Tunajifunza nini kutokana na uchaguzi Mkuu wa Afrika Kusini uliomalimizika hivi majuzi?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,484
30,160
Uchaguzi Mkuu umefanyika nchini Afrika Kusini wiki iliyopita, ambapo Tume ya Taifa ya Uchaguzi wa nchi hiyo Indapendent Electoral Commission, kilikitangaza Chama cha ANC cha aliyekuwa mzalendo namba moja wa nchi hiyo, Mzee Nelson Mandela, kuwa mshindi kwa kupata asilimia 57.5 kikifuatiwa na chama cha Democratic Alliance (DA) ambacho kimepata asimilia 20.7 na cha kilichofuatia ni chama cha cha mlengo wa kushoto cha Malema, cha Economic Freedom Fighters (EFF) kilichopata aslimimia 10.8

Vyama vingine vidogo vidogo vikajikusanyia asimia iliyobakia

Tunajifunza nini kutokana na uchaguzi uliomalimizika na kutangazwa huko Afrika Kusini??

Kitu kimoja tunachojifunza kutokana na uchaguzi huo ambao ulisimamiwa na Tume huru ya uchaguzi ( Independent Electoral Commission) ni kuwa uchaguzi huo ulikuwa huru na wa haki na Jeshi la Polisi la nchi hiyo lilikuwa na jukumu dogo kabisa la kusimamia usalama na wala siyo kuingilia upigaji kura na ndicho tulichokiona cha wapiga kura kupiga kura zao na matokeo yao kutangazwa kama yalivyo na wala hayakuchakachuliwa

Kwa hiyo kama nchi yetu itapenda kuendelea kudumisha amani ya nchi hii ambayo imekuwa nayo tokea nchi yetu ipate Uhuru wake ni lazima iheshimu sanduku la kura na wala siyo "kutusimikia" viongozi wao wanaowataka wao ambao hawakuchaguliwa na wananchi

Ni vyema tukaiga mfano wa Independent Electoral Commission ya Afrika Kusini katika uandaaji wa chaguzi zetu

Mungu ibariki Tanzania
 
Hatuwezi kuendelea na wasimamizi wa uchaguzi ambao mtu anayewateua amesikika akisema "Ninakupa mshahara mnono na marupurupu, nyumba nzuri ya kuishi na gari ya kutembelea, halafu nisikie unamtangaza mpinzani kashinda" Mwisho wa kunukuu
 
Hapa kwetu inaitwa Tume Huru ya Uchaguzi ila haiakisi uhuru wowote.
Inakuwaje huru wakati mwenyekiti wake anateuliwa na Rais,Rais ambaye ni mwanachama wa chana cha siasa...je aweza kumteua mtu ambaye hawaongei lugha ya chama chao?,..ni ngumu!
 
Uchaguzi Mkuu umefanyika nchini Afrika Kusini wiki iliyopita, ambapo Tume ya Taifa ya Uchaguzi wa nchi hiyo Indapendent Electoral Commission, kilikitangaza Chama cha ANC cha aliyekuwa mzalendo namba moja wa nchi hiyo, Mzee Nelson Mandela, kuwa mshindi kwa kupata asilimia 57.5 kikifuatiwa na chama cha Democratic Alliance, ambacho kimepata asimilia 20.7 na cha kilichofuatia ni chama cha cha mlengo wa kushoto cha Malema, cha Economic Freedom Fighters kilichopata aslimimia 10.8

Vyama vingine vidogo vidogo vikajikusanyia asimia iliyobakia

Tunajifunza nini kutokana na uchaguzi uliomalimizika na kutangazwa huko Afrika Kusini??

Kitu kimoja tunachojifunza kutokana na uchaguzi huo ambao ulisimamiwa na Tume huru ya uchaguzi ( Independent Electoral Commission) ni kuwa uchaguzi huo ulikuwa huru na wa haki na Jeshi la Polisi la nchi hiyo lilikuwa na jukumu dogo kabisa la kusimamia usalama na wala siyo kuingilia upigaji kura na ndicho tulichokiona cha wapiga kura kupiga kura zao na matokeo yao kutangazwa kama yalivyo na wala hayakuchakachuliwa

Kwa hiyo kama nchi yetu itapenda kuendelea kudumisha amani ya nchi hii ambayo imekuwa nayo tokea nchi yetu ipate Uhuru wake ni lazima iheshimu sanduku la kura na wala siyo "kutusimikia" viongozi wao wanaowataka wao ambao hawakuchaguliwa na wananchi

Ni vyema tukaiga mfano wa Independent Electoral Commission ya Afrika Kusini katika uandaaji wa chaguzi zetu

