Tunampenda Deo Filikunjombe Ludewa (CCM)

Niliangalia kwenye televisheni (bila shaka ITV) hivi karibuni akitawazwa kuwa kamanda wa vijana huko Ludewa na alitoa gari la wagonjwa. Alishangiliwa sana. Bila shaka anakubalika huyu kijana. Tuwaachie wapiga kura.
 
Go Filikunjombe go...utaupata tu. Tunataka watu kama nyie mwaka huu,wembe ni uleule Ushindi!!!
 
Hivi uchaguzi si chini ya miezi sita ijayo halafu mtu anaanza kampeni leo. Haule ulipashwa kuanza kampeni 5yrs ago. Where have you been eti leo ndio unatupatia gari la wagonjwa halafu na maandishi kabisa yenye jina lako. Huu ubunge mwaka huu kazi kweli kweli. Usituhonge tukupigie kura mimi siwapi kura yangu watu kama hawa. Kama ni ubunge wa mwaka huu umeliwa mnyalukolo vangu inongwa ngomi swee!!
 
Ingependeza sana huyu Filikunjombe kama angeenda kugombea jimbo la Njombe!
 
Hilo gari kalitoa yeye binafsi?Au CCM?
Maana isije ikawa ni serikali inatimiza wajibu wake kisha humohumo wanapandikiza na masuala ya ukamanda wa CCM.This is unfair advantage.Siasa za Tz bwana,kaaaaazi!!
 
Duh, jamaa anagombea ubunge?

Sina CV yake rasmi lakini alisoma Mass Communications (bachelor's degree) Makerere University Kampala na kumaliza mwaka 1999, baadae akajiunga na Wizara ya Mambo ya Ndani.

Jina kamili ni Deogratius Filikunjombe Haule. Labda kama wapo wawili

Deo Filikunjombe aligombea ubunge ndani ya CCM mwaka 2005, na alishindwa vibaya sana katika kura za maoni, Prof Mwalyosi akiibuka kidedea akifuatiwa na aliyekuwa mbunge Stanley Kolimba.

Mara baada ya uchaguzi, Deo alijikita sana katika kusaidia shughuli mbalimbali za maendeleo katika wilaya ya Ludewa na katika kusaidia kuwasomesha wanafunzi wanaotoka kwenye familia duni. na wakati huohuo mara kadhaa Prof Mwalyosi alikuwa akiwajibu vibaya wananchi pale alipokuwa akisomewa risala au kuombwa misaada na wananchi kwa kuwakumbusha kutokimbiliakimbila kwake kuomba misaada kwani mbunge siyo mfadhili, kimsingi Prof alikuwa sahihi lakini kwa mentality za wananchi wa kawaida ilitafsiriwa kama ni dharau na kutojali watu, hivyo kimbilio lao kubwa kwenye suala la misaada likabaki kwa kiasi kikubwa kuwa ni Deo, mtoaji msaada mzuri na anayewajali watu wa wilaya yake.

Ni muujiza tu ndio utaweza kuzuia ushindi wa Deo katika jimbo la Ludewa.
 
He he! Check out the avatar and decide for yourself. You?

Unajua nilikua nikiangalia hilo jengo lilikua linanikumbusha jengo fulani(administration),mbele kuna njia fulani niliokua nikipita wakati naenda East African school of Libriarianship. Kwahiyo ulikua unaishi wapi aisee? Club five ulikua unaenda? hivi mhandisi, kule kitivo cha technology ukipita geti dogo kwenda nje ndio kuna barabara ya Sir Apolo Kagwa?. Sijui ulioondoka lini aisee.
Namiss sana Club Obligato, Rock garden, Anje noir/anjemysteque,viper room(hotel equatoria) na samaki wa gaba beach.
 
Unajua nilikua nikiangalia hilo jengo lilikua linanikumbusha jengo fulani(administration),mbele kuna njia fulani niliokua nikipita wakati naenda East African school of Libriarianship. Kwahiyo ulikua unaishi wapi aisee? Club five ulikua unaenda? hivi mhandisi, kule kitivo cha technology ukipita geti dogo kwenda nje ndio kuna barabara ya Sir Apolo Kagwa?. Sijui ulioondoka lini aisee.
Namiss sana Club Obligato, Rock garden, Anje noir/anjemysteque,viper room(hotel equatoria) na samaki wa gaba beach.

