Tumia M-Pesa at your own Risk!

Tumia M-Pesa at your own Risk!

Nilipokea malipo kutoka sehemu ninawafanyia kazi Fulani meseji ikaja nusu bila zile pin nos kwakweli usumbufu nilioupata mpk kuipata hiyo pesa ulitosha kuwa disqualify!
 
Kwa sasa hiyo kampuni aina wafanyakazi mahiri,huwezi kupata taarifa sahihi kutoka kwao
 
nami nagongelea hapo hapo kama mhanga sugu wa transactions/miamala ya ki-elektroniki.

19.10.2017 nimenunua umeme kwaajili ya mashine ya kusaga kupitia MOBISTOCK. nikakatwa 20,000 na meseji yao ikatumwa kwamba salio limetumwa TANESCO na kwamba token zitatumiwa kwenye simu yangu.

nimezoea meseji ya arifa kuwa pesa imekatwa huambatana na ya tokeni (namba zinazojazwa kwenye mita). siku hiyo ikapita hadi zaidi ya dk 30. nikapiga simu. tena hii huduma ya mobistock unapiga simu kwa gharama halisi. sio bure km zilivyo huduma nyingine. nikajibiwa tatizo liko tanesco. kesho yake 20.10.17 nikapiga, 21.10.17 hadi 25.10.17 hadi leo hii sijapokea tokeni na salio halijarejeshwa.

wahudumu sasa wamebaki kunifokea kwamba tufanyeje sasa hali tatizo liko tanesco?

nami nahoji, nimuulize nani sasa endapo ninyi ndio watoa huduma, basi nipeni namba ya tanesco nishughulikie mwenyewe, wao hukata simu.

ebu fikirieni 20,000/= ya kununua lau 56kwh ingeshazunguka mara ngapi. imeshikiliwa kwa siku 12+ sasa.

hii ndiyo Tanzania na maisha yanasogea tu!
 
Kuna mengi yamewakuta watumiaji wa mpesa mtawasikia
nilikuwa na mizunguko zaidi ya wiki moja sasa imeisha, nawaza zikifika siku 14 nikatoe taarifa polisi maana hili ni suala la kibiashara. uzuri zimetumika namba zangu binafsi, na tin namba ya hilo jina la kibiashara inalitaja jina langu. sijui kama nitakuwa sahihi. wajuvi wa masuala ya sheria naombeni msaada tafadhali.

nimeshawatumia meseji ya reference ya muamala kwenda namba yao ya huduma kwz wateja lakini hata kujibu kumekuwa aghali kwao.

nawaza hawa ndio wanaotuchelewesha kutufikisha kwenye maendeleo.
 
sita wasahu hawa watu....walikula hela hivihvi...nilifanya transactio ikakaa hewani kwa week tatu eakaniambia itarudishwa kwangu bt kitu cha ajabu kabisa ni kwamba baafa ya week tatu ile transaction ilifanikishwa. Wakati huo nilishamaliza shida yangu kwa kutumia Mtandao mwingine. M pesa ni wezi hakuna mfano
 
nami nagongelea hapo hapo kama mhanga sugu wa transactions/miamala ya ki-elektroniki.

19.10.2017 nimenunua umeme kwaajili ya mashine ya kusaga kupitia MOBISTOCK. nikakatwa 20,000 na meseji yao ikatumwa kwamba salio limetumwa TANESCO na kwamba token zitatumiwa kwenye simu yangu.

nimezoea meseji ya arifa kuwa pesa imekatwa huambatana na ya tokeni (namba zinazojazwa kwenye mita). siku hiyo ikapita hadi zaidi ya dk 30. nikapiga simu. tena hii huduma ya mobistock unapiga simu kwa gharama halisi. sio bure km zilivyo huduma nyingine. nikajibiwa tatizo liko tanesco. kesho yake 20.10.17 nikapiga, 21.10.17 hadi 25.10.17 hadi leo hii sijapokea tokeni na salio halijarejeshwa.

wahudumu sasa wamebaki kunifokea kwamba tufanyeje sasa hali tatizo liko tanesco?

nami nahoji, nimuulize nani sasa endapo ninyi ndio watoa huduma, basi nipeni namba ya tanesco nishughulikie mwenyewe, wao hukata simu.

ebu fikirieni 20,000/= ya kununua lau 56kwh ingeshazunguka mara ngapi. imeshikiliwa kwa siku 12+ sasa.

hii ndiyo Tanzania na maisha yanasogea tu!
Hii mambo inachanganya sana, kwa hiyo mpaka leo hii bado hujapata token?
 
sita wasahu hawa watu....walikula hela hivihvi...nilifanya transactio ikakaa hewani kwa week tatu eakaniambia itarudishwa kwangu bt kitu cha ajabu kabisa ni kwamba baafa ya week tatu ile transaction ilifanikishwa. Wakati huo nilishamaliza shida yangu kwa kutumia Mtandao mwingine. M pesa ni wezi hakuna mfano
Wapuuzi sana mimi walirudisha baada ya kuwaanzishia kizaa zaa kwenye page yao FB, na hapo nishakaa zaidi ya siku ishirini wanarudisha pesa tayari nishatatua ishu yangu. Hovyo sana tena hao customer ni vihiyo waliotukuka!
 
