Tumwambie mumewe ukweli au?


mi nahisi mke atakuwa ajamuonyeshe mume hiyo barua
atakuwa ameificha ndo maana mzee akaamua kwenda kuwauliza kwa maandishi
 
Napata shaka kuamini kama kweli wewe ni hr.kwani mkataba wa kazi wa huyo mama,alisign akiwa na mumewe?sasa hapo amekuja kuuliza akiwa kama nani,na nyie mtamjibu kama nani?
 
Mkataba Wa mwajiri unasemaje? Na huyo mume kaandika barua kama nani? Hebu fata procedure zote umuterminate huyo mama na uweke document zote kwenye faili lake ndo litafanya kazi iwapo huyo mama atakwenda CMA na siyo huyo mume cause kampuni haimtambui na hana mkataba Wa kampuni hope muna mwanasheria Wa kampuni iwapo huyo mume ataenda mahakamani Kwa kosa lipi? Ukijiloga kumujibu barua yake Kwa maandishi utakuwa umejifunga mwenyewe cause maandishi ndo ushaidi mzuri Wa mahakama hata kama upo right so mujibu Kwa mudomo kuwa maandishi anayo mwenye mkataba na kampuni ambaye ndo mkewe.
 

Mkuu wa kichwa ndo maana unaitwa Tiba
 
Stili aibu ya mwenzio na yako pia istiliwe ila kama unaweza tu!
 

Fuata ushauri huu na utakuwa salama.
 
Kumfukuza mtu kazi ni jambo linalofuata taratibu na kanuni na sheria.Hivyo lazima kufuata mambo hayo kwa umakini.Kwa mfano lazima mhusika aandokiwe barua ya kujieleza au suala lichunguzwe ukweli uwekwe wazi halafu ndipo barua ya kumfukuza kazi kulingana na kosa lilivyokubwa inaandikwa.Barua yenyewe ni mfanyakazi husika.

Sio ya familia wala sio ya mwenza.Kwa hiyo mme hana haki ya kujua chochote kuhusu hilo isipokuwa kupitia kwa mkewe.Sio vema kujihusisha na mme kwa suala kama hilo.Kwani waweza kujikuta kwenya matatizo kama kesi kama mme akijua kipitia kwako halafu akasababisha madhala au kifo.

Hata vile kumbuka kwamba sio lazima kila kosa litolewe adhabu.Na adhabu sio lazima iwe kubwa kadri iwezekanavyo.Kama adhabu sahihi ni kufukuzwa kazi na kweli ndivyo ilivyo basi sio lazima ndoa yake nayo ivunjike.Si vema asipate adhabu nyingine kwa sababu yako.
 
Fuata Maadili Yako Ya Kazi!
Achana Na Ndoa Ya Hao Wachepukaji Itaweka Ajira Yako Panaya!
 
atanieleza leo nikifika nyumbani,yaani anafanya umalaya ofisini kwake alafu ananidanganya mimi

Acha mkwara mr mkude loo utadhani kweli ulivyowaka...ila issue imekaa vibaya lkn naona hr ajibu tu kwa busara kuwa mke ndio mwenye jibu lkn ht hivyo mume sidhani km ana.mamlaka ya kuhoji masuala ya kiofisi
 
Ni vema ukajivua jukumu hili na umwachie mke ajibu vizuri kwa mumewe. Mwambie pia mume akamuulize huyo mkewe kama anaipinga vipi hatua iliyochukuliwa.
 
Nakubaliana na wanaoshauri umjibu mzee kwa mdomo kuwa utaratibu wa kazi hauwaruhusu kumjibu his query kwa kifungu cha confidentiality
 
Human resource does not have to disclose anything to anybody if he/she feels employee's right/provacy will be violated. In the matter of fact, you can even hid the information from the boss if he/she has an interest in the matter. So be, DO NOT disclose any information abt this incident to anybody outside these employees line of duty, otherwise you risk a huge civil suit to ur organization. Give the husband a letter asking him to refrain from soliciting your employees private matters.
 
