Huu ni mwanzo.....kama marekani waliwahi kupigana wao kwa wao lengo likiwa ni kurudisha umoja na utii wa sheria.....basi nasi tusikate tamaa. Hawa akina chenge, makamba, lowasa, chiligati na wenzao muda si mrefu they will be dying.
Nadhani uchaguzi wa chadema ulikwisha salama na kambi zote mbili zilivunjwa siku hiyo kwa ajili ya kuleta mshikamano kwenye chama. Nadhani tusikae tuna quote mambo ya nyuma kila chama kina matatizo yake.
Hii topic ni nzuri.
mjj amelenga pazuri.
kuunda chama kipya itatuchukua muda mrefu kutarua matatizo ya nchii hii. tuwasaidie hawa viongozi wa vyama vilivyopo katika uteuzi mzuri wa kiongozi wa kitaifa (Rais) ambaye ana sifa zote ambazo sisi wananchi tunazi afiki. na ana maadili mema ya kiungozi na hasa mkali kwa tukio lolote linalokwenda kinyume na matakwa ya wananchi (adhabu iwepo pale pale kwa mtuhumu huyu). naamini candidates hao wapo. support ni muhimu sana baada ya kupatikana mtu huyu. natuanze kumfikiri sasa. Mimi nitaanza na dr slaa sisna mrengo wowote wa kichama. kama kuna mtu wa kunikosoa na anikosoe sasa.
Kabla ya kuanzisha chama kipya, kama kinataka kuwa cha maana, inabidi waanzilishi wajiulize maswali yafuatayo.
1. Kuna haja ya chama kipya?
2. Vyama vilivyopo haviwezi kukidhi mahitaji?
3. Kuna tofauti gani ya kimsingi kati ya vyama vilivyopo na hiki kipya?
4. Ni kwa vipi chama hiki kipya kitajizuia kurudia makosa ya vyama vilivyopo?
5. Chama hiki kipya kitachangia nini kipya?
Tatizo sio wananchi. tatizo ni vyama havijapata viongozi sahihi....mwaka 1995, upinzani chini ya mrema ulifanikiwa kushinda asilimia43 ya kura za urais, asilimia 40 za kura za ubunge...kumbukeni hii ilikuwa miaka3 tu tangu mfumo wa vyama vingi urejeshwe...na labda kwa taarifa tu ni kwamba jijiji la Dar es Salaam, upinzani ulishinda majimbo yote saba, serikali ikafuta uchaguzi....viongozi wa upinzani wasiendekeze lawama kuwa wananchi hawataki mabadiliko..NO. wananchi wako tayari, tatizo ni viongozi wa upinzani bado wanasua mno...hatujapata mtu wa kuvaa viatu vya mrema wa 1995...tukimpata, wananchi sio tatizo mwanakijiji....
Mkulu Bluray, with all due respect:-
- Tunahitaji chama kipya ambacho condition ya kujiunga itakuwa ni pamoja na kutowahi kushiriki kwenye siasa za taifa in the past, Rawlings aliwakusanya wanasiasa wote muhimu wa zamani na kuwatwanga risasi kule beach, leo Ghana ni numero uno na uongozi bora,
- Sisi hatuwapigi risasi ila hatuwataki kujiunga nasi, lengo la kwanza liwe ni kuwaamusha wananchi wa Tanzania, ambao sio siri wapo usingizini sana na kinachoendelea na taifa lao.
- Ni lazima wananchi waamushwe kwanza, the rest baadaye! Na yes tunahitaji chama kipya chenye wanachama wenye mawazo mapya na solutions kwa matatizo ya taifa letu.
Respect.
FMEs!
Usitegemee toka kwa NDIVYO TULIVYO.... Ukiweza kuelewa Wadanganyika na jinsi wanavyofikiria mkuu wangu chukua glass ya maji kunywa upoze koo. Ni swala ambalo haliwezekani na ndio maana tumekuwa hapa.
Mkulu Mwanakijiji, heshima mbele sana;-
- Haya nimeyasema sana hapa JF, kwamba dawa ni kuanza upya na ninashukuru kwamba finally umeliona hili kama lilivyo, kwamba tunahitaji kuanza upya. Kwa maoni yangu ni kwamba vyama vyote vya siasa nchini in one way or another vina spirit ya CCM ndani yake, hatuwezi kwenda popote wala kupata mabadiliko yanayotakiwa, na hivi vyama.
- Ni miaka karibu 15 sasa toka tuingie kwenye siasa za vyama vingi, matokeo hayaridhishi ukilinganisha na nchi zingine majirani ambao tulianza pamoja mabadiliko, CUF na Chadema, sio siri wamejitahidi sana lakini it is too little na ni too low to show for, huku the time is running out.
Wakati ni huu wa kuanza upya! I mean tunahitaji chama kipya very badly regardless ya its immediate effect kwa taifa, lakini ni lazima tuwaamshe wananchi kwa kuwaanika wazi hawa wanafiki kwamba wote wanafanana, kazi kupeana per-day za kusafiri nje na kamati uchwara za bunge huku wakidai serikali haina pesa, nonsense!
Respect.
Field Marshall Es!
Chama hicho kitakusanya ndani yake baadhi ya vipaji vya hali ya juu ktk siasa zetu. It is just a matter of time.