Tumia kanuni hii kutibu maumivu makali ya mgongo/ kiuno na miguu yako

Baba Vladmir

JF-Expert Member
Aug 31, 2021
271
447
Bila shaka hamjambo watu wa Mungu! Kwa wale wenye changamoto za kiafya na wanaendelea kuteseka na maumivu juu ya magonjwa waliyonayo, Mungu atawaponya.

Katika dunia ya sasa kumekuwa na wimbi kubwa sana la watu wanaoishi kwa kutumia dawa za kutuliza maumivu kila siku iendayo kwa Mungu,mara nyingi dawa hizo ni zile za kumeza kama vile diclopar, diclofenac, piroxam, muscle plus na nyingine nyingi.

Changamoto ya maumivu ya viungo imeongezeka sana kwa sasa ukilinganisha na zama za zamani ambapo iliwakumba sana watu wenye umri mkubwa, lakini siku hizi ni kawaida kukutana na vijana wadogo wenye shida hiyo.

Ikumbukwe kuwa kutumia dawa za maumivu haikupi kupona ugonjwa ulionao, bali ni kuendelea kuugua bila kusikia maumivu. Utumiaji wa dawa za kumeza kila siku unaweza pia kuacha madhara mengi mwilini na wakati mwingine kufanya misuli na neva za mwili kuwa tegemezi wa madawa hayo.

Basi leo ninakufundisha mchanganyo wa kawaida kabisa ambao utautumia wakati wowote utakapokuwa unasumbulia na maumivu katika sehemu ya mwili wako,hususani katika maeneo niliyoyataja hapo juu. Elimu hii ninakupa bure kabisa bila gharama yoyote, hivyo ni wewe tu kuzingatia.

Dawa hii inaandaliwa kwa mchanganyiko wa vitu vofuatavyo;
  1. Mafuta ya mzeituni( Olive oil)
  2. Pilipili kichaa iliyosagwa vizuri
  3. Ng'watya( unga wa mzizi).Hili ni jina la kibantu kwa mikoa ya Tabora, Mwanza, Shinyanga, Geita na Simiyu wanauelewa vyema huu mmea. Kwa wale wasioulewa ni mmea mkali ukinuswa puani, unaponusa unga wake unaweza kupiga chafya mfululizo mara kadhaa na unatumika katika tiba ya magonjwa mengi.
Changanya kijiko kimoja cha unga wa pilipili kichaa katika robo lita ya Olive oil, then ongeza vijiko vitatu vya unga wa mzizi wa Ng'watya.Koroga na hakikisha vinachanganyika katika uwiano sawa. Tumia kuchua sehemu ya maumivu mgongo/kiuno/miguu ama mabega mara mbili kwa siku.Chua asubuhi na jioni.

Dawa hii inafanya kazi kwa ufanisi mkubwa na hupunguza na kuondoa maumivu ndani ya dakika chache baada ya zoezi.Badala ya kumeza vidonge kila siku unaweza kutumia njia hii kama mbadala ili kupunguza madhara huku ukipambana kujitibu zaidi.

Mungu akupe wepesi na akuponye shida hiyo.
 
Mkuu Disk degenerative inatibika vipi?
🤔
Hii ni normal condition over aging,ingawa inaweza kuhusisha mtu wa umri wowote kulingana nature ya kazi ama ajali.Hii inaweza kutibika kwa kufanya mazoezi yanayohusisha uangalizi maalum,lakini pia pingili za uti wa mgongo zinaweza kusagana kwa sababu ya kupoteza ile asili ya ute wake ambao hufanya kazi kama shock absorber hivyo kusababisha vimbe chungu na maumivu makubwa yanayoweza kupelekea baadhi ya sehemu za mwili kuuma,hii inaweza hutibika kwa home remedy ili kurudisha hali ya asili.Vinginevyo kama kuna break ya disk ama disk kucheza hii huhusisha zaidi mazoezi pamoja na dawa za kupunguza maumivu ya neva.
 
Hii ni normal condition over aging,ingawa inaweza kuhusisha mtu wa umri wowote kulingana nature ya kazi ama ajali.Hii inaweza kutibika kwa kufanya mazoezi yanayohusisha uangalizi maalum,lakini pia pingili za uti wa mgongo zinaweza kusagana kwa sababu ya kupoteza ile asili ya ute wake ambao hufanya kazi kama shock absorber hivyo kusababisha vimbe chungu na maumivu makubwa yanayoweza kupelekea baadhi ya sehemu za mwili kuuma,hii inaweza hutibika kwa home remedy ili kurudisha hali ya asili.Vinginevyo kama kuna break ya disk ama disk kucheza hii huhusisha zaidi mazoezi pamoja na dawa za kupunguza maumivu ya neva.
Asante kwa maelezo mkuu!
Ila tangia mwanzo naelewa hili tatizo linasababishwa na nini, nilichohitaji kujua tu ni naweza vipi kulitibu.
 
Asante kwa maelezo mkuu!
Ila tangia mwanzo naelewa hili tatizo linasababishwa na nini, nilichohitaji kujua tu ni naweza vipi kulitibu.
Inawezekana kutibika.Eleza japo kidogo ili tusaiduane,wewe/huyo mwenye shida hiyo imempata lini na chanzo chake ni kipi,kama ni kwa sababu ya umri pia tufahamu.
 
Inawezekana kutibika.Eleza japo kidogo ili tusaiduane,wewe/huyo mwenye shida hiyo imempata lini na chanzo chake ni kipi,kama ni kwa sababu ya umri pia tufahamu.
Hii shida imetokea baada ya kufanya kazi ngumu sana, siyo kwa sababu ya umri au nyingine.
nilipata kusoma sehemu kuwa kubeba mizigo kuna ukomo, (kwamba ndani ya lisaa kuna uzito fulani unapaswa kubeba, ukizidisha hapo matatizo kama hayo yanaweza kutokea.
kwahiyo chanzo cha hilo tatizo kilikuwa hicho
 
Hii shida imetokea baada ya kufanya kazi ngumu sana, siyo kwa sababu ya umri au nyingine.
nilipata kusoma sehemu kuwa kubeba mizigo kuna ukomo, (kwamba ndani ya lisaa kuna uzito fulani unapaswa kubeba, ukizidisha hapo matatizo kama hayo yanaweza kutokea.
kwahiyo chanzo cha hilo tatizo kilikuwa hicho
Hiyo inapona!
 
Back
Top Bottom