Tunaanza kutengeneza kizazi cha watoto au watanzania wasiojua vizuri kiswahili kama ilivyo kwa wahindi licha ya kuzaliwa na kukulia humu nchini

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,014
144,371
Kila kitu kina faida na hasara zake.Moja ya faida ya hizi shule za kisasa ni watoto kujua lugha ya malaika angali wakiwa na umri mdogo na kuwa fluent tofauti na wale wanaosoma shule za St. Kayumba.

Hata hivyo, kuna kasoro naiona na ambayo baada ya muda, tutakuja kuiona huko mbele na hii si nyingine bali ni kuwa na kizazi cha watanzania wasioweza kujieleza vizuri kwa kiswahili bali kingereza huku lugha zetu za asili zikiendelea Kopotea kabisa.

Kwanini nasema hivi?

Mazingira wanayokulia watoto wetu wa leo ni tofauti sana na yale tuliokuia sisi.Siku hizi humu mijini kila mtu akijenga nyumba yake anajitahidi kuweka uzi wa ukuta na geti na matokeo yake watoto wetu hawachezi tena pamoja mitaani kama enzi zetu ambapo tukitoka shule, tunakutana mtaani tunacheza pamoja then kigiza kikianza kuingia tunarejea majumbani.

Nini kinatokea?

Watoto wetu hawa wa leo wakiwa katika hizi shule za kisiasa, ni kuongea kingereza mwanzo mwisho tangu wanapoanza shule tena siku hizi wakiwa na umri mdogo (wanamaliza darasa la saba wakiwa na miaka 12 mpaka 13) na wakirudi majumbani ni kufungiwa kwenye mageti mpaka kesho yake tena watapoenda shale.


Athari inajitokezaje?

Watoto hawa tangu wakiwa wadogo,wana-spend muda mwingi shuleni wakiongea kingerez na wakirudi nyumbani wanafungiwa kwenye magoti na hawapata nafasi ya kuchanganyikiwa na wenzao wa St.Kayumba walioko mtaani, hivyo hawakutani na watoto wenzao wanaozungumza kiswahili na matokeo yake wanakuwa wakijua kuongea zaidi kingereza kuliko kiswahili.

Mazingira haya wanaokulia na kulelewa yanafanana na mazingira wanayozaliwa na kukulia wahindi ambao licha ya kuzaliwa na kukulia humu nchini, wanakuwa hawawezi kuzungumza kiswahili fasaha kwani muda mwingi wanatumia lugha yao na kingereza wanachofundishwa.

Na katika hili, bora hata wahindi kwani mbali na watoto wao kufundishwa lugha ya kingereza, bado wanatumia zaidi kihindi katika mawasiliano yao huku sisi hata wazazi wakiendeleza matumizi ya lugha ya kingereza kwa watoto wao wawapo majumbani na kuona huku ndio kustaarabika.

Kujua kingereza ni muhimu kwasababu hiyo ni lugha ya kimataifa ambayo watoto wetu wataitumia kuombea ajira na kushindana na wenzao kimataifa na pia wataitumia kwa mambo mengine but not to this extent ya kuanza kusahau kabisa lugha yetu ya Taifa.

Tuchukue hatua na mojawapo iwe kuongea na kuandika lugha ya kiswahil kwa ufasaha kama ni added advantage kwenye usaili wa ajira za serikali huko mbeleni iwapo hali hii itafikia hatua mbaya.

Mnaweza msinielewa sasa hivi, ila miaka 15 mpaka 20 ijayo, hali hii itakuwa wazi kabisa, na mpaka sasa teyari kuna watoto ambao wako fluent zaidi katika kuongea kingereza kuliko kiswahili.

Usisahau hata mchicha ulianza kama mbuyu.

Tutakuja tena kulaumu wazungu kwa kuua lugha yetu kama ambavyo leo hii tunawalaumu kwa kuua utamaduni wetu.

Alietuloga alikuwa fundi!!
 
Ni uoga wako tu ! Hakuna logic yoyote kwenye wasilisho lako! Watoto wako pale Tandale kwa Mfuga Mbwa, Kwa Bibi Nyau au Mbagala na wanasoma St.Kayumba lakini hawajui Kiswahili fasaha! Mirathi wanasema "Mirasi" , Bidhaa wanaita " Bizaa" ,Habari wanasema "_Habali" , Rais wanamwita "_Laisi" ! Je tatizo ni English medium schools!
Tafuteni maarifa kwa namna ya juu zaidi na acheni visingizio dhaifu!
 
Tatizo hata wanaosoma shule za kata hawajui Kiswahili.

Hapo ndipo hoja yako inapopata changamoto.
Ni kweli hawajui vizuri kiswahili ila wanajua zaidi lugha zao za asili kwasababu ndizo zinatumika zaidi wawapo nyumbani.

Hata Mzee Baba kiswahili Kwake ni changamoto na bila shaka alikulia katika familia iliyokuwa inatumia kilugha muda mwingi kuwasiliana kuliko kiswahil na watu wa aina hii wapo wengi tu.
 
