1. David Mattaka (ATC):
Hakuna ndege, hakuna safari za ndege ndani na nje zinazoeleweka, hatuoni kama una program sahihi kufufua shirika letu. kuna ugumu gani kusema nimeshindwa ideas zimeniishia na uachie wengine watanzania watafute solution kwenye hili shirika?
2. Justin Mwandu (NIC):
Shirika lenye mtandao mkubwa kuliko zote Tanzania, imeshindwa kulipa wadeni wake wakiwemo walimu wa shule za msingi, umeshindwa kubuni mkakati wa kuokoa, umekuwa mwoga kupita kiasi kufanya chochote. Kuna ugumu gani kusema creativity yangu imeiishia hapo watafutwe watu wengine kutoa solution kwa shirika hili? kwanini wasijumuishiwe kule kwa Emanuel Humba (NHIF) walau kila mtanzania awe na bima ya afya ya lazima?
3. Mustafa Mkullo (MoF):
Wizara yenye dhamana ya kutoa mwelekeo wa uchumi na ukusanyaji wa pato la serikali pamoja na kuthibiti mapato imekuwa chanzo cha upotevu wa pesa za serikali, tumeishiwa na mawaziri yenye uwezo hadi uendelee kubakia wewe?
4. William Mhando (TANESCO):
Ulipoiingia tu kitu cha kwanza kufanya ni kuwaudhi wateja eti unaomba kupandisha bei ya umeme badala ya kupunguza, umeongeza gharama za kuunganisha umeme, umeshindwa kudhibiti wafanyakazi wabadirifu na wezi kwenye shirika. Hicho ndicho tulichokutuma sisi wananchi? badala ya kutoa huduma mnatukomoa? hivi unajua kwamba ukitaka kuunganisha umeme lazima ununue nguzo mwenyewe? halafu hizo nguzo mnaziita za Tanesco bila aibu? watu wote waliounganisha umeme kwa kununua nguzo wakizitoa wanapohama mtabakiwa na nini? hii aina gani ya huduma mkuu?
5. William Ngeleja (Madini na Nishati):
Umekuwa mwongo, wizara yako haijasaidia wananchi ku sera wala kiutendaji bado tunanyongwa kwenye madini hakuna udhibiti wa mapato na pia kwenye umeme kila mtu ni shahidi. Kwani lazima uongoze wewe kama huna maarifa si uache? unatutesa wananchi?
6. William Urio (PPF):
Ulitakiwa kusaidia wastaafu waliochangia sio wastaafu (bodi members). Kila mwaka wanachama rejea mikutano kule Arusha, wanakuomba ujitahidi kuwasiliana na serikali ili sheria za kukokotoa pension irekebishwe lakini wapi? husikie wahadhiri wa chuo kikuu wamekuandikia barua na mchanganuo wao hujawasikiliza. tumekupa dhamana umeshindwa..
Mmepewa dhamana na wananchi badilikeni au mjitoe?
Hakuna ndege, hakuna safari za ndege ndani na nje zinazoeleweka, hatuoni kama una program sahihi kufufua shirika letu. kuna ugumu gani kusema nimeshindwa ideas zimeniishia na uachie wengine watanzania watafute solution kwenye hili shirika?
2. Justin Mwandu (NIC):
Shirika lenye mtandao mkubwa kuliko zote Tanzania, imeshindwa kulipa wadeni wake wakiwemo walimu wa shule za msingi, umeshindwa kubuni mkakati wa kuokoa, umekuwa mwoga kupita kiasi kufanya chochote. Kuna ugumu gani kusema creativity yangu imeiishia hapo watafutwe watu wengine kutoa solution kwa shirika hili? kwanini wasijumuishiwe kule kwa Emanuel Humba (NHIF) walau kila mtanzania awe na bima ya afya ya lazima?
3. Mustafa Mkullo (MoF):
Wizara yenye dhamana ya kutoa mwelekeo wa uchumi na ukusanyaji wa pato la serikali pamoja na kuthibiti mapato imekuwa chanzo cha upotevu wa pesa za serikali, tumeishiwa na mawaziri yenye uwezo hadi uendelee kubakia wewe?
4. William Mhando (TANESCO):
Ulipoiingia tu kitu cha kwanza kufanya ni kuwaudhi wateja eti unaomba kupandisha bei ya umeme badala ya kupunguza, umeongeza gharama za kuunganisha umeme, umeshindwa kudhibiti wafanyakazi wabadirifu na wezi kwenye shirika. Hicho ndicho tulichokutuma sisi wananchi? badala ya kutoa huduma mnatukomoa? hivi unajua kwamba ukitaka kuunganisha umeme lazima ununue nguzo mwenyewe? halafu hizo nguzo mnaziita za Tanesco bila aibu? watu wote waliounganisha umeme kwa kununua nguzo wakizitoa wanapohama mtabakiwa na nini? hii aina gani ya huduma mkuu?
5. William Ngeleja (Madini na Nishati):
Umekuwa mwongo, wizara yako haijasaidia wananchi ku sera wala kiutendaji bado tunanyongwa kwenye madini hakuna udhibiti wa mapato na pia kwenye umeme kila mtu ni shahidi. Kwani lazima uongoze wewe kama huna maarifa si uache? unatutesa wananchi?
6. William Urio (PPF):
Ulitakiwa kusaidia wastaafu waliochangia sio wastaafu (bodi members). Kila mwaka wanachama rejea mikutano kule Arusha, wanakuomba ujitahidi kuwasiliana na serikali ili sheria za kukokotoa pension irekebishwe lakini wapi? husikie wahadhiri wa chuo kikuu wamekuandikia barua na mchanganuo wao hujawasikiliza. tumekupa dhamana umeshindwa..
Mmepewa dhamana na wananchi badilikeni au mjitoe?