Tunaposema maendeleo ya watu badala ya vitu, msikilizeni boss wa IMF, Christine Lagarde

halafu kibaya ziadi watanzania wengi hawafahamu kuwa elimu na afya si sekta za kuongeza pato la taifa ila za kusaidia tu jamii. zitakapojengwa hospitali na shule ni nani atazihudumia kama hakuna uzalishaji kwa sekta za mafuta, nishati na miundombinu? tunataka tufike mahali tuuze elimu kwa gharama kuongeze pato la taifa? hiyo kauli ya huyo mama mfaransa imekaa kushoto sana. kwa hiyo uzalishaji usifanyike kuhudumia sekta zisizozalisha?

Serikali inajukumu la kuhakikisha elimu bora na kuhakikisha afya bora kwa wananchi wake. Hii ni kwa kushirikiana na Sekta Binafsi. Hata hivyo kwa kuwa ni Sekta za huduma muhimu, hapa ndio kodi za wananchi zinatakiwa zitumike kwa ufasaha. Sekta za viwanda, biashara na miundombinu zinapaswa kujengwa na sekta binafsi. Serikali kazi yake ni kuhakikisha mazingira bora ya uwekezaji, kutoa dira ya muda mfupi na muda mrefu, kusimamia sera na kukusanya kodi. Serikali haipaswi kufanya biashara!

Hiyo elimu unayotaka tuuze, ni elimu ipi? umuuzie nani? Tusipowekeza kwenye hiyo elimu ipaswavyo, tutaendelea kuimport wataalam kwenye hizo sekta zinazozalisha na watanzania wengi tutabaki vibarua, mamantilie na wachache kwenye nafasi za kati. Na hata hali hiyo haitodumu kwa muda mrefu maana teknolojia inakuja kunyakuwa hizo kazi ndani ya miaka michache.

Tunaleta mchezo kwenye maisha ya watu. Sasa hivi watanzania tunazidi milioni 55, huku nusu ya idadi ya watu ni chini ya miaka 30. Do the math
 
huoni umeandika takataka ambazo zinakutapisha mwenyewe, ajabu kwelikweli kwenye jamii na wewe unaitwa msomi. Tanzania ni nchi yenye vivutio vingi vya utalii , kwa watalii wa ndani na watalii wa nje na moja ya njia za kukuza na kuimarisha utalii ni kuendeleza miundombinu hususani viwanja vya ndege na kuboresha huduma za ndege. leo taifa linanufaika na utalii kwa sababu ya serikali kuwa na ndege za kuhudumia watalii.

mapato yanayotokana na utalii ambayo yamechagizwa na ununuzi wa ndege yameongezeka na matunda yake yameonekana katika kuendelea kuhudumia huduma za jamii kama afya( ujenzi wa vituo vya afya zaidi ya 260 na hospitali za wilaya 67), maji( miundombinu ya maji inajengwa kwa kasi), elimu( elimu bure, mikopo elimu ya juu, uboreshaji wa elimu ya veta), hayo ni baadhi tu ya faida za kununua ndege. kwa mawazo yako huduma za jamii zitaboreshwaje bila kuwa na chanzo cha mapato na za uzalishaji?
Hebu leta vielelezo au takwimu kudhihirisha kwamba ununuzi wa ndege umechagiza maendeleo kwenye sekta ya utalii. Please prove me wrong kwamba hutuletei siasa uchwara hapa
 
Serikali inajukumu la kuhakikisha elimu bora na kuhakikisha afya bora kwa wananchi wake. Hii ni kwa kushirikiana na Sekta Binafsi. Hata hivyo kwa kuwa ni Sekta za huduma muhimu, hapa ndio kodi za wananchi zinatakiwa zitumike kwa ufasaha. Sekta za viwanda, biashara na miundombinu zinapaswa kujengwa na sekta binafsi. Serikali kazi yake ni kuhakikisha mazingira bora ya uwekezaji, kutoa dira ya muda mfupi na muda mrefu, kusimamia sera na kukusanya kodi. Serikali haipaswi kufanya biashara!

Hiyo elimu unayotaka tuuze, ni elimu ipi? umuuzie nani? Tusipowekeza kwenye hiyo elimu ipaswavyo, tutaendelea kuimport wataalam kwenye hizo sekta zinazozalisha na watanzania wengi tutabaki vibarua, mamantilie na wachache kwenye nafasi za kati. Na hata hali hiyo haitodumu kwa muda mrefu maana teknolojia inakuja kunyakuwa hizo kazi ndani ya miaka michache.

Tunaleta mchezo kwenye maisha ya watu. Sasa hivi watanzania tunazidi milioni 55, huku nusu ya idadi ya watu ni chini ya miaka 30. Do the math
Very well put 🙌
 
Hiyo kauli ya maendeleo ya vitu sijaielewa mpaka leo inamaanisha nini labda mnisaidie. kikawiada vitu vinavyojengwa ni kwa ajili ya watu na maendeleo yao kama ni barabara, reli, nadaraja yote yanajengwa kwa ajili ya watu, hiyo kauli ya maendeleo ya vitu ina mashiko gani?

Maendeleo ya vitu daima hupelekea maendeleo ya watu ila leo watanzania tunalishwa yasiyolika na tunameza bila kutafuna. ni wapi marekani utakuta hakuna lami, reli au viwanja vya ndege? serikali yao ilijenga miundombinu hiyo ili kuwanufaisha watu, kwa nini sio kwetu tz?

