Freesoule
JF-Expert Member
- Jun 18, 2013
- 269
- 272
Tunapozungumzia maendeleo ya watu badala ya maendeleo ya vitu, CCM na wapambe wa Rais Magufuli huwa hawaelewi kabisa. Trevor Noah kutoka The Daily Show with Trevor Noah anamhoji mkurugenzi wa shirika la fedha duniani (IMF), Bi Christine Lagarde kuelekea mkutano ujao wa mataifa 20 yenye uchumi mkubwa zaidi duniani (the G20).
Trevor Noah anamuuliza Bi Christine Lagarde kwa nini ni muhimu kuwekeza kwenye huduma za kijamii kama hospitali na shule badala ya sekta za kiuchumi zinazotumia mafuta (fossil fuels) ambazo pengine zinadaiwa kukuza uchumi kuliko sekta za kijamii kama hospitali na shule.
Bi Christine Lagarde anaanza kujibu kwa kusema "Kwanza kabisa inasaidia kwa kupunguza matabaka. Kama watoto wadogo kutoka sehemu zote ulimwenguni, hasa zile zenye kipato cha chini, wataweza kwenda shule, watakuwa kwenye nafasi nzuri zaidi". Anazidi kusema kuwa "wanawake, kwa mfano, badala ya kutembea maili kadhaa kuchota maji, kama ilivyo katika nchi nyingi, wataweza kufikiwa na barabara na kuzitumia hizo barabara kusafirisha maji bila kupoteza muda; ikiwa watoto wanazaliwa hospitalini ambako kuna huduma inayofaa, ni wazi kuwa watakuwa mahala pazuri zaidi maisha yao yote. Kwa hiyo kwa kufanya hivyo unaboresha maisha ya watu, siyo leo, pengine si kesho, lakini ndani ya miaka mitano au kumi ijayo, kwa sababu hilo ni muhimu sana kwa ajili ya baadaye"
Hii ni sehemu ndogo ya wazo zima lakini hata IMF inatambua wazi kuwa ni muhimu zaidi kuwekeza kwenye miradi ambayo inawagusa wananchi moja kwa moja. Nilitegemea sisi ambao ndio tunapigana na umasikini tungekuwa na uelewa mpana zaidi juu ya hili lakini siyo picha ninayoiona hapa kwetu Tanzania.
Mazungumzo yapo hapa chini na unaweza kutazama hasa kuanzia dakika ya 3:00.
Trevor Noah anamuuliza Bi Christine Lagarde kwa nini ni muhimu kuwekeza kwenye huduma za kijamii kama hospitali na shule badala ya sekta za kiuchumi zinazotumia mafuta (fossil fuels) ambazo pengine zinadaiwa kukuza uchumi kuliko sekta za kijamii kama hospitali na shule.
Bi Christine Lagarde anaanza kujibu kwa kusema "Kwanza kabisa inasaidia kwa kupunguza matabaka. Kama watoto wadogo kutoka sehemu zote ulimwenguni, hasa zile zenye kipato cha chini, wataweza kwenda shule, watakuwa kwenye nafasi nzuri zaidi". Anazidi kusema kuwa "wanawake, kwa mfano, badala ya kutembea maili kadhaa kuchota maji, kama ilivyo katika nchi nyingi, wataweza kufikiwa na barabara na kuzitumia hizo barabara kusafirisha maji bila kupoteza muda; ikiwa watoto wanazaliwa hospitalini ambako kuna huduma inayofaa, ni wazi kuwa watakuwa mahala pazuri zaidi maisha yao yote. Kwa hiyo kwa kufanya hivyo unaboresha maisha ya watu, siyo leo, pengine si kesho, lakini ndani ya miaka mitano au kumi ijayo, kwa sababu hilo ni muhimu sana kwa ajili ya baadaye"
Hii ni sehemu ndogo ya wazo zima lakini hata IMF inatambua wazi kuwa ni muhimu zaidi kuwekeza kwenye miradi ambayo inawagusa wananchi moja kwa moja. Nilitegemea sisi ambao ndio tunapigana na umasikini tungekuwa na uelewa mpana zaidi juu ya hili lakini siyo picha ninayoiona hapa kwetu Tanzania.
Mazungumzo yapo hapa chini na unaweza kutazama hasa kuanzia dakika ya 3:00.