Wakulu, mimi nimebahatika kukutana na huyu kijana, Deo, mara kadhaa kule Ludewa. Ninamfahamu kiasi. Deo ni kijana mcheshi na mwepesi wa kusaidia wenzake, pale inapobidi. Tabia hii iliianza toka akiwa shule. Kwa kifupi yeye ni mtu wa watu, na hiki ndicho kinachofanya wana - Ludewa wamkubali.
Ndani ya Chama (CCM) huyu dogo mwenye umri wa miaka 38 anakubalika pia. Na amepewa nyadhifa za kadhaa; Deo Filikunjombe ni Katibu wa Uchumi na Fedha wa Wilaya, Ni Mlezi wa SKAUTI wa Wilaya ya Ludewa, Ni Kamanda (Mpya) wa Vijana wa Wilaya, Ni Mlezi wa Iringa Mjini - Manispaa ya Iringa, Ni Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Iringa, Ni Mjumbe wa wa Mkutano Mkuu wa Taifa, na ni Mlezi wa Chipukizi - CCM Taifa.
Nimemsikiliza kwa makini - kwenye mahojiano - akisema kuwa bado hajafanya uamuzi kama atagombea au la. Kwa maoni yangu, Deo akigombea atamwacha professor Mwalyosi kwa zaidi ya asilimia 90%.
Ndani ya Chama (CCM) huyu dogo mwenye umri wa miaka 38 anakubalika pia. Na amepewa nyadhifa za kadhaa; Deo Filikunjombe ni Katibu wa Uchumi na Fedha wa Wilaya, Ni Mlezi wa SKAUTI wa Wilaya ya Ludewa, Ni Kamanda (Mpya) wa Vijana wa Wilaya, Ni Mlezi wa Iringa Mjini - Manispaa ya Iringa, Ni Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Iringa, Ni Mjumbe wa wa Mkutano Mkuu wa Taifa, na ni Mlezi wa Chipukizi - CCM Taifa.
Nimemsikiliza kwa makini - kwenye mahojiano - akisema kuwa bado hajafanya uamuzi kama atagombea au la. Kwa maoni yangu, Deo akigombea atamwacha professor Mwalyosi kwa zaidi ya asilimia 90%.