Meneja Wa Makampuni
JF-Expert Member
- Jul 7, 2020
- 8,988
- 11,862
Tunaokolewa kwa imani katika Yesu Kristo na sio kwa kufuata SHERIA.
Tunahesabiwa haki kwa imani ndani ya Yesu Kristo na si kwa matendo ya sheria. Wokovu ni kwa neema kupitia imani ya Yesu Kristo, si kwa jitihada za kufuata sheria.
YESU ANASEMA MKINIPENDA MTAZISHIKA AMRI ZANGU.
KUSHIKA AMRI KIKAMILIFU KUNAKUJA BAADA YA KUMPENDA YESU
KAZI YA SHERIA
1. Sheria huonyesha dhambi, ila haiondoi dhambi
2. Mtu mwenye dhambi hawezi kusamehewa kwa kuanza kufuata sheria bali ataepuka dhambi mpya huku akiwa na zile dhambi za mwanzo.
Yesu ndiye njia ya kweli na uzima. Na moja ya uzima ndio pamoja na uzima katika mwili yaani kuangamiza tamaa zote za mwili ambazo ni uzinzi, uuaji, uasherati, ibaada za sanamu, uongo, wizi, ujambazi, ulevi, fitina, ubinafsi, uchawi, mawazo mabaya, tamaa mbaya, uchafu, ufisadi, ugomvi, wivu, hasira, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo.
Basi ukisha kuwa na imani katika Yesu Kristo anakupatia kiongozi yaani Roho Mtakatifu atakaye kuongoza katika upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi kwasababu upo ndani ya Kristo Yesu yaani tumeusulibisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake mbaya.
Tunahesabiwa haki kwa imani ndani ya Yesu Kristo na si kwa matendo ya sheria. Wokovu ni kwa neema kupitia imani ya Yesu Kristo, si kwa jitihada za kufuata sheria.
YESU ANASEMA MKINIPENDA MTAZISHIKA AMRI ZANGU.
KUSHIKA AMRI KIKAMILIFU KUNAKUJA BAADA YA KUMPENDA YESU
KAZI YA SHERIA
1. Sheria huonyesha dhambi, ila haiondoi dhambi
2. Mtu mwenye dhambi hawezi kusamehewa kwa kuanza kufuata sheria bali ataepuka dhambi mpya huku akiwa na zile dhambi za mwanzo.
Yesu ndiye njia ya kweli na uzima. Na moja ya uzima ndio pamoja na uzima katika mwili yaani kuangamiza tamaa zote za mwili ambazo ni uzinzi, uuaji, uasherati, ibaada za sanamu, uongo, wizi, ujambazi, ulevi, fitina, ubinafsi, uchawi, mawazo mabaya, tamaa mbaya, uchafu, ufisadi, ugomvi, wivu, hasira, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo.
Basi ukisha kuwa na imani katika Yesu Kristo anakupatia kiongozi yaani Roho Mtakatifu atakaye kuongoza katika upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi kwasababu upo ndani ya Kristo Yesu yaani tumeusulibisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake mbaya.