  • Thanks
Reactions: MTK
Ni wizi tuu huo mbona kipindi cha nyuma Voda mlikua mnarudisha pesa haraka sana pindi mtu akikosea sasa hivi watu hawakosei ninyi ndio mnawaibia ni hatari sana kwa kweli kutumia mitandao yenu kutuma fedha...
 
  • Thanks
Reactions: MTK
Ni kweli kwamba Use Mpesa au mtandao mwingine wa pesa at your own risk and only when very very neccesary kwa sababu mbili kuu 1. Matukio ya kupotea kwa pesa yameongezeka sana na 2. tunapoteza pesa nyingi sana kwenye mitandao hii. Inaelekea kuna kamchezo wanafanya kutuibia kijanjajanja! TCRA kama regulatory body wanatusaidiaje wananchi au nao wamekuwa embedded?!
 
Mi mwemyewe nilifanya manunuzi ya mpesa kwao ilikuwa usiku. Huduma sikupata na pesa sijarudishiwa hadi leo. Kila ukipiga wanakwambia baada ya 24hrs sasa ni wiki tatu hadi nimechoka
 
Airtel money huwa wako fasta sana, shida tu mawakala wachache na watz wamekariri
 
Nilifanya transaction ya CRDB to Mpesa ilikuwa Ijumaa,ilikuja fanikiwa Jumatatu hapo toka Ijumaa nawapigia customer care wa SimBanking Crdb wananiambia tunashughulikia thn kufika jumamosi wakaniambia wanaohusika hawapo kazini mpaka jumatatu dah.
 
Mi mwemyewe nilifanya manunuzi ya mpesa kwao ilikuwa usiku. Huduma sikupata na pesa sijarudishiwa hadi leo. Kila ukipiga wanakwambia baada ya 24hrs sasa ni wiki tatu hadi nimechoka
Hutakiwi kuchoka bro hilo ni jasho lako how come useme umechoka? Mie pamoja na kukaa siku kibao sikukata tamaa kila nilipopata muda niliwapigia kuwakumbusha. Katika pita pita zangu huko FB nikakutana na page yao aisee nliwavuruga hadi pesa yangu ikarudi hapana chezea pesa kizembe zembe arifu.
 
Binafsi nafahamu kua wanakuaga na utaratibu was kusubirisha mteja.
Ila ninachoshangaa nikwanini Mimi hawaniletei huo ujinga?.
Mfano hai mdomoni kwangu salamu ni tusi, sura ya kinyonge, mkwara zaidi ya mgambo, nikipiga sim huduma kwa wateja naanza na kukariri Nina la mtoa huduma.
Nikianza mazungumzo namwambia unajua Fulani (namtaja jina) namwambia nibora ukanisaidia sasa kuliko baadae maana nitakushughulikia kisawasawa.
Utasikia usiwe Mkali, kua na subira unamwambia tuna zakwenuzilizopo kwenye sistim zakwangu zikiwa tayari rudishia hapo. Hutaki nitadili na Wewe na sio kampuni maana upon hapo kwaajili hiyo.
Utashangaa wanakuhudumia kwa wakati na SMS ya msamaha.
 
Peleka malalamiko yako tume ya mawasiliano (TCRA), ukiwa na barua rasmi yenye maelezo yako na nakala za vielelezo kutoka Mpesa. TCRA ndiye regulator wa mitandao ya simu. Pia kwa sababu mtandao wao unajihusisha na mambo ya pesa peleka malalamiko yako Benki kuu ambao ndio hutoa leseni ya kufanya biashara ya pesa kukomesha uhuni unaofanywa na hawa viumbe.
Next time nafanya hivi maana pia nishachezewa
 
elec000|ROBERT SENDABISHAKA
Meter 43153613864
Receipt SELCOM3EMDB90075213
Units 56.20kWh

Token 3137 6873 7127 1003 7736

Cost TZS 16,393.45
VAT 18% TZS 2,950.81
EWURA 1% TZS 163.93
REA 3% TZS 491.81
TOTAL TZS 20,000.00

JF nitaipigania popote. msg hii nimetumiwa saa 19.35 baada ya kuwachokonoa hapa. nimejikuta nawiwa kutuma meseji tu kuwa sijapokea umeme. nikapokea msg yao kuwa nitume namba ya mita.

daima
HAKI HAIOMBWI, INADAIWA!
 
Ni wizi tuu huo mbona kipindi cha nyuma Voda mlikua mnarudisha pesa haraka sana pindi mtu akikosea sasa hivi watu hawakosei ninyi ndio mnawaibia ni hatari sana kwa kweli kutumia mitandao yenu kutuma fedha...
kina uzi wao humu wenye sticky lakini waliutelekeza utadhani jamaa walianzisha ujenzi wakaishia msingi kisha mwenye nyumba akapata kesi na kufungwa jela. msingi hauna hata wa kung'olea magugu.

inauma sana kwakweli. na vijichenji vyenyewe tunavidunduliza kwa kuuza njugu, kodi ya tra humo humo, kodi ya pango, leseni za biashara, service leavy, tfda, mlinzi, mfanyakazi anyofoe chake looh. ndio maana mazao yameongezeka masokoni. wengo wameamua kulima. ujasiliamali si kwa enzi hizi!
 
Back
Top Bottom