Acheni hizo story zenu za Nsibirwa na Lumumba. Tupeni hoja za huyo jamaa wa Ludewa hapa.
 
Si yule aliekua askari polisi au? Kama ni hivi basi itapendeza mapolisi nao kutoa wagombea ubunge,mwe!!!. Tumezowea wahadhiri tu kila kukicha. Prof. Mwalyosi,Prof.Mungai,Prof. Msola, sasa waache wana Iringa wapate afande Deo(sijui tu kama anacheo gani sasa). Otherwise big up man!
 
Si yule aliekua askari polisi au? Kama ni hivi basi itapendeza mapolisi nao kutoa wagombea ubunge,mwe!!!. Tumezowea wahadhiri tu kila kukicha. Prof. Mwalyosi,Prof.Mungai,Prof. Msola, sasa waache wana Iringa wapate afande Deo(sijui tu kama anacheo gani sasa). Otherwise big up man!

Huyo Deo aliishaacha upolisi siku nyingi, siku hizi ana ofisi yake pale Benjamin Mkapa Towers ila sina uhakika inajishughulisha na nini. Ni mtu social sana na mwepesi wa kusaidia wenzake. Ubunge utamfaa sana yule kijana. Nimewahi kukutana naye mara mbili ingawa hakuwahi kunidokeza kwamba ana ambition ya ubunge. Binafsi namtakia kila la kheri katika mbio zake.
 
Unajua nilikua nikiangalia hilo jengo lilikua linanikumbusha jengo fulani(administration),mbele kuna njia fulani niliokua nikipita wakati naenda East African school of Libriarianship. Kwahiyo ulikua unaishi wapi aisee? Club five ulikua unaenda? hivi mhandisi, kule kitivo cha technology ukipita geti dogo kwenda nje ndio kuna barabara ya Sir Apolo Kagwa?. Sijui ulioondoka lini aisee.
Namiss sana Club Obligato, Rock garden, Anje noir/anjemysteque,viper room(hotel equatoria) na samaki wa gaba beach.

Ndio, hiyo ni Main Hall/ Ivory Tower. Mbele yake ni Freedom Square.
Nilikuwa mwana Gongom- Gongomes.
Hizo sehemu unazotaja nilivyokuwepo wala hazikuwa zimeanza isipokuwa Ange Noir, Silk, Viper room (I used to find that name rather vile) na hao samaki. Bila kusahau Kabalagala na Wandegeya.
 
Ndio nani huyo mkuu? tupe wasifu wake ili tumpigie kura hiyo siku itakapofika.

Namfahamu kidogo huyu ndugu kama ifuatavyo:-

Ni mseminari aliyesoma Kasita Seminary kule Morogoro na baadaye akahamia Forest Hill Sec. School mwaka 1993 na tukasoma darasa moja pale Forest (Form V na VI). Baadaye alienda Makerere Univ Uganda ambako alisomea Uandishi wa Habari na wakati huo huo akawa akiripoti na kutuma habari zake Redio One.

Baadaye alijiunga na World Vision Tanzania ambako alifanya kwa muda kidogo na baadaye akajiunga na Ikulu. Nilishittuka kusikia siku hizi ni Mfanyabiashara (aliacha kazi Ikulu) na ana fedha za kumtosha na alishaanza kampeni za kuwania Ubunge Jimbo la Ludewa kwa kutoa misaada mara kwa mara!

Zaidi ya hapo najua kuwa ni married na nlipokutana naye miaka 3 ilopita alikuwa na mtoto mmoja. SIjui kwa sasa.

My stand:

Mwacheni kijana ajaribu bahati yake ingawa mimi napata taabu sana mtu anapofanikiwa kidogo anawaza kutafuta Ubunge; sijui utamsaidia vipi kataka biashara zake au ndo itabidi aachane na biashara na afungamane na siasa kwa mujibu wa sheria.