Ni uoga wako tu ! Hakuna logic yoyote kwenye wasilisho lako! Watoto wako pale Tandale kwa Mfuga Mbwa, Kwa Bibi Nyau au Mbagala na wanasoma St.Kayumba lakini hawajui Kiswahili fasaha! Mirathi wanasema "Mirasi" , Bidhaa wanaita " Bizaa" ,Habari wanasema "_Habali" , Rais wanamwita "_Laisi" ! Je tatizo ni English medium schools!
Tafuteni maarifa kwa namna ya juu zaidi na acheni visingizio dhaifu!
Hivyo wewe unajua Tanzania ni Dar es Salaam pekee? Comment yako inadhihirisha namna exposure yako ilivyo finyu..

Hata kwa hao wazungu wanazo hizo lahaja.

Maarifa sahihi huja kwa lugha sahihi. Napendekeza tufumue mtaala wetu uwe ni kiswahili mwanzo 'mwenga'
 
Unaeleweka sana lakini je kuna umhimu gani wa kukumbatia lugha ambayo mwisho wa siku haikusaidii zaidi ya kubaki nayo kama utambulisho tu? Serikali yenyewe ndo imetufikisha hapa, nitajie ni taasisi gani ya serikali ukienda kuomba kazi usaili utafanya kwa kimakonde, kisukuma, kijita, kijaluo, kimakua, kichaga, kinyamwezi, kizanaki, kinyakyusa, kiswahili nk,
Kwa hali hii kwa nini mtoto ang'ang'anie kiswahili ambacho mwisho wake ni Kariakoo, ambako nako ukishataka kuagiza kitu Ali baba, Aliexpress, Amazon unatafuta anayejua kiingereza. Kiswahili tumeshachelewa acha kijifie kifo cha kawaida. Bungeni miswada yote kiingereza, mahakamani kiingereza, shule kiingereza, kiswahili cha nini sasa.
 
Ni uoga wako tu ! Hakuna logic yoyote kwenye wasilisho lako! Watoto wako pale Tandale kwa Mfuga Mbwa, Kwa Bibi Nyau au Mbagala na wanasoma St.Kayumba lakini hawajui Kiswahili fasaha! Mirathi wanasema "Mirasi" , Bidhaa wanaita " Bizaa" ,Habari wanasema "_Habali" , Rais wanamwita "_Laisi" ! Je tatizo ni English medium schools!
Tafuteni maarifa kwa namna ya juu zaidi na acheni visingizio dhaifu!
Tofautisha kutamka vibaya maneno na kushindwa kutengeza sentesi kwa lugha fulani.
 
Unaeleweka sana lakini je kuna umhimu gani wa kukumbatia lugha ambayo mwisho wa siku haikusaidii zaidi ya kubaki nayo kama utambulisho tu? Serikali yenyewe ndo imetufikisha hapa, nitajie ni taasisi gani ya serikali ukienda kuomba kazi usaili utafanya kwa kimakonde, kisukuma, kijita, kijaluo, kimakua, kichaga, kinyamwezi, kizanaki, kinyakyusa, kiswahili nk,
Kwa hali hii kwa nini mtoto ang'ang'anie kiswahili ambacho mwisho wake ni Kariakoo, ambako nako ukishataka kuagiza kitu Ali baba, Aliexpress, Amazon unatafuta anayejua kiingereza. Kiswahili tumeshachelewa acha kijifie kifo cha kawaida. Bungeni miswada yote kiingereza, mahakamani kiingereza, shule kiingereza, kiswahili cha nini sasa.
Alafu tutakuja kulaumu wazungu kuwa wameua lugha yetu kama ambavyo leo hii tunawalaumu kwa kuua utamaduni wetu.
 
Ni kweli hawajui vizuri kiswahili ila wanajua zaidi lugha zao za asili kwasababu ndizo zinatumika zaidi wawapo nyumbani.

Hata Mzee Baba kiswahili Kwake ni changamoto na bila shaka alikulia katika familia iliyokuwa inatumia kilugha muda mwingi kuwasiliana kuliko kiswahil na watu wa aina hii wapo wengi tu.
Hata wa shule za kata Dar wasiojua lugha zao za asili, nao hawajui Kiswahili.
 
Nimeona kwenye bandiko lako umetumia neno " not to that extent " kama Rais Magufuli, safi sana mkuu umeamua kuachana na Sacco's.

Sent from my Infinix X622 using JamiiForums mobile app
 
Hivyo wewe unajua Tanzania ni Dar es Salaam pekee? Comment yako inadhihirisha namna exposure yako ilivyo finyu..

Hata kwa hao wazungu wanazo hizo lahaja.

Maarifa sahihi huja kwa lugha sahihi. Napendekeza tufumue mtaala wetu uwe ni kiswahili mwanzo 'mwenga'
😀😀
 
Jambo Bora ni kuelewana, tena kuelewana kwa mapana yafikayo Canada, Australia, england mpaka Zimbabwe na Malawi na kule South Africa. Hilo ni Jambo jema, acha wakue.
 
Alafu tutakuja kulaumu wazungu kuwa wameua lugha yetu kama ambavyo leo hii tunawalaumu kwa kuua utamaduni wetu.
Wewe mwenyewe hujui Kiswahili sahihi.

