Tunapoteza muda na demokrasia. Ni bora mara mia kutawaliwa "kidikteta" kuliko kidemokrasia

Wakili wa shetani

JF-Expert Member
Nov 22, 2022
1,689
3,259
Kwa nini tunaendelea kupoteza muda kuwa au kufuatilia mfumo wa kidemokrasia na ushahidi unaonyesha wazi kuwa ni mfumo mbovu usiofaa kitu!!? Critics mmoja alisema kuwa tofauti kubwa ya mfumo wa kidemokrasia na kidikteta ni kuwa kwenye mfumo wa kidikteta walaji ni wachache na mfumo wa kidemokrasia walaji ni wengi. Kwenye mfumo wa kidikteta ili utawale unahitaji kuwaridhisha watu wachache wenye nguvu. Lakini kwenye mfumo wa kidemokrasia unahitaji kuwaridhisha watu wengi sana. Yaani kwenye demokrasia walamba asali wanakuwa wengi sana kuliko kwenye udikteta.

Ushahidi wa wazi unaonyesha kuwa nchi za kidikteta zinaendelea au zina uwezekano mkubwa wa kuendelea kuliko za kidemokrasia. Nchi kama Morocco inayoendeshwa na mfalme mwenye mamlaka yote imeendelea sana katika Afrika. Misri ni nchi iliyoendelea katika Afrika, walitaka kujaribu Demokrasia lakini waliona kabisa wanaelekea shimoni. Libya inajaribu kujenga deokrasia lakini vurugu tupu. South Africa toka ianzishe utawala wa kidemokraisa inadidimia kwa kasi ya ajabu. Nigeria na Ethiopia zipo karibu kugawanyika na demokrasia zao.

Hata hapa toka tuanze kutumia demokrasia hakuna cha maana tulichofanya zaidi ya walamba asali kuendelea kujitajirisha. Hata hatuna tofauti yeyote na nchi kama Uganda inayoendeshwa kidikteta kwa miaka zaidi ya 30. Hatuna tofauti yeyote na Rwanda. Hatuwezi kukaa na kusema kuwa kwetu au kufuatilia kwetu demokrasia kumetufaidisha hiki na kile ukilinganisha na nchi za kidikteta. Ni kweli una nchi zina madikteta na hovyo, lakini zipo nyingi zenye madikteta wanaojielewa wanaoendeleza nchi zao. Lakini kwenye demokrasia kiongozi awe mzuri au mbaya hawezi kuendeleza nchi yake. Mfumo haumruhusu kabisa.

Inabidi tukae chini na kuachana na hiki kiini macho cha Demokrasia, kinatupotezea muda. Pengine tukiumiza kichwa tunaweza kupata mfumo mzuri, lakini ukweli wa wazi ni kuwa nchi ya kidikteta ina uwezekano mkubwa kuenelea kuliko nchi yenye au inayofuatilia demokrasia.
 
Kwa nini tunaendelea kupoteza muda kuwa au kufuatilia mfumo wa kidemokrasia na ushahidi unaonyesha wazi kuwa ni mfumo mbovu usiofaa kitu!!? Critics mmoja alisema kuwa tofauti kubwa ya mfumo wa kidemokrasia na kidikteta ni kuwa ini ukweli wa wazi ni kuwa nchi ya kidikteta ina uwezekano mkubwa kuenelea kuliko nchi yenye au inayofuatilia demokrasia.
JPM alikuwa mwamba wa Tanzania

USSR
 
Kama Dictator wa Korea kaskazini na ule wa Mabutu seseko Hapana hawa waliji neemesha wao tu. Lakini wa Gaddafi naona sawa ingawa kaiba ila wananchi nao wamepata mafanikio. Ila kwa hapa bongo Demokrasia na Dictatorship hauna maana. Wenye chama kikuu ndio wala nyama
 
Kwa nini tunaendelea kupoteza muda kuwa au kufuatilia mfumo wa kidemokrasia na ushahidi unaonyesha wazi kuwa ni mfumo mbovu usiofaa kitu!!? Critics mmoja alisema kuwa tofauti kubwa ya mfumo wa kidemokrasia na kidikteta ni kuwa kwenye mfumo wa kidikteta walaji ni wachache na mfumo wa kidemokrasia walaji ni wengi. Kwenye mfumo wa kidikteta ili u
Naunga mkono hoja
P
 
Kwa nini tunaendelea kupoteza muda kuwa au kufuatilia mfumo wa kidemokrasia na ushahidi unaonyesha wazi kuwa ni mfumo mbovu usiofaa kitu!!? Critics mmoja alisema kuwa tofauti kubwa ya mfumo wa kidemokrasia na kidikteta ni kuwa zi ni kuwa nchi ya kidikteta ina uwezekano mkubwa kuenelea kuliko nchi yenye au inayofuatilia demokrasia.
Correct especially Africa, specifically Tanzania.
 
Sukuma gang lililomkumbuka Mungu wao dikteta muuaji, mporaji, mtekaji na mpiga watu kwa risasi. Pole !

Haitakaa itokee tena sukuma gang kupewa hii nchi tena ili muue na kupora watu.
Wewe tatizo lako kila jambo JPM huyo alishakufa na tuna songa mbele!
Demokrasia ni shimo la uharibifu kwa waafrica na nizao na kuua familia na kuvunja maadili!
Ukimuona mwanasiasa anazungumzia demokrasia hawezi kuwa mbali na USHOGA!
 
Wewe tatizo lako kila jambo JPM huyo alishakufa na tuna songa mbele!
Demokrasia ni shimo la uharibifu kwa waafrica na nizao na kuua familia na kuvunja maadili!
Ukimuona mwanasiasa anazungumzia demokrasia hawezi kuwa mbali na USHOGA!
Hizi ni akili za sukuma gang. Bora Mungu wenu kafa mmebaki wakiwa, mngeinajisi nchi kwa ushamba na ulimbukeni wenu huu.
 
Back
Top Bottom