Tumia M-Pesa at your own Risk!

Tumia M-Pesa at your own Risk!

POLE MI KUNA KIPINDI WALINISUMBUA NIKAINGIA TWITTER NIKAWATUNISHIA MISULI WITHIN SECONDS PESA IKARUDI KWENYE SIMU YANGU LAKINI HAPO NILISHAKAA SIKU ALMOST 6 ZA KAZI
Customer care hawana msaada full longo longo. Mbinu uliyotumia niliwahi kuitumia tigo, kwenye akaunti yao ya FB pesa ilirudi baada ya dk kadhaa.
 
M-pesa kesi za wateja wao ni nyingi sana,wanatakiwa wajitathimini au waachane na hiyo huduma ya m-pesa!
 
Ukiwa unaongea nao wao wanaona ni simple tu na wanakujibu simple tu kuwa kuna matatizo ya mtandao pesa yako itarudishwa baada ya masaa 72.Ila kiukweli ni kwamba kat ya wale macustomer care tunaoongea nao kuna mtu wenye uwezo wa kufanyia kazi tatizo husika na kuna wale wenzangu na Mimi.Fika vodashop iliyo karibu nao huku ukiendelea kufanya mazoezi ya kuwapigia simu kila wakat
ukiambiwa usubiri na ukasubiri kweli itafika tar 10 mwez ujao.Wasumbue sn upate pesa yako
Kweli kabisa wasumbufu sana, niliambiwa nisubiri baada ya saa 24 pesa itarejeshwa, muda wa saa 24 ukapita bila hata senti kurejeshwa. Nikapiga tena nikaambiwa itarudi baada ya saa 72, muda ukafika hola! Jamaa wasumbufu sana.
 
HEE MKUU TULIZA JAZBA HUWA WANAUDHI MI NILIGHAFILIKA SANA KWAKWELI NIKAWAPA MAKAVU LIVE KULE TWITTER WAKARUDISHA PESA ZANGU NA NILIANZISHA THREAD YA KUKAMPENIA WATU WASITUMIE MPESA HAHAHAHA WAKARUDISHA MAANA NILISHINDWA KABISA KUWAVUMILIA HALAF CUSTOMER CARE WANAKUJIBU KAMA WAPIGA RAMLI CHONGANISHI MAANA HATA HAWAELEWI ...A WALA B
UKIZIDISHA MASWALI WANAKUKATIA SIMU
Kabisa wanakata simu hata mimi imenitokea wamenikatia simu zaidi ya mara mbili. Halafu wako baadhi yao hawana ufahamu wa kazi yao wapo wapo tu.
 
Wanaiba pesa za wateja kuzitumia huku wakizungusha na kusubiri mwingine atoe hiyo pesa ili wakurudishie.. huku huyo mwingine watamzungusha kama wewe..

Ni kitu kinashangaza sana. Kama upo Dar nenda makao yao makuu ukapige kelele hadi kieleweke.
At least huku unaweza kueleweka sio kuleeeee! Yani kule huwa unavuruga hatari
 
Kabisa wanakata simu hata mimi imenitokea wamenikatia simu zaidi ya mara mbili. Halafu wako baadhi yao hawana ufahamu wa kazi yao wapo wapo tu.
karibia woote hawaelewi wako hapo kwa kazi ipi hawana majibu sahihi kwa wateja wakati mwingine unaweza kufikiri wale walinzi wa makampuni ndo wanapokea hizi simu
 
Mpesa ilikuwa zamani sio sasa mabraza men na machek sister kibao ofisini ngojeeni maumivu mnaotumia mpesa
 
Hilo ni wazo jema!
Mnishauri mwanasheria wa ku pursue!

Wiki iliyopita nilituma pesa kwa M Pesa, mpokeaji akawa akisubiri notification ya pesa kuingia. Akaamua kucheki salio akakuta pesa imeingia na notification hadi leo hajaipata.

Tukumbuke hii ni teknolojia na saa yeyote inaweza kutofanya kazi kabisa kwa muda fulani au kutegemea na ukubwa wa transaction mambo ya security na verification yanaweza kuchelewesha muamala au notification. Hizi flaws za teknolojia zipo kwenye taasisi za fedha, ila sio lazima zitokee na zinaweza kuzuilika.

Hivyo kabla ya lawsuit, ni vema kujua chanzo cha tatizo ili kujiridhisha kama sababu ni wizi, uzembe au ajali ya kiteknik.
 
Nimelazimika kulalamika katika mtandao huu wa JF maana naona M-Pesa sasa hivi ni very risky.

Jana nimemtumia mtu pesa kwa M Pesa akiwa dukani ili anunue madawa muhimu sana kwa mgonjwa. Jama dawa kazipata zote na zilikuwa na gharama kubwa. Nikatuma hela kwa M-Pesa immediately.

Baada ya nusu saa meseji ajapata kuwa pesa imeingia kwake. Nikawapigia M Pesa kwa huduma ya jamoo, namba 100. Jibu standard, tunatuma ujumbe mwingine. Baada ya nusu saa tena meseji haijaenda.

Nikapiga tena no 100 huduma kwa wateja, jibu bado standard, tutatuma meseji tena. Baada ya masaa mawili bado meseji y kuchukua fedha haijaenda, nikawapigia MARA YA TATU! Jamaa wa Voda M-Pesa wananiambia , tatuma meseji tena, tukusaidie tatizo jingine?

I blew my top.
Rudisheni hela yangu immediately, kama mmeshindwa kutuma. Jamaa wa M Pesa , itabidi usubiri withi 24hrs!

Leo napiga no 100 huduma kwa wateja , wananijibu, inabidi usubiri siku nne kurudishiwa pesa!! Mgonjwa wangu kue yuko hoi bin taaban.

USE VODACOM M-PESA A YOUR OWN RISK!!
Mimi najitoa.
Hizo ni hasira tu mkuu. Hapana shaka umekua ukitumia huduma ya mpesa kwa muda ss matatizo madogo ya kimtandao ndo yakupe uhakali wa kutoa matamshi hayo? Nonsense!

Ninajua jamaa wana utaratibu na hela yako haipotei. Kumbuka kuna systems na wanadamu na vyote haviko 100% ktk utendaji japo ni jukumu lao kuhakikisha mteja anapata huduma bora. Mfano mm tangu nimejiunga na huduma za vodacom nikiwa chuoni 2004 sijawahi juta nimesgatumia pia tigoline yaani hakuna ambako hakuna changamoto hilo uelewe. Kama haikukupata ww basi mwingine. Na hizo changamoto ndizo zinawafanya wazidi kuboresha huduma.

Hv umewahi kujiuliza mchango wa moesa kwenye uchumi wa nchi? Unajua mpesa inazungusha hela ngapi kwa siku? Unajua kuwa kuna usimamizi mkali toka benki kuu kwenye hizi huduma za kifedha au unadhani ni holela?

Kibinadamu najua uliumia kwa kutopata huduma in real time lkn haifai kutoa matamshi hayo. Mpesa ina zaidi ya watumiaji mil6 Tz. Je ukijisema ww pekeyako unajua ni % ngapi ya watumiaji?
 
Ni wakati wa Watanzania kuyashitaki haya makampuni yanapotokea matatizo kama haya maana wametuzoea mno hawa watu..
Yani Nataka issue kama hii inikute waone na huy umasikini unaotutawali naona Ni wakati wankutumia taalima kutajirika...kama vip Mzee niuzie hiyo Kesi tutakula nusu kwa nusu!!
 
Back
Top Bottom