Mwigamba Muchimati
Member
- Dec 4, 2018
- 15
- 28
Wakati mfanyabiashara Mohammed Dewji maarufu kama Mo alipotekwa, polisi wetu walifanya kazi nzuri sana kumtafuta ikiwa ni pamoja na kuwatafuta watekaji.
Kamanda wa Polisi Kanda maalum ya kipolisi Dar es Salaam Lazaro Mambosasa alikuwa msitari wa mbele kutujulisha kila hatua waliyofikia. Tukaambiwa jinsi walivyofuatilia mpaka nyumba alikopelekwa Mo, mpaka gari lililomtelekeza pale gymkhana tukaonyeshwa. Tukaambiwa hata juhudi zilizofanywa na watekaji hao kujaribu kuliteketeza gari ili kupoteza ushahidi, japo walishindwa. Tukaona mwishoni Mo akiwa na akina kamanda Mambosasa.
Kwa jinsi sakata lile lilivyokwenda ingawa tulikuwa na mashaka mashaka tulilazimika kumwamini kamanda Mambosasa na hata IGP Sirro.
Kumbe yale mashaka ya intelijensia ya akina Mambosasa hayakuishia kwetu tu yalikwenda mpaka kwa mkuu wa nchi. Akawaonya kwamba wasidhani Watanzania ni wajinga. Kweli hatukuwa wajinga katika hilo ila tulilazimika kuwaamini polisi wetu.
Sasa yule yule aliyeonywa kutodhani Watanzania ni wajinga, amekuja tena na taarifa nyeti ya kifo cha Lwajabe. Amejitahidi kueleza kitaalam lakini tunaweza kumuuliza swali moja tu kwamba kama Lwajabe aliamua kujinyonga, KWANINI AACHE MITI YOTE kuanzia nyumbani kwake Kinyerezi hadi Kongowe mpaka aende Mkuranga? Sikatai mtu kujinyonga, ila maelezo ya polisi wetu yasije mwishoni mkuu akajitokeza tena na kusema wasidhani Watanzania ni wajinga.
Kamanda wa Polisi Kanda maalum ya kipolisi Dar es Salaam Lazaro Mambosasa alikuwa msitari wa mbele kutujulisha kila hatua waliyofikia. Tukaambiwa jinsi walivyofuatilia mpaka nyumba alikopelekwa Mo, mpaka gari lililomtelekeza pale gymkhana tukaonyeshwa. Tukaambiwa hata juhudi zilizofanywa na watekaji hao kujaribu kuliteketeza gari ili kupoteza ushahidi, japo walishindwa. Tukaona mwishoni Mo akiwa na akina kamanda Mambosasa.
Kwa jinsi sakata lile lilivyokwenda ingawa tulikuwa na mashaka mashaka tulilazimika kumwamini kamanda Mambosasa na hata IGP Sirro.
Kumbe yale mashaka ya intelijensia ya akina Mambosasa hayakuishia kwetu tu yalikwenda mpaka kwa mkuu wa nchi. Akawaonya kwamba wasidhani Watanzania ni wajinga. Kweli hatukuwa wajinga katika hilo ila tulilazimika kuwaamini polisi wetu.
Sasa yule yule aliyeonywa kutodhani Watanzania ni wajinga, amekuja tena na taarifa nyeti ya kifo cha Lwajabe. Amejitahidi kueleza kitaalam lakini tunaweza kumuuliza swali moja tu kwamba kama Lwajabe aliamua kujinyonga, KWANINI AACHE MITI YOTE kuanzia nyumbani kwake Kinyerezi hadi Kongowe mpaka aende Mkuranga? Sikatai mtu kujinyonga, ila maelezo ya polisi wetu yasije mwishoni mkuu akajitokeza tena na kusema wasidhani Watanzania ni wajinga.