Mungu ibariki Tanzania
hawa waroho wa madaraka wanajua kuiga vitu vya hovyo kutoka rwanda tu,hawawezi kuiga kua na tume huru sababu wataondoshwa madarakani mchana kweupe
 
Huko kwenyewe S/Africa Kikwete alikua mmoja wa waangalizi wa Uchaguzi.,mnategemea nini?
 
nimejifunza kitu kimoja kikubwa sana, ni kuwa watu wanaviamini sana vyama vya ukombozi kuliko vyama mawakala wa ubepari
 
Huko kwenyewe S/Africa Kikwete alikua mmoja wa waangalizi wa Uchaguzi.,mnategemea nini?
Alikuwa mwangalizi mkuu wa uchaguzi huo kutoka nchi za SADCC

Hata hivyo nina uhakika moyo umemsuta, akilinganisha na uandalizi wa Tume hiyo ya uchaguzi ukilinganisha na yetu, ambayo huwa wamelipa jukumu Jeshi letu la Polisi, lisimamie kikamililifu na hatimaye "limtangaze" mshindi wa uchaguzi huo atakayetakiwa na chama tawala!
 
Hawanaga aibu hao mkuu wala hawajifunzi.

Kiila siku wanaenda kuzurura huko duniani lkn mambo mazuri ya huko wala hawaya-implement wakirudi makwao.
Alikuwa mwangalizi mkuu wa uchaguzi huo kutoka nchi za SADCC

Hata hivyo nina uhakika moyo umemsuta, akilinganisha na uandalizi wa Tume hiyo ya uchaguzi ukilinganisha na yetu, ambayo huwa wamelipa jukumu Jeshi letu la Polisi, lisimamie kikamililifu na hatimaye "limtangaze" mshindi wa uchaguzi huo atakayetakiwa na chama tawala!
 
Hatuwezi kuendelea na wasimamizi wa uchaguzi ambao mtu anayewateua amesikika akisema "Ninakupa mshahara mnono na marupurupu, nyumba nzuri ya kuishi na gari ya kutembelea, halafu nisikie unamtangaza mpinzani kashinda" Mwisho wa kunukuu
Haya maneno alikuwa anatamka utafikiri yupo na mke wake chumbani sasa watoa misaada wamkaushe makal+o
 
Sio sahihi, JK alikua kiongozi mkuu toka AU.

Pia, alikuwa ni mgeni rasmi wa Rais Ramaphosa siku ya utangazaji wa matokeo.

President Ramaphosa na IEC kwa pamoja ktk nyakati tofauti walimshukuru sana JK kwa kuhalalisha matokeo pale aliposema sio tu ni huru na haki bali pia ni CREDIBLE.

Ikumbukwe kua vyama vidogo 27 vinapinga matokeo na vilifungua shauri kutaka IEC irudie uchaguzi Kwa kua ulikuwa si Free and Fair.

Sasa hapo ndio utambue uzito wa kauli ya JK kwenye Urais wa Ramaphosa.

Pia msisahau kuwa ni huyo huyo mzee wa Msoga ndie alyeenda kusimamia na kuhalalisha matokeo ya uchaguzi wa Nigeria hivi majuzi.
Alikuwa mwangalizi mkuu wa uchaguzi huo kutoka nchi za SADCC

Hata hivyo nina uhakika moyo umemsuta, akilinganisha na uandalizi wa Tume hiyo ya uchaguzi ukilinganisha na yetu, ambayo huwa wamelipa jukumu Jeshi letu la Polisi, lisimamie kikamililifu na hatimaye "limtangaze" mshindi wa uchaguzi huo atakayetakiwa na chama tawala!
 
Kwa uwepo wa JK pale wala hakuna kitu nimejifunza kwenye huo uchaguzi.
Sio sahihi, JK alikua kiongozi mkuu toka AU.

Pia, alikuwa ni mgeni rasmi wa Rais Ramaphosa siku ya utangazaji wa matokeo.

President Ramaphosa na IEC kwa pamoja ktk nyakati tofauti walimshukuru sana JK kwa kuhalalisha matokeo pale aliposema sio tu ni huru na haki bali pia ni CREDIBLE.

Ikumbukwe kua vyama vidogo 27 vinapinga matokeo na vilifungua shauri kutaka IEC irudie uchaguzi Kwa kua ulikuwa si Free and Fair.

Sasa hapo ndio utambue uzito wa kauli ya JK kwenye Urais wa Ramaphosa.

Pia msisahau kuwa ni huyo huyo mzee wa Msoga ndie alyeenda kusimamia na kuhalalisha matokeo ya uchaguzi wa Nigeria hivi majuzi.
 
Back
Top Bottom