Miradi ipi ambayo serikali imeanzisha haiwanufaishi watu? mradi wa SGR umetoa ajira nyingi kwa watanzania, barabara zimerahisha usafirishaji, n.k hiyo yote ni kuonesha miundombinu lazima ilete maendelo ya watu. unachopinga ni nini? Taja walau mradi mmoja ambao watu hawanufaiki au hawatonufaika ukikamilika?
Sijui anamaanisha watu wasifanye kazi walale kwao,serikali iwe inapita kila siku kila nyumba kugawa pesa.

Ila misemo ya watanzania kugeuka geuka kila siku tulishawahi kusema Rwanda ka nchi kadogo kana ndege zake lakini leo tumegeuka tunasema ndege za nini
 
huoni umeandika takataka ambazo zinakutapisha mwenyewe, ajabu kwelikweli kwenye jamii na wewe unaitwa msomi. Tanzania ni nchi yenye vivutio vingi vya utalii , kwa watalii wa ndani na watalii wa nje na moja ya njia za kukuza na kuimarisha utalii ni kuendeleza miundombinu hususani viwanja vya ndege na kuboresha huduma za ndege. leo taifa linanufaika na utalii kwa sababu ya serikali kuwa na ndege za kuhudumia watalii.
Ufaransa ni moja ya taifa linaloongoza kwa kupokea watalii wengi kwa mwaka duniani. Lakini serikali ya Ufaransa haimiliki shirika lake la ndege kwa asilimia 100! Serikali ya Ufaransa ina less than 18% ya shares za Air France-KLM. Serikali ya Tanzania iliyo maskini wa kutupwa inajifanya kumiliki 100% ya biashara ya ndege. Jambo ambalo serikali ya nchi tajiri duniani halilifanyi tena!

Uboreshaji wa utalii ni multifaceted na complex venture. Siyo rahisi kama ulivyosema. Ni muunganiko wa mambo mengi. Ikiwemo kuacha mentality ya Jiwe ya kusema Tanzania haihitaji watalii maskini. Watalii wengi kutoka nchi za nje ni wale wanaodunduliza pesa, na wala si matajiri. Hivyo, masuala kama ada za utalii, gharama za malazi, usafiri na chakula lazima yazingatie hilo. Kwa wale wanaotaka exclusivity basi kuwe na soko la ku-carter mahitaji yako. Lakini assumption ya kwamba watalii wanaokuja ni matajiri, haifai.
 
Sijui anamaanisha watu wasifanye kazi walale kwao,serikali iwe inapita kila siku kila nyumba kugawa pesa.

Ila misemo ya watanzania kugeuka geuka kila siku tulishawahi kusema Rwanda ka nchi kadogo kana ndege zake lakini leo tumegeuka tunasema ndege za nini
Tatizo akili zenu zinalala mno, hamuwezi kwenda na nyakati. Kwamba Rwandair inatengeneza hasara hilo hulijui? Na utujulishe kama ndege za Rwandair zilinunuliwa kwa pesa taslimu kama za Air Tanzania
 
halafu kibaya ziadi watanzania wengi hawafahamu kuwa elimu na afya si sekta za kuongeza pato la taifa ila za kusaidia tu jamii. zitakapojengwa hospitali na shule ni nani atazihudumia kama hakuna uzalishaji kwa sekta za mafuta, nishati na miundombinu? tunataka tufike mahali tuuze elimu kwa gharama kuongeze pato la taifa? hiyo kauli ya huyo mama mfaransa imekaa kushoto sana. kwa hiyo uzalishaji usifanyike kuhudumia sekta zisizozalisha?
Hapo wanazungumzia pesa za kodi ambazo Serikali inazipata ,, inatakiwa zitumike kwenye huduma muhimu zaidi zinazogusa watu moja kwa moja, kama Elimu na afya. ....Hapo watu binafsi hawazuiwi kuwekeza kwenye miradi ya uzalishaji ambayo itafanya serikali iendelee kukusanya kodi... Uwekezaji kama wa ndege unaweza kufanywa na watu binafsi kama wanaona fursa......zile pesa za ndege zingeweza kujenga shule bora na Hospitali za maana,, na pia kuimarisha miundombinu ya kilimo cha umwagiliaji.
 
halafu kibaya ziadi watanzania wengi hawafahamu kuwa elimu na afya si sekta za kuongeza pato la taifa ila za kusaidia tu jamii. zitakapojengwa hospitali na shule ni nani atazihudumia kama hakuna uzalishaji kwa sekta za mafuta, nishati na miundombinu? tunataka tufike mahali tuuze elimu kwa gharama kuongeze pato la taifa? hiyo kauli ya huyo mama mfaransa imekaa kushoto sana. kwa hiyo uzalishaji usifanyike kuhudumia sekta zisizozalisha?
Huelewi ulichoandika. Hivi kwanini Ndugai akienda kutibiwa India hivi Ni watu wangapi hapa Tanzania wanahitaji huduma Kama aliyopata Ndugai huko India? Tangu lini usafiri wa ndege ukawa issue kubwa Kama ya mabasi ya mikoani hasa WAKATI wa mwisho wa mwaka?
 
Back
Top Bottom