Tunajifunza nini kuhusu kufukuzwa kazi kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi na Waziri wa usalama wa Uganda?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,484
30,159
Hivi Leo zimetolewa taarifa za kufutwa kazi Mkuu wa Jeshi la Polisi wa Uganda, Jenerali Kayihura na Waziri wa Usalama Henry Tumukunde, ambako kumefanywa na Rais Museveni.

Sababu za kufutwa kwao kazi ni kukithiri kwa matukio ya mauaji ya raia wasio na hatia, kutekwa na kuteswa kwa watu.

Sababu zilizotolewa huko Uganda kwa kufutwa kazi kwa watu hao wawili ndiyo kilio cha muda mrefu hapa nchini kuwa IGP Simon Sirro na Waziri wake wa ndani Mwiguru Nchemba, wajiuzulu nafasi zao au Rais atengue nafasi hizo kutokana na matukio ya watu "wasiojulikana" kuua watu hapa nchini bila watu hao kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Rais wa Uganda ameamua kuwafuta kazi watu hao ambao walikuwa wanaharibu sifa ya utendaji kazi wa Jeshi hilo nchini Uganda.

Ni wakati muafaka kwa sasa Rais wetu naye afuate nyayo za Rais mwenzake wa nchi jirani kwa kuwafuta kazi IGP Simon Sirro na Waziri wa mambo ya ndani, Mwigulu Nchemba
 
Hamia Uganda kwa sababu kuna Rais anayefanyia kazi vilio vyako!

Ujinga ni kudhani kuwa unaweza ku copy na ku paste tukio fulani wakati mazingira ni tofauti.

Rais Museveni amewaondoa kwa sababu walikuwa wanarumbana kikazi kutokana na uhasama wao binafsi wa muda mrefu. Kwa hiyo usifikirie eti wameondolewa kwa sababu wananchi walitaka waondolewe.
 
Hamia Uganda kwa sababu kuna Rais anayefanyia kazi vilio vyako!

Ujinga ni kudhani kuwa unaweza ku copy na ku paste tukio fulani wakati mazingira ni tofauti.
Siyo kucopy na kupaste.....

Bali mazingira ya hao waliofukuzwa kazi Uganda yanafanana sana na hapa kwetu, ambapo wakuu wetu hao wawili, yaani IGP Simon Sirro na Waziri wanalazimika wajiuzulu kutokana na utendaji kazi mbovu wa idara wanazoziongoza
 
Hapa kwetu watu kama hao wanafanya kazi iliyotukuta kwa aliowateua,

Nakukumbusha tu kwamba formu tulichukua sisi,tukagombea sisi hivyo huwa hatupangiwa.

Na kingine cha mwisho hatujaribiwi na usituchezee kabisa sisi ni wa tofauuti

Hatujalelewa hivyo..........
Subirini waje wengine ndo muwachezee.......
 
Natamani kusepa chato,
ugeni kukaribishwa kwato,
kule wazuri wapo watoto,
Range nayo kwa mtoko,
Lami straight hakuna kokoto...



Freestyle rap...
 
Musemen ni mwanajeshi aliyeingia msituni kupambana wakati
magufuli ni raia sana sana atakuwa kapitia JKT so wana tofaut nyingi sana katika utendaji na shughuli nzma za kuongoza watu.
 
Mmm watu walikuwa wakipotezwa miaka na miaka uganda. Huku na sisi tuvumilie tu miaka na miaka mpaka huyu wetu atakapoanza kusoma alama za nyakati
 
Hivi Leo zimetolewa taarifa za kufutwa kazi Mkuu wa Jeshi la Polisi wa Uganda, Jenerali Kayihura na Waziri wa Usalama Henry Tumukunde, ambako kumefanywa na Rais Museveni.

Sababu za kufutwa kwao kazi ni kukithiri kwa matukio ya mauaji ya raia wasio na hatia, kutekwa na kuteswa kwa watu.

Sababu zilizotolewa huko Uganda kwa kufutwa kazi kwa watu hao wawili ndiyo kilio cha muda mrefu hapa nchini kuwa IGP Simon Sirro na Waziri wake wa ndani Mwiguru Nchemba, wajiuzulu nafasi zao au Rais atengue nafasi hizo kutokana na matukio ya watu "wasiojulikana" kuua watu hapa nchini bila watu hao kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Rais wa Uganda ameamua kuwafuta kazi watu hao ambao walikuwa wanaharibu sifa ya utendaji kazi wa Jeshi hilo nchini Uganda.

Ni wakati muafaka kwa sasa Rais wetu naye afuate nyayo za Rais mwenzake wa nchi jirani kwa kuwafuta kazi IGP Simon Sirro na Waziri wa mambo ya ndani, Mwigulu Nchemba
Kwa hiyo JPM awe anafuata yanayotekelezwa na Rais wa Uganda, Kenya, Rwanda, e.t.c kama kwamba ni maagizo, atakuwa Rais wa Tanzania au mtumishi wa ma rais wa nchi hizo?
 
Back
Top Bottom