Tiba naomba kujua hili nalo limekaaje, Mara nyingi wanawake huenda kushtaki ofisini kwa mumewe iwapo huduma stahiki ya matunzo kwa familia haipo, na Mara nyingi husikilizwa unakuta baba atakatwa mshahara wake, sehemu itaenda kwa mkewe, je kwann wakate mshahara,kwani familia au mke ndo kaajiriwa pale? Kwani na wenyewe si third part? Kwanini asiambiwe hili jambo halituhusu kamalizaneni nyumbani?
 
Last edited by a moderator:
Be extremely careful with this matter, the evidence presented to you about the matter must be anything but hear-say. You must make an informed decision not because the white-guy saw them. Obtain physical evidence about these 2 individuals conduct.

If you have to obtain their email communications pls do, but do not make your decision solely based on what the white-guy said. Anything involving a woman, MUST be handled with extreme care.What about she changed the story that the Two Men wanted to rape her in the office. What about she claim the white guy wanted her for an affair and just said that for revenge.

This is the time the Organization's legal counsel steps in and not Jamii Forum.If you do not have a company's lawyer, pls ask the organization to pay for you to consult one before you proceed. Well, Bongo hakuna sheria anyway I guess you can whatever you want bro..
 
Anyway mkuu unaweza usimweleze ukweli this time lakini nina uhakika taarifa atazipata tu kwa baadae.mweleze mzee kuwa mkewe ametenda kosa kinyume na taratibu na maadili ya kiutumishi.akiuliza kosa gani mwambie huruhusiwi kutoa taarifa za ofisi kwakuwa siyo maadili ya kazi.ila huyo mama ni ndorroooobo.
 

Ndugu yangu kama hayo maelezo yako ndivyo ilivyo, huyo HR anapashwa kibarua chake kioteshwe nyasi. Hakuna cha kujadili hapo, huyo Mzee hana haki ya kuuliza ni kwa nini mke wake amesimamishwa kwani kampuni haina mkataba wowote na huyo mzee. Mwenye mkataba ni mke wake. Hayo maswali yake akamuulize mkewe kwani yeye ni mtu mzima na anao uwezo wa kujieleza.

Kazi zina taratibu zake Bwana. Kwa mfano mume wangu hata kama nimemuandikisha ofisini kama mume, nisipotaka kumwambia nalipwa shilingi ngapi kwa mwezi, hawezi kuja ofisini kudai ofisi imwambie nalipwaje. Hata akija ofisi haipashwi kutoa jibu. Ni sawa na hii issue, huyu HR hakupashwa kutoa nafasi ya ili suala kujadiliwa kiofisi wala kutoa ahadi ya kuijibu barua. Kama alifanya hivyo, basi hiyo nafasi haimfai hata kidogo.

Hapa nazungumzia taratibu za kazi zilivyo, huyo mume ni third party hana haki ya kuhoji chochote kinachohusu ajira ya mke wake iwe kwa mdomo au maandishi. Ningekuwa ni boss wa huyo HR, mpaka sasa angekuwa kazi hana kwa kuukaribisha huu ujinga.

Tiba
 
Kanuni za utumishi (standing order)zinatambua haki za mume,mke na mtoto kwahiyo mwenza yeyote ana haki ya kwenda kushtaki kwa mwajiri kwa issue yeyote inayoathiri familia kwa namna moja ama nyingine.kwa upande wa suala la huyu mzee na mkewe ni haki kabisa kwa mwajiri kumweleza ukweli mwanaume tatizo lililopelekea mkewe kuachishwa kazi.lakini sisi kama binadamu sometime unatakiwa kutumia busara na kuona side impact endapo utaeleza ukweli wa jambo hilo.
 
mkuu mke wa jamaa yeye vipi, hakuja? manake wote si wana ndoa zao
 

Mume ana haki ya kujuwa ukweli. Kama mwajiri ataamuwa kumweleza wala haitakuwa na shida kwani kanuni zinamlinda.hapa ni mwajiri kutumia busara kuona kwamba jambo hili akieleza litaweza kuwa na madhara gani kwa familia ya mtumishi aliyesababisha makosa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…