Tumfanyeje Lowassa?

Kigarama

JF-Expert Member
Apr 23, 2007
2,492
1,230
Kwenye mijadala 100 ya kwenye jukwaa hili amini usiamini mijadala 98 ndani yake halikosi kutajwa jina la Edward Lowassa kwa mema, mabaya kwa kuungwa mkono au kwa kupingwa. Lowassa imethibitika kuwa ndiye nguzo ya siasa zetu hapa Tanzania. Ukimshambulia au kumsifia Lowassa ni lazima utavuta hisia (attention) za jamii ziwe chanya au hasi dhidi yako.

Leo hii Lowassa akiacha siasa kitakachofuatia ni mjadala mwingine kama aachwe apumzike au ashitakiwe. Ndani ya CCM makundi yanayotajwa ni ama wanaomuunga mkono Lowassa au wanaompinga, na nje ya CCM mwanasiasa anayetajwa kama atashindwa kirahisi au atawashinda wapinzani wake ni Lowassa. Inavyoonekana kwenye siasa za Tanzania kumuepuka Lowassa haiwezekani.

Lakini kama taifa tunatakiwa tutoke kwenye mkwamo huu wa jinamizi la Lowassa, kwani kwa hali ilivyo sasa inaonekana kama vile Lowassa ni "Control Machine" ya maisha yetu ya kisiasa. Tuamue kushughulika na Lowassa leo na milele (once for all) ili tubakie na kazi ya kuijenga nchi yetu.

Haiwezekani ionekane kama kwa nchi nzima Lowassa anao uwezo wa kufanya chochote halafu sisi kama taifa tunabaki kumwangalia, kulalamika na kuwayawaya kama swala aliyekoswakoswa na simba. Kama analimiki bunge, mahakama, Serikali na chama chake basi asitumiliki na tusiofaidika na mfumo aliouweka.

Kama hatuna cha kumfanya Lowassa basi tujue huko tuendako kama taifa hatuna heri hata kidogo!!
 
Kwenye mijadala 100 ya kwenye jukwaa hili amini usiamini mijadala 98 ndani yake halikosi kutajwa jina la Edward Lowassa kwa mema, mabaya kwa kuungwa mkono au kwa kupingwa. Lowassa imethibitika kuwa ndiye nguzo ya siasa zetu hapa Tanzania. Ukimshambulia au kumsifia Lowassa ni lazima utavuta hisia (attention) za jamii ziwe chanya au hasi dhidi yako.

Leo hii Lowassa akiacha siasa kitakachofuatia ni mjadala mwingine kama aachwe apumzike au ashitakiwe. Ndani ya CCM makundi yanayotajwa ni ama wanaomuunga mkono Lowassa au wanaompinga, na nje ya CCM mwanasiasa anayetajwa kama atashindwa kirahisi au atawashinda wapinzani wake ni Lowassa. Inavyoonekana kwenye siasa za Tanzania kumuepuka Lowassa haiwezekani.

Lakini kama taifa tunatakiwa tutoke kwenye mkwamo huu wa jinamizi la Lowassa, kwani kwa hali ilivyo sasa inaonekana kama vile Lowassa ni "Control Machine" ya maisha yetu ya kisiasa. Tuamue kushughulika na Lowassa leo na milele (once for all) ili tubakie na kazi ya kuijenga nchi yetu.

Haiwezekani ionekane kama kwa nchi nzima Lowassa anao uwezo wa kufanya chochote halafu sisi kama taifa tunabaki kumwangalia, kulalamika na kuwayawaya kama swala aliyekoswakoswa na simba. Kama analimiki bunge, mahakama, Serikali na chama chake basi asitumiliki na tusiofaidika na mfumo aliouweka.

