K-wire
JF-Expert Member
- Dec 6, 2017
- 278
- 286
MAMA NA MWANA
Gozbert ; Mama wamenifukuza shule
Mama : Hivi ndo nimetoka kijiji cha Mkomanzila kwa rafiki yangu kuchukua pipa nikoroge pombe, nikiuza nitakutumia mwanangu. Kazana kusoma
Gozbert; Sawa mama naomba na pesa ya Matumizi, nitashukuru.
Mama; Sawa Mwanangu
Gozbert: Mama shikamoo, nashukuru nilipata ile pesa naomba nisaidie na pesa ya mtihani mama tumeanza usajili
Mama; Mwanangu sina hela kwa sasa jana tumelala kwa kunywa uji na wadogo zako. Nitajitahidi niende kwa Mzee Mwaka nikakope pesa za Parizi nitaenda kupalilia shamba kwa wiki nzima. Jitahidi usome mwanagu nakuombea.
Akamaliza chuo ukafika muda wa kwenda chuo.
Gozbert; Mama sina pesa kabisa, nimeomba mkopo mama nimekosa sijui nifanye nini mama
Mama; Mwanangu kama nimekusomesha kote huko chuo nitshindwaje? Namshukuru Mungu kwanza umefanya vizuri mwanangu. Nipo tayari kujaza madeni usome
Baada ya kusoma na kupata kazi nzuri mambo yakageuka
Mama; Gozbert siku hizi haunikumbuki mwanangu shida nini? Hata simu mwanangu!
Gozbert; Yaani mama majukumu ya kazi huwezi amini juzi nilikuwa Zanzibar ndo nimerudi majuzi hapa Dar. Utanisamehe mama
Mama; Kwani Zanzibar kuna mitandao tofauti nay a huku?
Gozbert; Hapana, halafu mkwe wako mjamzito kwa hiyo muda mwingi nakuwa namhudumia naporudi nyumbani.
Mama; Mdogo wako amefukuzwa shule ada inasumbua. Nilichukua pesa kidogo niliyouza pombe nikampa wameenda kumfukuza tena.
Gozbert; Mama hivi bado unatengeneza pombe? Hivi biblia inasema nini kuhusu pombe mama? Hapana mama hapo unanikwaza kwa kweli
Mama; Sawa mwanangu kumbuka nimekusomesha kwa kuuza pombe na yalaiti ungenipunguzia mzigo huu wa kusomesha, kwa kutuma pesa ningekuwa nimeacha
Gozbert; Ningekutumia sasa hivi nakimbizana na ujenzi mama, hata nikikuahidi sasa hivi nitakudanganya. Nilichukua mkopo benki kwa hiyo wananikata. Nitakupigia baadae kuna simu inaita hapa
Siku nyingine ikafuata
Mama; Nataka nije nimsalimie mjukuu wangu mwezi huu
Gozbert ; daah yaani kwa sasa hatuna pesa kabisa mama mjukuu mwezi mmoja tu zimentoka kama milioni mbili
MSIMU WA SIKUKUU
Mama; msimu wa sikukuu nataka nije nisherehekee na mjukuu wangu huko dar
Gozbert; Daah bahati mbaya likizo hii mimi na mke wangu tutakuwa uingereza kusherehekea huko. Tukirudi tutafanya utaratibu uje kutusalimia.
Tunakwama wapi watoto wa walala hoi
Gozbert ; Mama wamenifukuza shule
Mama : Hivi ndo nimetoka kijiji cha Mkomanzila kwa rafiki yangu kuchukua pipa nikoroge pombe, nikiuza nitakutumia mwanangu. Kazana kusoma
Gozbert; Sawa mama naomba na pesa ya Matumizi, nitashukuru.
Mama; Sawa Mwanangu
Gozbert: Mama shikamoo, nashukuru nilipata ile pesa naomba nisaidie na pesa ya mtihani mama tumeanza usajili
Mama; Mwanangu sina hela kwa sasa jana tumelala kwa kunywa uji na wadogo zako. Nitajitahidi niende kwa Mzee Mwaka nikakope pesa za Parizi nitaenda kupalilia shamba kwa wiki nzima. Jitahidi usome mwanagu nakuombea.
Akamaliza chuo ukafika muda wa kwenda chuo.
Gozbert; Mama sina pesa kabisa, nimeomba mkopo mama nimekosa sijui nifanye nini mama
Mama; Mwanangu kama nimekusomesha kote huko chuo nitshindwaje? Namshukuru Mungu kwanza umefanya vizuri mwanangu. Nipo tayari kujaza madeni usome
Baada ya kusoma na kupata kazi nzuri mambo yakageuka
Mama; Gozbert siku hizi haunikumbuki mwanangu shida nini? Hata simu mwanangu!
Gozbert; Yaani mama majukumu ya kazi huwezi amini juzi nilikuwa Zanzibar ndo nimerudi majuzi hapa Dar. Utanisamehe mama
Mama; Kwani Zanzibar kuna mitandao tofauti nay a huku?
Gozbert; Hapana, halafu mkwe wako mjamzito kwa hiyo muda mwingi nakuwa namhudumia naporudi nyumbani.
Mama; Mdogo wako amefukuzwa shule ada inasumbua. Nilichukua pesa kidogo niliyouza pombe nikampa wameenda kumfukuza tena.
Gozbert; Mama hivi bado unatengeneza pombe? Hivi biblia inasema nini kuhusu pombe mama? Hapana mama hapo unanikwaza kwa kweli
Mama; Sawa mwanangu kumbuka nimekusomesha kwa kuuza pombe na yalaiti ungenipunguzia mzigo huu wa kusomesha, kwa kutuma pesa ningekuwa nimeacha
Gozbert; Ningekutumia sasa hivi nakimbizana na ujenzi mama, hata nikikuahidi sasa hivi nitakudanganya. Nilichukua mkopo benki kwa hiyo wananikata. Nitakupigia baadae kuna simu inaita hapa
Siku nyingine ikafuata
Mama; Nataka nije nimsalimie mjukuu wangu mwezi huu
Gozbert ; daah yaani kwa sasa hatuna pesa kabisa mama mjukuu mwezi mmoja tu zimentoka kama milioni mbili
MSIMU WA SIKUKUU
Mama; msimu wa sikukuu nataka nije nisherehekee na mjukuu wangu huko dar
Gozbert; Daah bahati mbaya likizo hii mimi na mke wangu tutakuwa uingereza kusherehekea huko. Tukirudi tutafanya utaratibu uje kutusalimia.
Tunakwama wapi watoto wa walala hoi