Tumwambie mumewe ukweli au?

huyo mmewe anahusika vipi na mambo ya kiofisi...mpotezee wala usimjibu.
 
Wanatuogopesha kuoa wengine we mpaka uzee lkn anachepuka
 
Well, nadhani kila ofisi ina utaratibu wake, na according to the story inaonyesha hiyo ofisi wako obliged kufanya hivyo, ndio maana wamemuahidi watamjibu na wameshajadili namna ya kumjibu pia.

Ningependa nijue hiyo ni ofisi gani inayo entertain ujinga kama huu. Mume wa huyo mama ni third party kwenye hiyo kampuni na hivyo hawawajibiki kuijibu hiyo barua. Huyo mume akitaka sababu amuulize mkewe after all aliposimamishwa kazi alipewa barua. Amuulize mke wake amuonyeshe hiyo barua. HR anayejua taratibu za kazi hawezi kukubali kufanya ujinga eti wa kujibu kwa maandishi. Yaani mpaka nasikia kichefuchefu na huyo mleta mada hiyo kazi ya HR haimfai kabisa.

Tiba
 

Ni kweli. Ila pia Kisheria mwajiri ana obligation ya kusema ukweli na kutoa sababu za msingi za kumsimamisha kazi mwajiriwa. Nadhani pia mume ana haki ya kufuatilia haki za mkewe kisheria, kama atahisi uonevu. Labda wao kwa kutaka kutoleta matatizo katika hiyo ndoa, waliamua ku-cover ukweli katika barua ya kumsimamisha kazi huyo mama, na mzee kawapa nafasi ya kusema ukweli kabla hajachukua hatua yoyote.

Wakimpotezea na akaenda mbele na uchunguzi ukafanyika, ikagundulika walidanganya, there will be consequences kwa upande wa ofisi.
 
Hr asiyejua cha kufanya

Huyo mumewe amewahoji kwa barua yeye akiwa kama nani? Mliingia makataba na mke au mume? ??

Anyway mwambieni alivunja kanuni na taratibu za ofs.....mengine hayawahusu

Mkuu Mchakavumlasana, tuko pamoja hapa ila ofisi haina wajibu wa kumwambia chochote huyo, akamuulize mkewe, ni mtu mzima na ana uwezo wa kujieleza mwenyewe kwa nini atake maelezo kutoka ofisini? Niliisha sema nina wasiwasi na uwezo kiutendaji na huyo HR. Huyu HR eti bila aibu anasema alimuahidi kumjibu kwa maandishi, you must be out of your mind mr/mrs HR.

Tiba
 
Barua ya kumsimamisha kazi (heading yake) inasemaje? Kwa sababu usije ukamdanganya Mr. wake akadai kopi au wanoko wameshampa kopi sasa anataka uthibitisho kutoka kwako maelezo yakapishana au mmewasimamisha bila maandishi? Eleza Mkuu

Mchane live mme wake ajue kuwa ameoa Malaya na sio mke,wewe unadhani upuuz kama huo kwa nini asifanyie hata kweny gari km kweli yy ana master ya ngono Au aende kwa wenzake kona bar akatege. Hv na hilo kubwa jinga umeliuliza kwa nn linamgegeda mama wa watu ofisini?
 
ndugu yangu, kwanza nikupe pole kwa changamoto hiyo ila ushauri wangu ni kwamba kamwe ucje changia kuvunja ndoa ya huyo mama kwani mwenye kutenganisha ndoa ni MUNGU pekee na c binadamu ila kwa habari ya uzinzi mume anaweza kumwacha mkewe na hili jambo ni mpaka mume atakapomfumamia live cku ya 40. hebu fikiria mama huyo ana familia na watoto wakubwa na leo hii aachike kwa sababu umemwandikia barua mumewe na kumweleza kuwa alifumwa akifanya mapenzi ofcn.! mie nakushauri mweleze mumewe kwa mdomo tu na kwa barua kuwa ninyi mnawajibika kwa mwajiriwa wenu na c kwake hivyo basi mwenye jukumu la kumwelexa kulikoni ni mkewe.! maana ukimjibu kwa barua tena kwa kutumia uongo mzee huyo anaweza kwenda mahakamani kuwashitaki kwa kutumia barua yenu kama ushahidi na hapo ndo msala utaanzia.!!
 

Mkuu sina uhakika na utaalamu wako kwenye mambo ya HR lakini mume wake na huyo Mama hana uhusiano wowote na hiyo kampuni kiasi cha kufikia kutaka maelezo kwa maandishi. Mke ni independent legal entity na mume hana nafasi ya kwenda kuhoji ni kwa nini mke wake alisimamishwa. Kwa nini asimuulize mkewe? Mkewe ni bubu hawezi kuongea? Na wakati anasimamishwa si alipewa barua? Apewe hiyo barua na mkewe asome period.

Tiba

Tiba
 
Kimsingi nyie kama Kampuni hamna wajibu wa kudeal na huyo mume kiofisi kwa suala ambalo sio Company business kwake yeye (mume) bali mkewe. Hivyo, kwasababu partner mliyefunga naye kandarasi ni mkewe, unatakiwa kumjibu tena sio kwa barua kuwa suala la mkewe atafahamishwa yeye mwenyewe baada ya maaumuzi ya vikao husika. Kama anataka kufahamu, mkewe atamfahamisha ila nyie hamwajibiki kwake.
 
Wengine bado tunazienzi ahadi za mwanatanu"nitasema kweli daima fitina kwangu mwiko.
 

Kiongozi;Mi nakushauri mchane live mumewe haya masuala ya kulindana hata kweny vitu ambavyo wala sio vya kulindani,ndio yanasababisha mmomonyoko wa maadili hata mkimficha mumew Mungu atamuonyesha hiyo tabia ni mbaya sana na ni aibu hana tofauti na mnyama.......Fanya maamuz magum kama wa Monduli
 
huyu mzee aende akalalmke kama nan?? what if yule mama akienda kuwashtak kwa kutoa
privacy zake kwa third party?
 
Yawezekana kashamdanganya mumewe kuwa mnamtaka kimapenzi ndo mume anakuwa na mahasira akidhani mtamjibu hiyo barua yake.katu msimjibu kimaandishi,mwambieni kuwa hakuna kipengele ktk mkataba kinachotamka kuruhudu kumshirikisha mwenza wa mwajiriwa ktk masuala ya kazini.
 
ma hr siku hiz mmeamua kwlei...kila siku lazima pawe na thread ya hr humu!!

juzi kulikuwa yule hr ambaye mke wake alipata ziro kwenye interview!!! nk... btw huyo mkanada alichukua hata picha?..solid evidence anayo?
 
Naungana na huyo naiman64 usidangaye afu na wewe baadae yakakugeukia sema ukweli kama utaongopa bac dhambi hiyo nawe utakuwa umeshiriki
 
Boss, Sina utaalamu na mambo ya HR, na sijaajiriwa bado. Nimejaribu kuongea kulingana na story ilivyo. Naweza kutokuwa sawa.

According to the HR of moment here, huyo mzee ana wajibu/haki ndio maana walikaa kujadili kama wamwambie ukweli ama lah, na ndio maana huyo mama alienda kumlilia huyo boss wake ili asiseme ukweli, na ndio maana pia walimuahidi huyo mzee kwamba watamjibu, na ndio maana yuko hapa kuomba ushauri wa namna ya kumjibu.

Now, i'm sure 'Mr HR' anajua sheria na utaratibu wa ofisi yake better than anyone here, na kama yeye anadhani huyo mzee anastahili kupewa maelezo, then that's it.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…