Namshauri pia awe makini na siasa maana anaweza kujikuta Ubunge anakosa na anafilisika.
 
Namfahamu kidogo huyu ndugu kama ifuatavyo:-

Ni mseminari aliyesoma Kasita Seminary kule Morogoro na baadaye akahamia Forest Hill Sec. School mwaka 1993 na tukasoma darasa moja pale Forest (Form V na VI). Baadaye alienda Makerere Univ Uganda ambako alisomea Uandishi wa Habari na wakati huo huo akawa akiripoti na kutuma habari zake Redio One.

Baadaye alijiunga na World Vision Tanzania ambako alifanya kwa muda kidogo na baadaye akajiunga na Ikulu. Nilishittuka kusikia siku hizi ni Mfanyabiashara (aliacha kazi Ikulu) na ana fedha za kumtosha na alishaanza kampeni za kuwania Ubunge Jimbo la Ludewa kwa kutoa misaada mara kwa mara!

Zaidi ya hapo najua kuwa ni married na nlipokutana naye miaka 3 ilopita alikuwa na mtoto mmoja. SIjui kwa sasa.

My stand:

Mwacheni kijana ajaribu bahati yake ingawa mimi napata taabu sana mtu anapofanikiwa kidogo anawaza kutafuta Ubunge; sijui utamsaidia vipi kataka biashara zake au ndo itabidi aachane na biashara na afungamane na siasa kwa mujibu wa sheria.

Namshauri pia awe makini na siasa maana anaweza kujikuta Ubunge anakosa na anafilisika.

Mara polisi mara Ikulu. Inaonekana jamaa umesoma nae ila hujanyoosha hapo mkuu,labda umepitiwa kidogo. Inasemekana alikua polisi wewe unasema alikua Ikulu baada ya kuacha world vision.
 
Ndio, hiyo ni Main Hall/ Ivory Tower. Mbele yake ni Freedom Square.
Nilikuwa mwana Gongom- Gongomes.
Hizo sehemu unazotaja nilivyokuwepo wala hazikuwa zimeanza isipokuwa Ange Noir, Silk, Viper room (I used to find that name rather vile) na hao samaki. Bila kusahau Kabalagala na Wandegeya.

Kwenye bold hapo.
Injinia umenikumbusha mbali sana. Kuna geti dogo lingine lilikua unaibukia wandegeya. Tulikua tunakatiza sana hapo kwenda kuwaona vijana Akamwesi au tukiwa tunaenda mulago.
Deo kumbe ndio yule aliekua anareport toka Kampala(radio One) kipindi fulani?
 
Hongera sana Wakulu wa MUK, Mugamba Chi? Nawapa big up sana,mimi sikusoma pale ila nilikuwa navisiti sana miaka ya 2000. Kuhusu huyo kamanda aliyesimikwa, mimi nafikiri anastahili kupongezwa kwa hilo. Kuhusu kugombea au kutogombea ubunge ni yeye ndiye atakayeamua, ila ni haki yake Kikatiba kama Mtanzania, wapiga kura wa Ludewa itakuwa kazi kwao kuamua,tuwaachie. Asante sana kwa wakuu mlotupa data walau kidogo,tukizipata zaidi tutazimwaga hapa.

Nawakilisha
 
Kwa kweli sina shaka/tatizo na umri wake kuitwa kamanda wa vijana. Nahisi (nionavyo mimi) ukamanda wa vijana kwenye hiki chama hauna cut-off ya umri. Kwasababu hata Mr paul Kimiti mbunge wa Sumbawanga mjini bado ni kamanda wa vijana wilyaya ya Sumbawanga mjini (Sina hakika kama amestaafu mwaka huu). Wengi wetu tutakumbuka kijana mwenzetu Kingunge Ngombale Mwiru, alivyotumikia nafasi ya ukamanda wa vijana mpaka miaka ya hivi karibuni. Umri sio issue kabisa kule chamani!!!

Basi wabadilishe jina.Haileti maana kabisa.kamanda wa Vijana huku Mzee.kwani vijana wenyewe hawawezi kuwa makamanda mpaka wapewe hawa kina Kimiti?
 
Back
Top Bottom