Kama hatuna cha kumfanya Lowassa basi tujue huko tuendako kama taifa hatuna heri hata kidogo!!
Lowasa hastahili kuwa raisi japo anajua na ni jasiri kuongoza hii inatokana na kupenda kwake visa na visasi kitendo cha kumfanya vile mwakyembe sidhani iwapo atakua rais mbeya itaendelea kuwa sehemu ya Tanzania!!!Alafu atamshinda nani maana anaogopwa kama ukoma labda apindue nchi
 
Nashauri kama kweli anautaka uraisi aende kwenye media atangaze JK alihusikaje kwenye EPA na Richmond na jinsi alivyotumika,aeleze dhamira yake kuwa ni safi awaombe msamaha Mwakyembe na Mwandosya pamoja na wanambeya kwa ujumla wao na pia aondoke CCM ajiunge na M4C akiwa zigo la lawama kalitupa kwa JK hapo ataaminika tena na wabongo watamsamehe na kumpa umagogoni!!!Komaa lowasa my school mate pale Tabora...."Wanaumeee Eeeee"Nadhani unaikumbuka hii EL
 
Kashfa ya Richmond imemchafua sana EL. Namshauri aache siasa! apumzike Kijijini Monduli.Urais ni ndoto kwake kwa sababu maadui wake wakubwa wako magamba.Dhaifu alisema EL amepata ajali ya kisiasa! Alimaanisha ajali ya kisiasa ni mbaya sana mara kumi upate ajali ya gari.
 
Lowassa anapaswa kujiulaumu kwa kutooana mbali kiasi cha kujiruhusu kutumiwa na Kikwete. Lowassa kweli ana madoa tangu enzi za Mwalimu, lakini hili la kutumika kama nepi ya kusafisha uchafu wa Kikwete itamgharimu maisha yake yote. Kugombea urais japo ni haki ya kikatiba ya kila mtanzania, hili Lowassa asahau. Anaweza kulazimisha chama chake kumteua ili kishindwe vizuri ingawa anaamini kuwa pesa aliyochuma kwenye ufisadi inaweza kumletea ushindi kama mshirika wake Kikwete alivyotumia pesa ya EPA. Wakati umebadilika. Ni mihumu kulielewa hili hata kama hakubaliani nalo.
 
epa,richmond na zingine zote ilikua kwa kazi ya uchaguzi, hakula lowasa. Amebeba mzigo kwa makubaliano.
angeeleza hayo maPema ningemwelewa.though sijawahi kufikiria akiLini mwangu kuwa lowasa sio mwizi toka niielewe kauli ya mwlm jkn
 
mkuu Gwakisa Mwandule kumbe EL alisoma tabora skul?no wonder ni mtendaj mzuri,kwel atoke hadharan amchane dhaifu ajitoe magamban aombe msamaha alowazuru ajoin M4C then 2shirikiane kuwangoa magamba otherwise 2mpeleke the hague
 
Last edited by a moderator:
Kwenye mijadala 100 ya kwenye jukwaa hili amini usiamini mijadala 98 ndani yake halikosi kutajwa jina la Edward Lowassa kwa mema, mabaya kwa kuungwa mkono au kwa kupingwa. Lowassa imethibitika kuwa ndiye nguzo ya siasa zetu hapa Tanzania. Ukimshambulia au kumsifia Lowassa ni lazima utavuta hisia (attention) za jamii ziwe chanya au hasi dhidi yako.

Leo hii Lowassa akiacha siasa kitakachofuatia ni mjadala mwingine kama aachwe apumzike au ashitakiwe. Ndani ya CCM makundi yanayotajwa ni ama wanaomuunga mkono Lowassa au wanaompinga, na nje ya CCM mwanasiasa anayetajwa kama atashindwa kirahisi au atawashinda wapinzani wake ni Lowassa. Inavyoonekana kwenye siasa za Tanzania kumuepuka Lowassa haiwezekani.

Lakini kama taifa tunatakiwa tutoke kwenye mkwamo huu wa jinamizi la Lowassa, kwani kwa hali ilivyo sasa inaonekana kama vile Lowassa ni "Control Machine" ya maisha yetu ya kisiasa. Tuamue kushughulika na Lowassa leo na milele (once for all) ili tubakie na kazi ya kuijenga nchi yetu.

Haiwezekani ionekane kama kwa nchi nzima Lowassa anao uwezo wa kufanya chochote halafu sisi kama taifa tunabaki kumwangalia, kulalamika na kuwayawaya kama swala aliyekoswakoswa na simba. Kama analimiki bunge, mahakama, Serikali na chama chake basi asitumiliki na tusiofaidika na mfumo aliouweka.