Unaandika "Alafu" badala ya "Halafu".

Labda ujiongeze kwanza kabla ya kulaumu wengine.
 
Faida za kiswahili ni nini
Ni kama tu kimakonde, kichaga kizaramo ni kama lugha tu kwaajili ya mawasiliano na hakiwezi kupotea kwa namna yoyote ile

Kujifunza lugha nyingine ni kupanua maarifa kujua kingereza ni kuwa wa kimataifa zaidi kwa hiyo ni faida kwa sasa sisi ni local hatuwezi kuchangamana na dunia ipasavyo kwasababu ya lugha tu

South Africa kuna lugha 12 na Kuna foreigners wengi kuliko nchi yoyote Africa zinaongelewa lugha nyingi sana za kigeni watoto mashuleni wanafundisha kiingereza fasaha kwa kuwa hata mtaani wanaongea ila siyo kizuri sana
Lakini pamoja na hayo bado kizulu ni lugha mama haiwezi kupotea

Nawaonea wivu Hawa jamaa wasouth ni ma linguistics
Msouth yoyote ukimgusa analugha kuanzia nne anazozijua na kuendelea
 
Kila kitu kina faida na hasara zake.Moja ya faida ya hizi shule za kisiasa ni watoto kujua lugha ya malaika angali wakiwa na umri mdogo na kuwa fluent tofauti na wale wanaosoma shule za St. Kayumba.

Hata hivyo, kuna kasoro naiona na ambayo baada ya muda, tutakuja kuiona huko mbele na hii si nyingine bali ni kuwa na kizazi cha watanzania wasioweza kujieleza vizuri kwa kiswahili bali kingereza huku lugha zetu za asili zikiendelea Kopotea kabisa.

Kwanini nasema hivi?

Mazingira wanayokulia watoto wetu wa leo ni tofauti sana na yale tuliokuia sisi.Siku hizi humu mijini kila mtu akijenga nyumba yake anajitahidi kuweka uzi wa ukuta na geti na matokeo yake watoto wetu hawachezi tena pamoja mitaani kama enzi zetu ambapo tukitoka shule, tunakutana mtaani tunacheza pamoja then kigiza kikianza kuingia tunarejea majumbani.

Nini kinatokea?

Watoto wetu hawa wa leo wakiwa katika hizi shule za kisiasa, ni kuongea kingereza mwanzo mwisho tangu wanapoanza shule tena siku hizi wakiwa na umri mdogo (wanamaliza darasa la saba wakiwa na miaka 12 mpaka 13) na wakirudi majumbani ni kufungiwa kwenye mageti mpaka kesho yake tena watapoenda shale.


Athari inajitokezaje?

Watoto hawa tangu wakiwa wadogo,wana-spend muda mwingi shuleni wakiongea kingerez na wakirudi nyumbani wanafungiwa kwenye magoti na hawapata nafasi ya kuchanganyikiwa na wenzao wa St.Kayumba walioko mtaani, hivyo hawakutani na watoto wenzao wanaozungumza kiswahili na matokeo yake wanakuwa wakijua kuongea zaidi kingereza kuliko kiswahili.

Mazingira haya wanaokulia na kulelewa yanafanana na mazingira wanayozaliwa na kukulia wahindi ambao licha ya kuzaliwa na kukulia humu nchini, wanakuwa hawawezi kuzungumza kiswahili fasaha kwani muda mwingi wanatumia lugha yao na kingereza wanachofundishwa.

Na katika hili, bora hata wahindi kwani mbali na watoto wao kufundishwa lugha ya kingereza, bado wanatumia zaidi kihindi katika mawasiliano yao huku sisi hata wazazi wakiendeleza matumizi ya lugha ya kingereza kwa watoto wao wawapo majumbani na kuona huku ndio kustaarabika.

Kujua kingereza ni muhimu kwasababu hiyo ni lugha ya kimataifa ambayo watoto wetu wataitumia kuombea ajira na kushindana na wenzao kimataifa na pia wataitumia kwa mambo mengine but not to this extent ya kuanza kusahau kabisa lugha yetu ya Taifa.

Tuchukue hatua na mojawapo iwe kuongea na kuandika lugha ya kiswahil kwa ufasaha kama ni added advantage kwenye usaili wa ajira za serikali huko mbeleni iwapo hali hii itafikia hatua mbaya.

Mnaweza msinielewa sasa hivi, ila miaka 15 mpaka 20 ijayo, hali hii itakuwa wazi kabisa, na mpaka sasa teyari kuna watoto ambao wako fluent zaidi katika kuongea kingereza kuliko kiswahili.

Usisahau hata mchicha ulianza kama mbuyu.

Tutakuja tena kulaumu wazungu kwa kuua lugha yetu kama ambavyo leo hii tunawalaumu kwa kuua utamaduni wetu.

Alietuloga alikuwa fundi!!

Tatizo kiswahili chenyewe bado tatizo
 
Shule za kisiasa au kisasa umeharibu uzi mzima kwa kutokuwa makini kwenye spelling
 
Back
Top Bottom