Kigarama
JF-Expert Member
- Apr 23, 2007
- 2,492
- 1,230
Kwenye mijadala 100 ya kwenye jukwaa hili amini usiamini mijadala 98 ndani yake halikosi kutajwa jina la Edward Lowassa kwa mema, mabaya kwa kuungwa mkono au kwa kupingwa. Lowassa imethibitika kuwa ndiye nguzo ya siasa zetu hapa Tanzania. Ukimshambulia au kumsifia Lowassa ni lazima utavuta hisia (attention) za jamii ziwe chanya au hasi dhidi yako.
Leo hii Lowassa akiacha siasa kitakachofuatia ni mjadala mwingine kama aachwe apumzike au ashitakiwe. Ndani ya CCM makundi yanayotajwa ni ama wanaomuunga mkono Lowassa au wanaompinga, na nje ya CCM mwanasiasa anayetajwa kama atashindwa kirahisi au atawashinda wapinzani wake ni Lowassa. Inavyoonekana kwenye siasa za Tanzania kumuepuka Lowassa haiwezekani.
Lakini kama taifa tunatakiwa tutoke kwenye mkwamo huu wa jinamizi la Lowassa, kwani kwa hali ilivyo sasa inaonekana kama vile Lowassa ni "Control Machine" ya maisha yetu ya kisiasa. Tuamue kushughulika na Lowassa leo na milele (once for all) ili tubakie na kazi ya kuijenga nchi yetu.
Haiwezekani ionekane kama kwa nchi nzima Lowassa anao uwezo wa kufanya chochote halafu sisi kama taifa tunabaki kumwangalia, kulalamika na kuwayawaya kama swala aliyekoswakoswa na simba. Kama analimiki bunge, mahakama, Serikali na chama chake basi asitumiliki na tusiofaidika na mfumo aliouweka.
Kama hatuna cha kumfanya Lowassa basi tujue huko tuendako kama taifa hatuna heri hata kidogo!!
Leo hii Lowassa akiacha siasa kitakachofuatia ni mjadala mwingine kama aachwe apumzike au ashitakiwe. Ndani ya CCM makundi yanayotajwa ni ama wanaomuunga mkono Lowassa au wanaompinga, na nje ya CCM mwanasiasa anayetajwa kama atashindwa kirahisi au atawashinda wapinzani wake ni Lowassa. Inavyoonekana kwenye siasa za Tanzania kumuepuka Lowassa haiwezekani.
Lakini kama taifa tunatakiwa tutoke kwenye mkwamo huu wa jinamizi la Lowassa, kwani kwa hali ilivyo sasa inaonekana kama vile Lowassa ni "Control Machine" ya maisha yetu ya kisiasa. Tuamue kushughulika na Lowassa leo na milele (once for all) ili tubakie na kazi ya kuijenga nchi yetu.
Haiwezekani ionekane kama kwa nchi nzima Lowassa anao uwezo wa kufanya chochote halafu sisi kama taifa tunabaki kumwangalia, kulalamika na kuwayawaya kama swala aliyekoswakoswa na simba. Kama analimiki bunge, mahakama, Serikali na chama chake basi asitumiliki na tusiofaidika na mfumo aliouweka.
Kama hatuna cha kumfanya Lowassa basi tujue huko tuendako kama taifa hatuna heri hata kidogo!!