisho kwa Spika wa Bunge la JMT dhidi ya mkaguzi n mdhibiti wa hesabu za serikali.
Ndugai anaongea hadharani kwamba alitarajia Prof Assad ajiuzulu baada ya vitisho vyake vya kumkamata na pingu. Watanzania wote hatuoni kosa la Prof Assad, ni kweli bunge ni dhaifu na Ndugai mwenyewe dhaifu na kama sio dhaifu basi ni kibaraka wa jiwe.
Kuna kauli yake moja Ndugai anasema Prof Assad anampa "wakati mgumu" mheshimiwa Rais....swali, CAG anampaje wakati mgumu Rais?
Rais anashindwa kufanya kazi zake? Au akiibua madudu wanavulika nguo wateule wake na hivyo naye anatapa aibu? Maana zile samosa na chapati za bil 1 si mchezo. Na mkulu kakaa kimya as if hakijatokea kitu. Si anasemaga mtu umemkamata red handed uchunguzi wa nini? Weka ndani. Mbona jamaa wamekula samosa za bil 1 na mnawaacha tu?
Ushauri wangu tuweke shinikizo Ndugai ajiuzulu. Na hili likifanikiwa itampa picha halisi jiwe kuwa hata yeye mwenyewe sisi "wenye nchi" tukiamua aondoke pale nyumba nyeupe ataondoka. Na wale wanaotumika kulinda maslahi yake. Policcm, tawi jipya la ccm jw na tisi. Maana hawa wameacha uzalendo walioapa wa kuilinda katiba sasa hivi wana agenda moja ya kulinda chama.
Nina hasira sana na upumbavu wa chama chao.
Hafai. Bure kabisa! Ajiuzulu fasts!Tulieni, taratibu, tuna plan kitu kitachacho trend ili kufifisha issue ya CAG... coming soon...
Cc: mahondaw
AJIUZULU siyo kujitathimini. hili lispika limeingiliwa na panya,mende,kunguni,viroboto na chawaNdugai ajitathmini
Ndugu zangu hasa kaka zangu ambao mmekuwa mkishiriki mijadala mbalimbali hapa JF, napenda kuwahakikishia kwa mara nyingine tena kuwa CAG ameshasukiwa mbinu ya kumwondoa madarakani.
Mara nyingi nimekuwa nikitoa taarifa au kuandika baadhi ya post na hakika mambo yamekuwa yakitokea kama nilivyo predict..
Wapo wataalamu wa kubeza posts za watu wengine bila kufanya utafiti, nakumbuka niliwahi ku post kuwa nimepokea taarifa kutaka Tanzania kuwa Lissu kashambuliwa kwa risasi, mtu wa kwanza ku comment aliishia kunitukana, kuwa mimi ni muongo na chizi.
Tarehe 8/01/2019 nili post thread kibarua cha CAG kuota nyasi, naamini ndicho kinachoenda kutokea.
Upo mpango wa kuhakikisha CAG anaondolewa ofisini na mkakati huo unaongozwa na Speaker, na unazo baraka zote kutoka juu, amini usiamini hata kama ingakuwaje mwaka huu hauwezi kwisha CAG akiwa ofisini.
Mbaya zaidi wakubwa wanahisi kuwa CAG anatumika na wapinzani kuikomoa serikali ya ccm na kuvujisha siri kwa wapinzani kwa malengo ya kuichonganisha serikali kwa wananchi ambao waliokwisha kuamini kuwa hii ndio serikali pekee yenye nia ya kukomesha rushwa nchini.
CAG lazima aondolewe madarakani, hiyo ndio kaulimbiu iliyopo mioyoni mwa wazalendo namba moja