Tutor B
JF-Expert Member
- Jun 11, 2011
- 9,025
- 6,619
Niende moja kwa moja kwenye kile nilichokilenga,
Shuleni kuanzia elimu ya msingi hadi vyuo tunakatazwa kabisa kutazamia. Mwanafunzi anayetazamia huwa anapewa adhabu. Huu ndo ukweli kwa elimu ya Tanzania.
Katika maisha ya kawaida, msingi wetu ni kutazamia. Anzia kwako mwenyewe, mambo mengi unayofanya ni kwa kutazamia kwa wengine, uvaaji, ulaji, imani n.k. Njoo kwenye familia yako – mwangalie jirani yako hapo mtaani, hadi kwa kiongozi wako wa jimbo (naishia hapa jimboni kwa sababu mwingine juu ya jimbo hairuhusiwi kumwongelea). Yote yanayotendeka ni kwa kutazamia tu. Ni wachache sana wanaofanya mambo kwa kutumia misingi ya akili zao.
Ushauri: Taasisi zinazohusika na elimu hapa nchini jaribuni kuliangalia hili. Kutazamia sio dhambi hadi kufikia hatua ya kumfutia mwanafunzi matokeo yake ya mwisho.
Una mtazamo upi katika hili?
Shuleni kuanzia elimu ya msingi hadi vyuo tunakatazwa kabisa kutazamia. Mwanafunzi anayetazamia huwa anapewa adhabu. Huu ndo ukweli kwa elimu ya Tanzania.
Katika maisha ya kawaida, msingi wetu ni kutazamia. Anzia kwako mwenyewe, mambo mengi unayofanya ni kwa kutazamia kwa wengine, uvaaji, ulaji, imani n.k. Njoo kwenye familia yako – mwangalie jirani yako hapo mtaani, hadi kwa kiongozi wako wa jimbo (naishia hapa jimboni kwa sababu mwingine juu ya jimbo hairuhusiwi kumwongelea). Yote yanayotendeka ni kwa kutazamia tu. Ni wachache sana wanaofanya mambo kwa kutumia misingi ya akili zao.
Ushauri: Taasisi zinazohusika na elimu hapa nchini jaribuni kuliangalia hili. Kutazamia sio dhambi hadi kufikia hatua ya kumfutia mwanafunzi matokeo yake ya mwisho.
Una mtazamo upi katika hili?