Tumuenzi Mandela kwa kupinga ukaburu Tanzania

Jeanclaude

JF-Expert Member
Aug 30, 2013
259
237
Tuache unafiki watanzania kujifanya tunaudhamini mchango wa Nelson Mandela wa kupambana na ubaguzi wakati huku nyumbani tunaendekeza mawazo ya kibaguzi. Hapa kuna wanasiasa wanaeneza chuki za kibaguzi dhidi ya wachaga, wanasambaza chuki kwa msingi wa udini na ukanda kwa malengo ya kisiasa tukiwafumbia macho. Huo ni ubaguzi kama ule wa makaburu tofauti yake ni kuwa ule wa makaburu msingi wake ulikuwa rangi ukiwa na uhalali wa kisera na kisheria. Kama tunataka kumuenzi madiba bila unafiki tuupinge ukaburu hapa hapa nyumbani.
 
Back
Top Bottom