Tumfute machozi Freeman Mbowe, tusikubali aachie uenyekiti 2023. Ametupigania sana

Memento

JF-Expert Member
Jun 13, 2021
4,423
9,962
Kwenye nchi hii unaachane kumfuta machozi mtu kama Freeman Mbowe? Hata kama unamchukia kiasi gani ina maana aliyofanya na anayofanya hamuyaoni?

Freeman Mbowe hili ni jina linalopaswa kuwa kwenye kumbukumbu za kudumu nchi hii, huyu ni mpiganaji halisi hakuna vita ambayo hajawahi kushinda.

Freeman amezaliwa kwenye familia tajiri sana na yeye ni tajiri sana ila amekubali kuweka pembeni utajiri wake ili kuwazungumzia watu haki zao kwa gharama yoyote.

Ni tajiri gani angeweza ku-risk kama anavyofanya jabali Freeman? Hakuna.

Freeman amekubali kunyanyaswa, kupigwa, kutukanwa kila tusi na amekubali kupewa kesi zaidi ya 100 na kukaa jela zaidi ya mara 3 yote ili sisi wananchi tufikie nchi ya ahadi.

Hakuna utawala ambao Freeman hajateswa, hakuna ila kakubali yote hayo, tunataka nini tena?

Nawaomba tuungane kukataa mwenyekiti kuachia ngazi 2023. Simaanishi CHADEMA hakuna wa kutupeleka mbali zaidi, ila kwa kipindi hiki bado mwenyekiti Freeman tunamuhitaji sana.

Tumfute machozi Freeman, ana mengi amekubali kuteseka kwa ajili yetu.

Ninaomba wale wote wenye mapenzi mema na nchi hii tuungane tumfute machozi mwenyekiti hata kwa post yoyote au hashtag inayoonyesha kazi kubwa ambayo mwenyekiti Freeman ameifanya nchi hii.

Tumsaidie Freeman kushinda uchaguzi mkuu wowote utaokuja mbele yetu.

#freeman wewe ni jabali#
 
Hapana, kama ni kufutwa machozi itafutwe njia nyingine ya kumfuta hayo machozi, lakini kuhusu kupumzika, nashauri aachwe apumzike, yeye ndie ameamua kufanya hivyo japo anajua bado anaungwa sana mkono na wapenda mabadiliko, msiogope, iacheni Chadema iende phase nyingine, hakuna chenye mwanzo kikakosa mwisho, kama tunaogopa mabadiliko hivi basi bora CCM iendelee kututawala.
 
Hizi nguvu za kumfariji mtu mwenye mshahara wa zaidi ya 10+million amekuwa mbunge na mwenyekiti wa kambi ya upinzani zielekezwe kuwafariji na kuwatia moyo madaktari wanaokesha usiku na mchana walimu wanaofundisha kwenye mazingira magumu na askari wanaotulinda na Mali zetu.
 
Kuna wakati mtu anaandika kitu ambacho kwa fikira zake anaamini ni sahihi ila kiuhalisia hakina maana yoyote kwenye jamii inayo tuzungukuka

Kuna wakati viongozi wanaondoa mifumo imara ili watutawale daima

Kuna wakati viongozi wanatujaza upepo tuone bila wao hatuwezi kusonga mbele

Kuna wakati tunashabikia vitu ambavyo viko nje ya uwezo wa fahamu zetu
 
Imani yako ipo ktk mtu na sio mfumo, mtu hubadirika wakati wowote, leo unaweza kumuona wa maana kesho akabadirika na kuwa wa hovyo, kikubwa amini ktk mfumo sio mtu.

Marehemu Keneth Kaunda alifungwa jela sababu nakuamini ktk mfumo aliamini vila yeye Zambia haiwezi kuendelea, watu wakamchukia kila kona, ila kama angekuwa mjanja kama Nyerere hata asingejikuta yupo hatiani.

Hivyo hivyo kwa mbowe, muda ukifika aachie ngazi hakika tutamkumbuka.
 
Namkubali sana Mbowe, lakini sikubaliani na wewe, eti tumfute machozi! Mbowe ana maisha yake, na uenyekiti wa CHADEMA kwake ni sacrifice, yeye ndo anafuta wengi machozi! Labda ungesema Mbowe abakie kwenye nafasi yake aendelee kuwafuta wengi machozi! Na kuachia uenyekiti kwake ni kutuliwa mzigo, ambayo ni Sawa na kufutwa machozi!
 
Bila shaka ww ni Mbowe mwenyewe umeamua kuja kujitengenezea mazingira ya kuendelea na madaraka, au ni kibaraka wake ulietumwa na Mbowe uje utengeneze mazingira ya yeye kubadilisha mawazo ya kubaki kitini.

Hili halishangazi kwa sababu sio mara ya kwanza Mbowe kuwahadaa watu kuwa anataka kustaafu, afu baadae wanatafutwa wazee njaa kadhaa wanatengenezwa na kujifanya wanakuja na matamko ya kumtaka Mbowe aendelee kubaki madarakani. Marekani raisi hata akifanya mazuri vipi mwisho wake wa madaraka ukifika anatoka na kupisha wengine.
 
Wewe kama unataka kumfuta hayo machozi, unaweza kutumia njia nyingine unayo ona inafaa. Ila kwa sasa unatakiwa kuheshimu uamuzi wa mtu, ingawa pia umekuja kwa kuchelewa.
 
Magu Part 2 na wazee wa Atake Asitake. Alazimishweeeeee.

Organisms kwenye siasa na madaraka ni wale wale.
hahahaaa organism kwenye madaraka ?mbowqe ni zaidi ya dictator kama humjui ule uenyekiti umeondoa watu wengi sana iqal kama humjui utamuimbia mapambio hakuna mtu mbaya kwenye siasa kama mbowe
 
Freeman Mbowe ni mtu wa aina yake, ni mtu wa pekee sana! Amekuwa chanzo cha Neema na maisha mema kwa watu wengi sana! Ni mtu wa kuachilia na kusamehe sana! Yule aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai baadaye akawa mkuu wa Mkoa wa Mtwara, ndugu Gelasius Byakamwa alipokwenda na kikosi chake kuharibu miundombinu ya bustani ya mboga ya Mbowe (Green House) eti ipo kwenye vyanzo vya maji alinyamaza kimya lakini Mungu amelipa.

Huyo ndugu alipofanya hivyo mwendazake alifurahishwa sana na kitendo hicho na kumpandisha cheo kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara. Lakini Mungu kajibu kwa mtumwa na mtumaji. Vivyo hivyo kwa Sabaya.

Ndugu mmoja anaitwa Mchechu wa Shirika la Nyumba alikwenda na kikosi chake kubomoa kitega uchumi cha Mbowe cha Billicanas, Lakini Mungu akajibu. Nehemia Mchechu hadi leo hajulikani alipo.
 
Mlivyokosa haya wapinzani wa nchi hii, wakati wabunge wa CCM wanapigia Chapuo hayati Magufuli aendelee kuongoza mlipinga kwa nguvu zote, matusi na kejeli tuliyaona leo kwenu mnaona ni sawa, hakika hicho chama ndio baba wa uDikteta,

Halafu mwaota kupewa nchi.
 
Back
Top Bottom