Kama hatuna cha kumfanya Lowassa basi tujue huko tuendako kama taifa hatuna heri hata kidogo!!


598677_4751537345516_1048337149_n.jpg


LOL... SON this time DAD is HUNGRY OK... Politics is damn hard to Swallow
 
Anyongwe!

Mtu haadhibiwi kwa ushahidi wa kufikirika.
Kuna watu wameshikwa kwa ushahidi ulio timilifu na wanapeta...Chenge amekamatwa na mabilioni ya wizi benki. Tungekua na nia dhabiti ya kupinga ufisadi tuanzie hapo tulipo na ushahidi wa kutosha.
Lowasa angekua fisadi angeomba rushwa CityWater ili waendelee na mkataba wao.
 
Nashauri kama kweli anautaka uraisi aende kwenye media atangaze JK alihusikaje kwenye EPA na Richmond na jinsi alivyotumika,aeleze dhamira yake kuwa ni safi

Aisee, umemaliza kila kitu. Acha akina Pasco wadanganye wanajamvi kwamba Lowassa alibebeshwa mzigo siyo wake
 
Lowassa anapaswa kujiulaumu kwa kutooana mbali kiasi cha kujiruhusu kutumiwa na Kikwete. Lowassa kweli ana madoa tangu enzi za Mwalimu, lakini hili la kutumika kama nepi ya kusafisha uchafu wa Kikwete itamgharimu maisha yake yote. Kugombea urais japo ni haki ya kikatiba ya kila mtanzania, hili Lowassa asahau. Anaweza kulazimisha chama chake kumteua ili kishindwe vizuri ingawa anaamini kuwa pesa aliyochuma kwenye ufisadi inaweza kumletea ushindi kama mshirika wake Kikwete alivyotumia pesa ya EPA. Wakati umebadilika. Ni mihumu kulielewa hili hata kama hakubaliani nalo.

Nimeipenda hiyo ya "kulazimisha chama chake kimteue ili kishindwe vizuri". Natumia kimchina, kamata LIKE yako mkuu!
 
Kimya kingi kina mshindo mkuu na ukiona kobe kainama ujue anatunga sheria mh. Lowassa katika siasa ya nchi hii rekodi yake ni mzuri sana hasa katika uwajibikaji na hii ilijionesha dhahili alipojiuzu wadhafa wake kwa maslai ya nchi kwa wakati ule ambao serikali hii ya awamu ya nne ilikuwa bado changa.Katika hilo alionesha ujasiri wa hali ya juu sana,actually is very intelligent katika hili tusibishe kabisa maana angelikuwa mpumbavu angelopokalopoka tu hovyo ama kulaumulaumu tu huku na kule lakini wapi.Tukiachilia masuala ya ukanda,dini,kabila na rangi Mh.Lowassa he may be a good leader for future Tanzania we need,kwani aliyeumwa na nyoka akiguswa na jani tu lazima astuke so kwa yote wanayodhania kumtuhumu Mh.Lowassa katika awamu yake no body can corrupt public funds na hata wale watumishi wezi wote watakimbia ama kuogopa kufanya kazi za umma.Nia hayo tu.
 
Mtu haadhibiwi kwa ushahidi wa kufikirika.
Kuna watu wameshikwa kwa ushahidi ulio timilifu na wanapeta...Chenge amekamatwa na mabilioni ya wizi benki. Tungekua na nia dhabiti ya kupinga ufisadi tuanzie hapo tulipo na ushahidi wa kutosha.
Lowasa angekua fisadi angeomba rushwa CityWater ili waendelee na mkataba wao.

Misaada ya mamilioni ya pesa kwa makanisa anayatoa wapi yeye kama mtumishi wa umma?
 
Simpendi Lowassa lakini akiweza kupita yoote na kuibukia kuwa Rais
nitaheshimu Urais wake....

too much hate is harmfull

wapo watu wanamchukia Obama but wanaheshimu Urais wake
 
Back
Top Bottom